Vibaraka wa mabeberu tambueni kuwa Tanzania ni dola huru, ina mamlaka kuamua iwalinde namna gani raia wake

Vibaraka wa mabeberu tambueni kuwa Tanzania ni dola huru, ina mamlaka kuamua iwalinde namna gani raia wake

Nyankurungu2020

JF-Expert Member
Joined
Oct 2, 2020
Posts
4,170
Reaction score
6,757
Ibara ya 1 ya katiba ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania (JMT) imetamka wazi kuwa Tanzania ni dola huru yenye mamlaka yake ya kujitawala.

Kwa mantiki hii rais wa JMT ana mamlaka ya kuwalinda raia na taifa zima la Tanzania bila kuingiliwa na ushawishi toka mahala popote.

Tambueni kuwa Tanzania ina mamlaka ya kuchagua kama Chanjo dhidi ya Covid 19 zinafaa au hazifai. Tambueni kuwa Tanzania ina mamlaka ya kuwaaambia raia wake wawe makini juu ya matumizi ya barakoa zisizo na mashaka au la.

Hakuna haja nyie vibaraka msio na mbele wala nyuma kuanza kuinanga Tanzania kuwa inapuuza kuwepo kwa Covid 19 hapa Tanazania. Kisa tu mnalindwa na mabeberu wanaowapa hifadhi huko ughaibuni.

Hii ni dola huru, ambayo mkuu wake wa nchi ana mamlaka ya kuamua ailinde vipi hii dola na raia wake.

My take; kuweni makini hii ni Tanzania, maslahi yenu ya kisiasa yatawatokea puani na mtaumbuka bure.
 
Hivi huwa hata mnajua kinachoendelea duniani kabla ya kuleta uzi humu? Mkuu Samahani naomba uniambie ni Taifa gani limeilazimisha Tz kutumia chanjo? Au ushauri ni shurutisho? Pathetic
Vibaraka wa mabeberu.
 
Back
Top Bottom