Uzinduzi wa Jukwaa la Uwekezaji Wanawake Kiuchumi Kata ya Makongo

Uzinduzi wa Jukwaa la Uwekezaji Wanawake Kiuchumi Kata ya Makongo

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301

UZINDUZI WA JUKWAA LA UWEZESHAJI WANAWAKE KIUCHUMI KATA YA MAKONGO

Mbunge Viti Maalum Wanawake Mkoa wa Dar Es Salaam na Mwanzilishi wa taasisi ya Tisha Mama Foundation, Mhe. Mhe. Janeth Elias Mahawanga amekuwa mgeni rasmi katika kuzindua rasmi Jukwaa la Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi Kata ya Makongo.

Mhe. Janeth Mahawanga ametoa pongezi nyingi kwa Serikali ya awamu wa sita kwa kutambua mchango wa Wanawake katika kukuza Uchumi wa Taifa na pato la Taifa kwa ujumla kwa kuendelea kuongeza fursa mbalimbali zinazozidisha chachu kwa Wanawake na Mabinti kupata mitaji ya shughuli zao mbalimbali za Kiujasiriamali.

"Ukiacha fursa ya mikopo ya Halmashauri, mikopo ya Wanawake, Vijana na Watu wenye mahitaji maalum kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum na sasa kuna hii fursa ya Majukwaa ya Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi."

"Niwaombe sana Wanawake na Mabinti tuzitumie hizi fursa kiufasaha lakini zaidi ya yote tuchape kazi ili fursa hizi ziwe na tija kwetu mtu mmoja mmoja, Familia zetu na Taifa letu." #Kamatafursatwendezetu #Wanawaketunaweza #TishaMamaFoundation

#TishaMama
#MamaVicoba
#ItazameDarKiutofauti
#Kaziiendelee

WhatsApp Image 2023-03-21 at 23.17.06.jpeg
WhatsApp Image 2023-03-21 at 23.17.06(1).jpeg
WhatsApp Image 2023-03-21 at 23.17.07.jpeg

 
Ni mambo haya ndio yamepelekea kuvuruga familia nyingi na ndoa kuvunjika. Leo hii ndani ya ndoa kunasababisha mwanamke na mwanamume.

Sio tena mke na mume ambao ni mwili mmoja. Badala ya kuzungumzia uwezeshaji FAMILIA tumekuwa wajinga mno kuongelea uwezeshaji MWANAMKE!

Halafu kesho utasikia, "iundwe tume kuchunguza kwa nini ndoa zinavunjika sana. " Tumerogwa!!!!
 
Ni mambo haya ndio yamepelekea kuvuruga familia nyingi na ndoa kuvunjika. Leo hii ndani ya ndoa kunasababisha mwanamke na mwanamume.

Sio tena mke na mume ambao ni mwili mmoja. Badala ya kuzungumzia uwezeshaji FAMILIA tumekuwa wajinga mno kuongelea uwezeshaji MWANAMKE!

Halafu kesho utasikia, "iundwe tume kuchunguza kwa nini ndoa zinavunjika sana. " Tumerogwa!!!!
Was*ng* sana hawa me huwa wananiboa kama nikiwa natazama tv nikiona huu us*ng* nabadili channel au nazima. Maana ni upumbavu kushabikia jambo ambalo halina faida kwenye jamii.
 
Back
Top Bottom