#COVID19 Uzoefu wangu kwenye chanjo ya COVID-19 leo

#COVID19 Uzoefu wangu kwenye chanjo ya COVID-19 leo

The Good

Senior Member
Joined
May 26, 2010
Posts
185
Reaction score
119
Leo nimebahatika kupata chanjo katika kituo cha jirani. Vitu viwili ambavyo nimeviona na nadhani kuna haja ya wahusika kuvifanyia kazi ni hivi

1. Booking
Jana nilifanya on-line booking na kuweka tarehe ya leo katika kituo nilichochagua
Nilipofika kituoni nikakuta hawana taarifa yoyote ya on-line booking na kila kitu unaanza upya.
Ni vizuri wahusika wakaliangalia hili maana huko tuendako iwapo watu watajitokeza kwa wingi kutakuwa na ucheleweshaji mkubwa kwa watu kujaza taarifa zao upya

2. Cheti
Cheti kinachotolewa hakina ubora kabisa. Nilitegemea kwa kuwa nilifanya on-line booking basi taarifa ningeziona na baada ya chanjo ningepata electronic certificate chenye barcode ambayo itamwezesha mtu yoyote kuhakiki uhalisia wa cheti pindi kitakapohitajika
Kwa cheti hiki ambacho hakina security feature yoyote very soon kila mtu atakuwa nacho na tatizo litakuwa kwa watanzania watakaokuwa wanasafiri kwenda nchi zinazohitaji ushahidi wa chanjo

Cheti chetu nina mashaka hakitakuwa kinatambulika

Naomba haya mawili wahusika wayafanyie kazi ili kuongeza ubora wa huduma na kuifanya kuwa inayotambulika kimataifa
 
Vipi Watu wameitikia wito wa kuchanjwa kwa wingi?!
 
Kiukweli… cheti hakuna shida

abs maybe in the future itakua integrated kuwa inajazwa Kwenye Ile yellow card za chanjo

Ila online booking imefeli kabisa
 
Vipi Watu wameitikia wito wa kuchanjwa kwa wingi?!
Nadhani wameitikia vya kutosha. Hii awamu ya watu wenye umri mkubwa na wagonjwa. Hao wote wako hatarini na mwitikio kwa kituo nilichochanja ni mzuri
Labda tusubiri wahusika after a week or so watupe mrejesho kitaifa
 
wagonjwa wa;
1.KISUKARI
2.UKIMWI
3.SARATANI
4.PRESHA
5TB
wapo kwenye hatari kubwa sana ya kupoteza maisha ktk wimbi hili la 3 la Corona.
chukua tahadhari pata chanjo.
Chanjo hii inawashambulia sana kundi hili

Au mmepanga kuwamaliza?
 
wagonjwa wa;
1.KISUKARI
2.UKIMWI
3.SARATANI
4.PRESHA
5TB
wapo kwenye hatari kubwa sana ya kupoteza maisha ktk wimbi hili la 3 la Corona.
chukua tahadhari pata chanjo.
Wewe ndo Mungu unaamua Nani afe na Nani asife?

Watu waliokufa zaidi ya 4m. Walikuwa na matatizo hayo?

Kwani chanjo inazuia maambukizi na vifo? Kwanini wanaendelea kuvaa barakoa hata waliochanjwa Kama kuchanja ni Kinga?

Acha upotoshaji.
 
wagonjwa wa;
1.KISUKARI
2.UKIMWI
3.SARATANI
4.PRESHA
5TB
wapo kwenye hatari kubwa sana ya kupoteza maisha ktk wimbi hili la 3 la Corona.
chukua tahadhari pata chanjo.
Wewe ndo Mungu unaamua Nani afe na Nani asife?

Wato waliokufa zaidi ya 4m. Walikuwa na matatizo hayo?
Kwani chanjo inazuia maambukizi na vifo?, Kwanini wanaendelea kuvaa barakoa hata waliochanjwa Kama kuchanja ni Kinga?

Acha upotoshaji
Vipi Watu wameitikia wito wa kuchanjwa kwa wingi?!
Hili swali jibu lake litakuwa watu wengi ili nchi iendelee kupata inachokihitaji hata Kama ni wachache.

Ukiuliza aliyechanjwa atasema wengi maana yeye tayari ameshalikoroga na kulinywa,anatamani nawe ulinywe muwe wengi,ili lolote likitokea kifo Cha wengi ,..
 
Wewe ndo Mungu unaamua Nani afe na Nani asife?

Watu waliokufa zaidi ya 4m. Walikuwa na matatizo hayo?

Kwani chanjo inazuia maambukizi na vifo?, Kwanini wanaendelea kuvaa barakoa hata waliochanjwa Kama kuchanja ni Kinga?

Acha upotoshaji.
huna haja ya kupaniki, kama una kisukari chukua tahadhari maana hii delta inalamba kweli sio masihara, tumetoka kuzika zaidi ya watu 4 ndani ya wiki hii.
 
Nadhani wameitikia vya kutosha. Hii awamu ya watu wenye umri mkubwa na wagonjwa. Hao wote wako hatarini na mwitikio kwa kituo nilichochanja ni mzuri
Labda tusubiri wahusika after a week or so watupe mrejesho kitaifa
Si kweli
 
tuendelee kuchukua tahadhari hata kama ulichanjwa chukua tahadhari, vaaa barakoa kwa usahihi, nawa mikono, epuka misongamano.
zingatia.
ukifa unamekufa ww.jilinde
 
Uzuri wa wabongo, unaweza kuta wapinga chanjo ni waliowahi vituoni kupigwa chanjo..

Wabongo tuna degree za unafiki ,wewe wasikilize tu kwamba chanjo hazifai wakati nyuma ya pazia ndio wa kwanza kufika vituoni.
 
huna haja ya kupaniki, kama una kisukari chukua tahadhari maana hii delta inalamba kweli sio masihara, tumetoka kuzika zaidi ya watu 4 ndani ya wiki hii.
Unajua kipindupindu kilivyokuja kilikuwa kinachukua wangapi? Vipi UKIMWI ulikuwa unachukua wangapi? Malaria unajua inachukua wangapi kwa siku! Leo hata uje na prom.ya Corona?
 
Nadhani wameitikia vya kutosha. Hii awamu ya watu wenye umri mkubwa na wagonjwa. Hao wote wako hatarini na mwitikio kwa kituo nilichochanja ni mzuri
Labda tusubiri wahusika after a week or so watupe mrejesho kitaifa
Mkuu watu wa kawaida ambao siyo wagonjwa,siyo wahudumu wa afya wala hawana umri mkubwa wanapokelewa pia?
 
Back
Top Bottom