Vichwa vya habari vya magazeti yetu vinaanza kubadilika

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011

Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye amesema Rais Samia Suluhu Hassan ameanza vizuri kwa kutoa maagizo yanayoliondoa Taifa kwenye kutumia mabavu na kujielekeza kwenye kutumia akili katika ukusanyaji kodi bila kuathiri walipakodi.

Mbali na hivyo, Nape alisema pia Rais Samia ameonyesha nia ya kuliongoza Taifa kwa kuwatendea haki Watanzania, hasa alipoitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kuziangalia na ikiwezekana kuzifuta kesi zisizo na msingi wala uhalali ili kuleta haki.

Mwezi mmoja uliopita usinge thubutu kusoma Nape amchambua Rais John Magufuli.
 
Eti Kuna watu wanategemea jipya kutoka kwa mama wakati nyani walewale ukoo uleule
 
Eti Kuna watu wanategemea jipya kutoka kwa mama wakati nyani walewale ukoo uleule
Awamu iliyokwisha ilikuwa ni Unchanted Territory..., Yaani haieleweki eleweki..., bora hata kama ni uozu huu, utakuwa uozo tuliouzoea ule ilikuwa kesho hatuji una-mutate na kuleta uozo zaidi kwa kiwango kipi
 
Wanasiasa sio wa kuwaamini kabisa...sasaivi hamis kigwa anavaa barakoa na anataka chanjo..
 
Nape alisema pia Rais Samia ameonyesha nia ya kuliongoza Taifa kwa kuwatendea haki Watanzania, hasa alipoitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kuziangalia na ikiwezekana kuzifuta kesi zisizo na msingi wala uhalali ili kuleta haki.
Hapa inatakiwa uangalifu mkubwa, baadhi ya watumishi watatumia mwanya huu kuwataka rushwa hao waliodhurumiwa haki zao kwa kuwekwa ndani pasipo hatia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…