Viashiria hatari kwa Mama Wajawazito

Viashiria hatari kwa Mama Wajawazito

bryan2

JF-Expert Member
Joined
Jun 8, 2016
Posts
3,323
Reaction score
4,679
Serikali yetu kushirikiana na Wizara ya Afya wakiwa na mkakati wa kupunguza/kudhibiti/kuzuia Kabisa vifo vya mama wajawazito sio mbaya tukiangalia dalili za hatari kwa mama wajawazito.

Hizi ni dalili ambazo Mama mjamzito ukiziona na lazima utafute ushauri wa haraka au endapo Drs/nurses ameziona ni vyema kuchukua tahadhari mapema ikiwa na pamoja kama Mama anahudhuria Clinic Zahanati na vyema akashauriwa ajifungulie Hospitali kubwa.

Dalili hizo japo kwa kifupi ni kama vile...

Shinikizo la damu zaidi ya 140/90mmhg

Kuvimba miguu(edema)

Kukuta protein/albumin kwa wingi kwenye Mkojo

Uwingi wa damu chini 8.5gdl(anaemia)

kutokwa na damu kabla ya 28wks na baada ya 28wks kabla ya muda wa kujifungua.

maumivu makali ya chembe ya moyo,kichwa,kizunguzungu,uoni hafifu(imminent eclampsia)

Kupata degedege(convulsion) ni dalili za kifafa cha mimba(eclamspia)

Urefu chini 150cm.

maumivu ya makali ya tumbo.

Kutohisi/kutosikia mtoto anacheza na huku alikua akicheza.

Kutokwa na uchafu usioleweka wenye harufu kali maeneo ya siri.

Homa kali.

ujauzito kwa kwanza zaidi ya miaka 35.

ujauzito chini ya miaka 20....nk

TUZUIE VIFO VYA WAMAMA WAJAWAZITO KWA KUCHUKUA TAHADHARI MAPEMA PINDI TUONAPO VIASHIRIA VYA HATARI.

asanteni.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom