willzkichaa
JF-Expert Member
- Feb 21, 2013
- 422
- 190
Habari wapendwa!
Hapa naomba ku sharevaina nyingine ya chakula cha ki- bachelor na cha fasta kidogo.
Naamini sio muda wote unakua na mood ya kupika ila unakuta una nenge/gwanda/njaa na ukahitaji msosi wa fasta na pia ukizingatia vitambi na presha tunaziepuka. Leo nawaletea pishi la haraka na lililojaa virutubisho vya kutosha. Tuanze kazi...
Mahitaji ni viazi vitamu,

Karoti, chumvi na sukari

Maandalizi;
Menya viazi na uvikate katika ukubwa utakaoupendelea. Na kisha tia kwenye maji na uoshe kwani vikipigwa na upepo au ubaridi huwa vinaunda kama utando mweusi.

Kata karoti katika maumbo madogo (usiisage)

Chemsha viazi na tia chumvi (weka maji mengi kiasi) kisha funika viive

Na vikianza kuiva. Mwaga maji na uweke masafi (hapa weka kiasi na ikibidi yasipite kimo cha wingi wa viazi) maji yakianza pungua weka nazi na usifunike kwani tui litakatika. Pitisha mwiko kuchanganya nazi kote. Kisha acha kiendelee kuiva.

baada ya dakika kumi weka sukari (kama utapendelea) na karoti ulizoziandaa.

Hapo acha maji yapungue na yatajitengeneza mchuzi/supu yenyewe. Ila ukiona supu nyepesi waweza ponda viazi vilaini vilivyomo ndani kuongeza uzito wake.

Hapo acha kiive na baada ya dakika 15 waweza kuepua na ku serve.

P.S. Hicho ni chakula cha watu watatu na kinalika hadi asubuhi. Viungo na mahitaji
weka upendavyo. Karibuni.
Hapa naomba ku sharevaina nyingine ya chakula cha ki- bachelor na cha fasta kidogo.
Naamini sio muda wote unakua na mood ya kupika ila unakuta una nenge/gwanda/njaa na ukahitaji msosi wa fasta na pia ukizingatia vitambi na presha tunaziepuka. Leo nawaletea pishi la haraka na lililojaa virutubisho vya kutosha. Tuanze kazi...
Mahitaji ni viazi vitamu,

Karoti, chumvi na sukari

Maandalizi;
Menya viazi na uvikate katika ukubwa utakaoupendelea. Na kisha tia kwenye maji na uoshe kwani vikipigwa na upepo au ubaridi huwa vinaunda kama utando mweusi.

Kata karoti katika maumbo madogo (usiisage)

Chemsha viazi na tia chumvi (weka maji mengi kiasi) kisha funika viive

Na vikianza kuiva. Mwaga maji na uweke masafi (hapa weka kiasi na ikibidi yasipite kimo cha wingi wa viazi) maji yakianza pungua weka nazi na usifunike kwani tui litakatika. Pitisha mwiko kuchanganya nazi kote. Kisha acha kiendelee kuiva.

baada ya dakika kumi weka sukari (kama utapendelea) na karoti ulizoziandaa.

Hapo acha maji yapungue na yatajitengeneza mchuzi/supu yenyewe. Ila ukiona supu nyepesi waweza ponda viazi vilaini vilivyomo ndani kuongeza uzito wake.

Hapo acha kiive na baada ya dakika 15 waweza kuepua na ku serve.

P.S. Hicho ni chakula cha watu watatu na kinalika hadi asubuhi. Viungo na mahitaji
weka upendavyo. Karibuni.