VENGU (Joseph Shamba) anaumwa, kalazwa Muhimbili tumuombee na kumjulia hali

VENGU (Joseph Shamba) anaumwa, kalazwa Muhimbili tumuombee na kumjulia hali

Pole vengu lakini ni nini hasa chanzo cha kulazwa? I mean anaumwa ni nini?
 
nakushukuru Rais Kikwete kwa Moyo wako wa Huruma kwa kumjulia Mgonjwa Josef hali. Inaleta tumaini na faraja kwa tunaompenda msanii wetu. Asante kwa kutoa muda wako kwa jambo hilo ambalo hata familia ya Vengu wamepata faraja. Mheshimiwa, Vengu ndio alikuwa mzima wa afya akifanya kazi yake na kutuburudisha, ghafla tunasikia yuko hoi kiasi hicho, hivyo kama inawezekana kupata tiba pengine ninaomba naye apatiwe. Mungu akubariki Mheshimiwa Rais na uendelee kuwa na moyo huo wa kuwatia faraja wagonjwa.
 
Nawasalimu wote hasa wale wenye moyo wa huruma na upendo kwa wenzetu wahitaji. Nimekwenda Muhimbili Jana kwenye Wodi ya Mwaisela namba 1. Lengo langu lilikuwa kumjulia hali Msanii wa Komedi VENGU baada ya kutokumuona kwenye kipindi muda mrefu na kusikia amelazwa Muhimbili.

Niliwakuta Ndugu zake ambao walinikaribisha kwa upendo katika kumjulia hali Ndugu yao. Jamani kusema ukweli Yule kijana anaumwa na anahitaji Sala na Maombi yetu. Hatambui mtu wala hawezi kuongea. Waliniambia kwa sasa wanashukuru mungu ana nafuu baada ya kukaa ICU muda mrefu tangu Masanja alivyokuwa anasema Jembe lake linaumwa bila kufafanua.

Nawaombeni mwenye nafasi , hali na mali akamjulie hali Kijana huyu. Alituburudisha wengi kwa USANII wake wa KOMEDI tulicheka alipokuwa Mzima. Na sasa tukamuone hospitali kwani ni jambo la dhawabu kumuona mgonjwa. Wengi labda walikuwa hawajui kalazwa wapi ni MUHIMBILI, Mwaisela WARD 1.

Labda tunaweza kuomba serikali iingilie kati Ugonjwa wake naye wampeleke INDIA ili arudi Chuoni na Kazini kwake. Mungu amnyoshee mkono wake wa uponyaji Josef Shamba.

Amen.

Mungu fanya kitu..huyu jamaa uwa ananifurahisha akiigiza kama Mrema...CCM wampeleke India maana ni mwanachama wao..Namuombea sana apone jamani...
 
Back
Top Bottom