Uzi wa waliopata mtoto wakiwa shule

rikiboy

JF-Expert Member
Joined
Feb 19, 2017
Posts
21,952
Reaction score
43,265
Katika maisha ya ujana hasa mahusiano kuna changamoto nyingi Sana tunakutana nazo.. Ilaa suala la MTU ulienae kwenye mahusiano kubeba Ujauzito na mwanaume hujajipanga Huwa linachanganya Sana akili na kuharibu mipangi mingi Sanaa...

Tupeane uzoefu juu ya Changamoto ulizopata pale ulipopata mtoto mapema hasa kipindi upo shule au chuo na namna gani ulizikabili ukizingatia hukuwa vizuri kiuchumi na labda hukutaka nyumbani wajue???? Karibuni
 
Haa ha noma Sana mkuu
 
Mkuu mbona hujatoa yako kwanza,Mara nyingi ukianzisha Uzi wenye lengo kama huu wako basi unaanzia kwako wengine tunatiririka
 
Mimi nilipata mtoto nikiwa mwaka wa kwanza, alikuja na baraka zake maana kila mishe niliyofanya ilitiki, pesa ikawa inaonekana, full heshima kitaa, changamoto kwa kweli zilikuwa za kawaida sana, jinsi alivyopatikana mtoto na upatikanaji wa pesa uliongezeka, ila alipofariki mishe zote zililala, mambo yakagoma kwenda full upweke.

Mtoto ana raha yake mkuu!
 
Kwangu haijawahi kunikuta ila kuna rafiki yangu wa karibu sana wakati tupo kidato cha nne alimpa ujauzito binti wa kidato cha pili mbaya zaidi yule binti baba yake alikuwa afisa elimu wa hiyo wila yetu.

Uzuri hazo taarifa za ujauzito zinamfikia msela tupo kwenye kumalizia mitihani ya kidato ya kidatp cha nne. Hivyo jamaa alipomaliza mtihani wa mwisho tu akasepa kwao bukoba huko binti alivyoona maeachwa kwenye mataa akamfahamisha baba yake.

Walimpompigia simu msela akadanganya yupo Uganda hivyo akirudi ataenda kwa mzee wayamalize.

Lakini mpaka leo hajawahi kumuona huyo mtoto aliyezaliwa wala hakuna mawasiliano na mzazi mwenzie kwa sababu alibadilisha namba ili kuogopa jela .
 
Daah pole Sana mkuu...!! Bhasi kweli alikuja na baraka zakee
 
Pole sana mkuu
 
Aisee "...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…