BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,165
Askofu Mwamakula atazindua kampeni kubwa ya "Matembezi ya Hiyari" katika Jiji la Dar es Salaam katika Mwezi Februari 2021 katika siku na tarehe itakayotangazwa. Kampeni hiyo inalenga kuuhamsisha umma kuhusu umuhimu wa kuunda Tume Huru ya Uchaguzi na kuandika Katiba Mpya. Utaratibu wa matembezi hayo utakuwa kama ifuatavyo:
1. Washiriki wanashauriwa kuvaa barakoa (masks) ili kujikinga na Covid 19.
2. Washiriki watakaotembea na Askofu watatakuwa katika makundi makundi ambapo kila kundi halitazidi watu 10 ambapo kutakuwa na umbali wa mita 100 kutoka kundi moja hadi lingine.
3. Kundi la Askofu halitazidi watu 20 watakaoambatana naye
4. Washiriki wengine watatakiwa kujipanga barabarani ambako Askofu atapitia wakiwa wamevalia barakoa wakiachiana umbali wa mita 1 kati ya mtu na mtu.
5. Barabara zitakazotumika ni Morogoro, Malamba Mawili-Kinyerezi, Goba-Mbezi, Bagamoyo, Uhuru, Nyerere, Morogoro, Shekilango, Kilwa Road, Umoja wa Mataifa, Azikiwe, Kawe, Kigamboni, Chang'ombe, Mandela, Tabata-Segerea, Tandale kwa Tumbo, Kawawa, Bibi Titi Mohammed, Lumumba, Msimbazi, Tandika, Sam Nujoma, nk.
6. Siku ya kwanza itakuwa katika Wilaya ya Ubungo katika Barabara ya Morogoro katika Manzese na Mbezi kwa Yusufu.
5. Utaratibu utafanyika ili Askofu pamoja na baadhi ya waalikwa maalum waweze kuhutubia mikutano ya hadhara katika viwanja vya Kawe, Machava, Tabata, Mwembe Yanga, Mbagala, Biafra, Chanika, nk.
6. Washiriki watakaoweza watavaa t-shirts na kofia maalum zenye ujumbe kuhusiana na matembezi. Wasioweza watavaa mavazi ye yote!
7. Pale ambapo itashindikana kuhutubia mkutano wa hadhara, Askofu atahitimisha kwa kunywa maji au chai pamoja na watembeaji.
8. Matembezi yatakuwa yanaanza saa 8:00 mchana na yatakuwa yakifanyika katikati ya wiki ili kutoa nafasi kwa waajiriwa kushiriki.
Baada ya kumaliza kuzindua katika Mkoa wa Dar es Salaam, Askofu na timu yake wataelekea katika Mikoa ya Songwe na Mbeya kabla ya kuelekea Mikoa mingine. Mikoa itakayopewa kipaumbele kuanza ni ile ambayo itakuwa imekamilisha maandalizi mapema. Mkoa wa Songwe umekuwa wa kwanza kumuomba Askofu kuanza nao hivyo atazindua Tunduma! Hata hivyo, Askofu atafika katika kila Mkoa na kila Wilaya na hivyo matembezi yatadumu kwa muda wa mwaka mzima.
Tarehe ya matembezi kwa kila sehemu, wilaya au mkoa itakuwa ikitangazwa siku tano kabla. Utaratibu na mpangilio wa matembezi unaweza kubadilika kulingana na mazingira ya sehemu husika.
Vyama vya siasa, na taasisi za kiraia vinatiwa moyo kuhamasisha watu kujitokeza kwa wingi na hata kusaidia katika uratibu na maandalizi.
Sambaza ujumbe huu kwa kila mtu.
Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula
1. Washiriki wanashauriwa kuvaa barakoa (masks) ili kujikinga na Covid 19.
2. Washiriki watakaotembea na Askofu watatakuwa katika makundi makundi ambapo kila kundi halitazidi watu 10 ambapo kutakuwa na umbali wa mita 100 kutoka kundi moja hadi lingine.
3. Kundi la Askofu halitazidi watu 20 watakaoambatana naye
4. Washiriki wengine watatakiwa kujipanga barabarani ambako Askofu atapitia wakiwa wamevalia barakoa wakiachiana umbali wa mita 1 kati ya mtu na mtu.
5. Barabara zitakazotumika ni Morogoro, Malamba Mawili-Kinyerezi, Goba-Mbezi, Bagamoyo, Uhuru, Nyerere, Morogoro, Shekilango, Kilwa Road, Umoja wa Mataifa, Azikiwe, Kawe, Kigamboni, Chang'ombe, Mandela, Tabata-Segerea, Tandale kwa Tumbo, Kawawa, Bibi Titi Mohammed, Lumumba, Msimbazi, Tandika, Sam Nujoma, nk.
6. Siku ya kwanza itakuwa katika Wilaya ya Ubungo katika Barabara ya Morogoro katika Manzese na Mbezi kwa Yusufu.
5. Utaratibu utafanyika ili Askofu pamoja na baadhi ya waalikwa maalum waweze kuhutubia mikutano ya hadhara katika viwanja vya Kawe, Machava, Tabata, Mwembe Yanga, Mbagala, Biafra, Chanika, nk.
6. Washiriki watakaoweza watavaa t-shirts na kofia maalum zenye ujumbe kuhusiana na matembezi. Wasioweza watavaa mavazi ye yote!
7. Pale ambapo itashindikana kuhutubia mkutano wa hadhara, Askofu atahitimisha kwa kunywa maji au chai pamoja na watembeaji.
8. Matembezi yatakuwa yanaanza saa 8:00 mchana na yatakuwa yakifanyika katikati ya wiki ili kutoa nafasi kwa waajiriwa kushiriki.
Baada ya kumaliza kuzindua katika Mkoa wa Dar es Salaam, Askofu na timu yake wataelekea katika Mikoa ya Songwe na Mbeya kabla ya kuelekea Mikoa mingine. Mikoa itakayopewa kipaumbele kuanza ni ile ambayo itakuwa imekamilisha maandalizi mapema. Mkoa wa Songwe umekuwa wa kwanza kumuomba Askofu kuanza nao hivyo atazindua Tunduma! Hata hivyo, Askofu atafika katika kila Mkoa na kila Wilaya na hivyo matembezi yatadumu kwa muda wa mwaka mzima.
Tarehe ya matembezi kwa kila sehemu, wilaya au mkoa itakuwa ikitangazwa siku tano kabla. Utaratibu na mpangilio wa matembezi unaweza kubadilika kulingana na mazingira ya sehemu husika.
Vyama vya siasa, na taasisi za kiraia vinatiwa moyo kuhamasisha watu kujitokeza kwa wingi na hata kusaidia katika uratibu na maandalizi.
Sambaza ujumbe huu kwa kila mtu.
Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula