Uzoefu wetu na India: Kwanini wafanyabiashara wanaagiza mazao kutoka nje ya nchi?

Uzoefu wetu na India: Kwanini wafanyabiashara wanaagiza mazao kutoka nje ya nchi?

Joined
Jun 1, 2021
Posts
99
Reaction score
104
Wadau wa Biashara na Ujasiriamali,

Tumeona humu kuna wazoefu wa biashara hizi za mazao ya kilimo, bila shaka ni sahihi kuleta jambo hili kwenu ili tubadilishane uzoefu.

Pichani ni mzigo wa nafaka za mahindi uliagizwa na mteja wetu wiki kadhaa zilizopita. Mzigo huu ulitokea nchini India na tukausafirisha hadi mkoani Arusha kwenye kiwanda (jina limehifadhiwa) kikubwa tu.

Je, ni bidhaa gani nyingine huagizwa kwa wingi kutoka India? Ni kwanini baadhi ya wafanyabiashara wanaagiza mazao ya kilimo nje licha ya kufahamika kuwa hapa nchini pia zinazalishwa nafaka kwa wingi?

Sisi kama wadau wa usafirishaji, tuna utayari wa kusafirisha pia bidhaa zinazotokea nchini kwenda nje ya nchi ili kukuza soko la bidhaa zetu. Kama hapa kuna wadau wanaofanya biashara ya kutuma mizigo nje ya nchi, nao tungependa kupata maoni yao.

E8REucgXIAsfZSC.jpg


E8REuNsXoAQ2utm.jpg
 
Kama ambavyo mnawasaidia watanzania kununua bidhaa nje ya nchi na kuwasafirishia je mnajihusisha pia na kuwatafutia masoko nje ya nchi ya bidhaa zao na kuwasafirishia???
 
Kama ambavyo mnawasaidia watanzania kununua bidhaa nje ya nchi na kuwasafirishia je mnajihusisha pia na kuwatafutia masoko nje ya nchi ya bidhaa zao na kuwasafirishia???

Swali zuri Bachelor. Jibu ni ndiyo, moja ya majukumu yetu ni kutangaza bidhaa za ndani kwa masoko ya nje na wadau wetu tunaoshirkiana ili kukuza biashara baina ya Tanzania na nchi za nje.
 
Hata Baresa huwa analeta meli ya mahindi na ngano, tuchunguze shida nini kwa haya yetu. Mayai ya kuku pia nasikia tunanunua Kenya. Sasa tuchunguze huko wanafuata unafuu wa bei au ubora? Kisha hayo majibu tuyafanyie kazi, tuachane na mazoea
 
Hata Baresa huwa analeta meli ya mahindi na ngano, tuchunguze shida nini kwa haya yetu. Mayai ya kuku pia nasikia tunanunua Kenya. Sasa tuchunguze huko wanafuata unafuu wa bei au ubora? Kisha hayo majibu tuyafanyie kazi, tuachane na mazoea

Wanachofanya sio ustaarabu japo kwa juu juu itaonekana ni jambo halali sana lakini kufanya hivyo wanahujumu sarafu ya Kitanzania,,,, mahindi ni mengi sana katika nchi hii mpaka hamna sababu ya kwenda kununua nje ya TZ
 
Nje wanafanya kitu kinachoitwa 'massive production' kutokana na teknolojia waliyonayo na kupelekea bei kwa kila 'unit' kupungua. Kinachowavutia wengi kwenda nje,ni kutokana na bei kuwa chini na uhakika wa kupata mzigo mkubwa hasa pale utakapohitajika. Viwanda vinaingia mikataba na wazalishaji wa uhakika ili utengenezaji wa bidhaa uendelee.
 
Nje wanafanya kitu kinachoitwa 'massive production' kutokana na teknolojia waliyonayo na kupelekea bei kwa kila 'unit' kupungua. Kinachowavutia wengi kwenda nje,ni kutokana na bei kuwa chini na uhakika wa kupata mzigo mkubwa hasa pale utakapohitajika. Viwanda vinaingia mikataba na wazalishaji wa uhakika ili utengenezaji wa bidhaa uendelee.
Ok, kama alivyokuwa anazalisha sumri, naona hizo fursa zinahitaji uwekezaji mkubwa
 
Back
Top Bottom