Vichoma nguo ni mboga?

Crispin Nyoni

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2012
Posts
413
Reaction score
90
Jamani niko ugenini wenyeji wangu wamepika vichoma nguo kabla havijaota miba vikiwa vidogo sana wamekatakata kama mchicha wameunga kwa karanga.

Je nile ni salama kwa afya?
 
Jamani niko ugenini wenyeji wangu wamepika vichoma nguo kabla havijaota miba vikiwa vidogo sana wamekatakata kama mchicha wameunga kwa karanga. Je nile ni salama kwa afya?

Wageni wengine tabu sana. Umekuta wenzio wanakula na wewe kula tu hapo kibaya kiko wapi?. Argh!
 
Vichoma nguo ni vitu gani tena Bajameni?
 
Ndio tatizo lenu kuzoea chips mayai, ------- kabisa! Hio ni mboga Tamu sana lazima nikienda home Mama yangu aniandalie na nyanya chungu kwa ugali lainiiiii. Ndio maana akina Elli wetu hawahitaji kunywa supu ya pweza!!!!!
 
Last edited by a moderator:
Ndio tatizo lenu kuzoea chips mayai, ------- kabisa! Hio ni mboga Tamu sana lazima nikienda home Mama yangu aniandalie na nyanya chungu kwa ugali lainiiiii. Ndio maana akina Elli wetu hawahitaji kunywa supu ya pweza!!!!!

Mkuu natumia "like" ningegonga "simu". Umekuta wenyeji wako wanakula ingekuwa na madhara ungewakuta? Bibi yangu aliniambia kuwa inatibu hadi vidonda vya tumbo na inakausha vidonda haraka sana. Unapokea mgeni kama huyu balaa.
 
Last edited by a moderator:
Vichoma nguo ni vitu gani tena Bajameni?

Ukipita porini huwa kuna mmea fulani hivi unachoma miba zake kwenye nguo. Nyakati za mvua kama hizi kwenye shamba la mahindi vinamea sana. Ni chakula pia cha ng'ombe na nguruwe. Ni mboga tamu sana we acha tu.
 
Haya ndio madhara ya kuzoea chips na yai, ukiwa mikoani kuna raha yake kula vyakula vya asili.
 
Naomba 'mutuwekee' picha ya "vichoma nguo"!
 
Kama mie sili, kama ni ugali bora waniletee maziwa, kama wali narumanga.

Matembele yenyewe siku ya kwanza yalinitoa jasho, nikawaza inakuwaje tunakula marando? Nikitafuna naskia yananata kama tope la mfinyanzi, ilikuwa tabu. SIku hizi nimezoea tena naskia matamu tu, ila nisiyatafune saaaana.
 
Huwezi kufa pia ni mboga maarufu sana kula
 
tuwekeeni picha basi

Mkuu jinsi wa kuweka picha kwa sisi tunaotumia simu shughuli. Pia kujua jina lake kwa kingereza sijajua kabisa. Ila usijali kuna wataalam watajua jinsi ya kuingiza hapa. Ila nadhani ni mboga ya porini ya pekee yenye tiba kubwa zaidi
 
Jamani niko ugenini wenyeji wangu wamepika vichoma nguo kabla havijaota miba vikiwa vidogo sana wamekatakata kama mchicha wameunga kwa karanga. Je nile ni salama kwa afya?

Kama unawasiwasi, subiria waanze kula, ikipita kama dakika kadhaa hivi hawajadhurika na wewe kula!
 
Kama unawasiwasi, subiria waanze kula, ikipita kama dakika kadhaa hivi hawajadhurika na wewe kula!

Sana tu. yanaongeza damu balaa
Tz kuna mboga kibao kwetu had I manyoya ya kuku tunarost tunalia chapati au tunapata juice
 
Mkuu natumia "like" ningegonga "simu". Umekuta wenyeji wako wanakula ingekuwa na madhara ungewakuta? Bibi yangu aliniambia kuwa inatibu hadi vidonda vya tumbo na inakausha vidonda haraka sana. Unapokea mgeni kama huyu balaa.

sure mkuu vichoma nguo hutibu vidonda aina zote hasa vidonda vinavyotoa damu kwa wanatokea BK mtanisaidia maana hukausha vidonda haraka
Na hukausha vidonda vya tumbo haraka hili nimeona kwa mdogo wangu imesaidia sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…