Video aliyorusha Miss World kuhusu hali ya umaskini Tanzania; Mama Salma na wenza wa viongozi wa Tanzania bado wanaona ni sahihi kulipwa mabilioni?

Video aliyorusha Miss World kuhusu hali ya umaskini Tanzania; Mama Salma na wenza wa viongozi wa Tanzania bado wanaona ni sahihi kulipwa mabilioni?

Wamemchangia 120 million kumchukulia fomu
Hawajitambui na nimeshangaa sana PM anasizitiza fomu ya uchaguzi ni moja tu.this is injustice and purely unfair.Nini maana ya demokrasia.tunarudi kwenye zama za picha na kivuli.
 
Mkuu;

Hoja ya yako sio video ya huyo Miss world ila umejiegesha kwenye hiyo habari ili umseme mama Salma Kikwete.

Hii inaonesha ni jinsi gani huna uelewa mzuri wa haki, madaraka, kazi na majukumu ya bunge na mbunge.

Pia huna taarifa sahihi kuhusu taratibu na hatua za kutunga na kupitisha sheria bungeni na kwa kwa ujumla namna bunge linavyojiendesha.

Nakushauri upitie katiba na kanuni za bunge kabla ya kunyoshea watu vidole!

Mheshimiwa Salma kama mbunge alitumia haki yake kupeleka hoja hiyo bungeni, ikapolewa na kuandaliwa kupitia ofisi ya mwanasheria Mkuu wa serikali na kurudishwa bungeni ambapo ilipitishwa na wabunge wengi bungeni.

Kosa lake liko wapi?? Tupunguze chuki!
Pia na wewe uelewe hoja hiyo hakuipenyesha from nowhere bali kulikuwa na backing na kwa yeye ni bora angeisogeza kupitia kwa wabunge wengine.si kweli mwandishi hajui namna mchakato wa kutunga sheria inavyopitia bali hiyo skeptic yako tu.
 
Vile Vita Vya kupambana na ujinga ,Maradhi na umasikini aliyoianzisha Hayati Mwalimu JK Nyerere vinaendelea au Tumeipata ushindi tayari, au ndiyo tumepikwa knockout kama ya Nganou
 
Miss world ni binti mdogo aliyezaliwa masafa ya mbali na Tanzania. Alipofika Tanzania miaka minne iliyopita alitembelea Arusha na kukuta familia zisizo na uwezo wa mlo wa siku wala malazi. Watoto wengi zaidi ya asilimia 20 walibainika kutokwenda shule. Wawapo shuleni wanakosa chakula huku wakitumia muda wa zaidi ya masaa manne kwenda na manne kurejea majumbani kwao.

Binti huyu alishiriki kujenga shule na akajitolea kufundisha. Alijitolea chakula na malazi ikiwemo kuwanunua wanafunzi mavazi. Stori hii imerushwa live na inasambaa mitandaoni. Wanaojadili wanaona kama fedhea kwa watawala wetu huku watawala wakijinadi kwamba inatangaza utalii na kuitangaza nchi yetu.

Kwa maana nyingine watawala tatizo la watoto kukosa shule siyo big deal bali kwao wao wanaona kama video hii inatangaza utalii. Nimesoma comment ya waziri mmoja akisifia video ile akidai imesaidia wengi kuifahamu Tanzania.

Mimi nikawa na Mtizamo tofauti; nilipoona video hii nimejiuuliza Mama Salma Kikwete anakosa nini hadi achukue fedha za wananchi maskini ziwe zake na familia yake kupitia sheria mpya aliyopenyeza bungeni ya mafao ya wenza wa viongozi?

Hao wenza wa viongozi wana umaskini gani hadi wajione wao wanafaa kulipwa mabilioni ya kodi za umma for years huku wananchi wakikosa mlo mmoja?

Huyu binti Miss Worl hana pensheni lakini ana moyo wa Mungu na upendo. Huyu binti siyo Mtanzania ila ameonyesha kujali na kuthamini uhai wa watoto wetu. Huyu binti siyo mweusi bali ametambua kila binadamu anahitaji haki ya elimu na kuishi.

Natambua wenza walio wengi ni wanawake kuliko wanaume. Natambua waliopigania kulipwa mabilioni haya ni wanawake na siyo wanaume. Natambua wanawake wote waliopigania hii hoja wamezaliwa familia bora. Natambua wanawake hawa hawajawahi kuwaza wala kufikia kusaidia yeyote kwa fedha zao kama alivyofanya huyu binti. Wengi wao utumia fedha za umma kuzifanya mali yao na kutumia miradi ya umma kama fadhila kwa jamii.

Wanawake weusi jitafakarini, waume zenu walipopata madaraka walijilimbikiza mali za umma. Mwenyenzi Mungu akakasirika na sasa wakimaliza muda wa huduma wanachokiona mbele yao ni magonjwa na hivyo vile walivyochuma kwa dhulma vimeoza na kuishia kuwatibu kuliko kuvisaza.

Naona wanawake nao wameamua kujilimbikizia mali za maskini kwa msingi wa sheria. Wanawake viongozi wa Tanzania wamewakwa tamaa na nafsi zao zinawaza kuishi kwa anasa pale wenzao wao wanapoostaafu.

Amini Amin nawaambia......kwa kuwa pensheni hii italipwa mkiwa hai na ili msilipwe pensheni hii kwa muda mrefu na kunyonya maskini , Mwenyenzi Mungu anakwenda kuwapa maisha mafupi sana. Kisheria mtalipwa ila kiroho mtalipwa kwa muda mfupi sana.

Haiwezekani binti wa miaka 24 aje kwenye nchi yenye kila kitu akasaidie kulisha watoto wetu huku ninyi mkijilimbikizia mabilioni msiyoyafanyia kazi

Hongera miss world kwakuwainua wanetu.
We ungekuwa kwenye position yake ungeon sahihi kulipwa hicho kibumda?
 
Hongera mkuu umepangilia na kuandika uhalisia.Sio huyo waziri.
 
Mh! ishu sio kujustify the wrong doing by using the correct judiciary and/or parliament process. The whole concept was wrong even if it follows the correct parliament process.

Raisi ni mtumishi wa umma, je tuna watumishi wa umma wangapi? mafao ya Rais na marupurupu yake yote ukiondoa magari mawili, walinzi, mafao ya mishahara, mafao ya nyumba na mshahara wake kila mwezi vinatosha kabisa kutunza familia yake na mke kwa maisha yake yote, hapo siongelei mishemishe na ma-project makubwa anayokuwa ameyatengeneza wakati wa uongozi.

Je? hawa watumishi wa umma wengine ambao kwanza mishahara yao ni kidunchu sana, hawana mafao makubwa, hawana benefits za nyumba, magari , walinzi na mishahara etc. mbona wenza wao hawafikiliwi tena waliofanya kwenye mazingira magumu mara 80% ya viongozi wetu hawa.

Kama bunge lingekuwa linataka usawa nafikiri watu wa kupewa kipaumbele walikuwa ni hawa hoehae kajamba nani na si mabilionea wanaostahafu wakiwa na life insurance ya benefits zote maisha yao yote.

Ifike mahali tusijustify udhalimu, dhuluma, ufisadi kwa sababu tu tumefuata taratibu za kibunge au za kimahakama.

Pia na wewe uelewe hoja hiyo hakuipenyesha from nowhere bali kulikuwa na backing na kwa yeye ni bora angeisogeza kupitia kwa wabunge wengine.si kweli mwandishi hajui namna mchakato wa kutunga sheria inavyopitia bali hiyo skeptic yako tu.
Mkuu mbunge anayetoa mawazo, maoni au hoja bungeni kwa kufuata kanuni na taratibu za bunge na hoja yake ikakubaliwa hawezi kuhukumiwa kwa ku exercise haki hiyo.

Mkuu wajibu, mamlaka na haki ya kukubali au kukataa hoja hiyo ipo mikononi mwa bunge na wabunge wote.

Na yeye sio wa kwanza kufanya hivyo. Kwa mfano Zungu alitoa hoja ya tozo ya uzalendo bungeni ikakubaliwa, ikapitishwa na tunakatwa hiyo tozo!
 
Salma hajawahi kuwa na akili kama mumewe
Unategemea azitowe wapi? Ni kudra ya mwenyezi Mungu kufikia serhemu aliyopo lakini sijawahi kumuona akiwa na wazo lolote maana kuhusu taifa hili. Labda mswada wa mafao kwa wenza wa viongozi wakuu.
 
Miss world ni binti mdogo aliyezaliwa masafa ya mbali na Tanzania. Alipofika Tanzania miaka minne iliyopita alitembelea Arusha na kukuta familia zisizo na uwezo wa mlo wa siku wala malazi. Watoto wengi zaidi ya asilimia 20 walibainika kutokwenda shule. Wawapo shuleni wanakosa chakula huku wakitumia muda wa zaidi ya masaa manne kwenda na manne kurejea majumbani kwao.

Binti huyu alishiriki kujenga shule na akajitolea kufundisha. Alijitolea chakula na malazi ikiwemo kuwanunua wanafunzi mavazi. Stori hii imerushwa live na inasambaa mitandaoni. Wanaojadili wanaona kama fedhea kwa watawala wetu huku watawala wakijinadi kwamba inatangaza utalii na kuitangaza nchi yetu.

Kwa maana nyingine watawala tatizo la watoto kukosa shule siyo big deal bali kwao wao wanaona kama video hii inatangaza utalii. Nimesoma comment ya waziri mmoja akisifia video ile akidai imesaidia wengi kuifahamu Tanzania.

Mimi nikawa na Mtizamo tofauti; nilipoona video hii nimejiuuliza Mama Salma Kikwete anakosa nini hadi achukue fedha za wananchi maskini ziwe zake na familia yake kupitia sheria mpya aliyopenyeza bungeni ya mafao ya wenza wa viongozi?

Hao wenza wa viongozi wana umaskini gani hadi wajione wao wanafaa kulipwa mabilioni ya kodi za umma for years huku wananchi wakikosa mlo mmoja?

Huyu binti Miss Worl hana pensheni lakini ana moyo wa Mungu na upendo. Huyu binti siyo Mtanzania ila ameonyesha kujali na kuthamini uhai wa watoto wetu. Huyu binti siyo mweusi bali ametambua kila binadamu anahitaji haki ya elimu na kuishi.

Natambua wenza walio wengi ni wanawake kuliko wanaume. Natambua waliopigania kulipwa mabilioni haya ni wanawake na siyo wanaume. Natambua wanawake wote waliopigania hii hoja wamezaliwa familia bora. Natambua wanawake hawa hawajawahi kuwaza wala kufikia kusaidia yeyote kwa fedha zao kama alivyofanya huyu binti. Wengi wao utumia fedha za umma kuzifanya mali yao na kutumia miradi ya umma kama fadhila kwa jamii.

Wanawake weusi jitafakarini, waume zenu walipopata madaraka walijilimbikiza mali za umma. Mwenyenzi Mungu akakasirika na sasa wakimaliza muda wa huduma wanachokiona mbele yao ni magonjwa na hivyo vile walivyochuma kwa dhulma vimeoza na kuishia kuwatibu kuliko kuvisaza.

Naona wanawake nao wameamua kujilimbikizia mali za maskini kwa msingi wa sheria. Wanawake viongozi wa Tanzania wamewakwa tamaa na nafsi zao zinawaza kuishi kwa anasa pale wenzao wao wanapoostaafu.

Amini Amin nawaambia......kwa kuwa pensheni hii italipwa mkiwa hai na ili msilipwe pensheni hii kwa muda mrefu na kunyonya maskini , Mwenyenzi Mungu anakwenda kuwapa maisha mafupi sana. Kisheria mtalipwa ila kiroho mtalipwa kwa muda mfupi sana.

Haiwezekani binti wa miaka 24 aje kwenye nchi yenye kila kitu akasaidie kulisha watoto wetu huku ninyi mkijilimbikizia mabilioni msiyoyafanyia kazi

Hongera miss world kwakuwainua wanetu.
Ukombozi wa Tanzania upo Mikononi mwa Watanzania wenyewe.
Ukombozi wa African upo Mikononi mwa waafrika Wenyewe.
"Ee Mungu tusaidie kufungua frikra zetu tuondokane na uvivu wa kufikiri na utupatie moyo wa kizalendo kwa kufanya kazi kwa bidii pasipo kunufaisha matumbo yetu iwe kwaajili ya ustawi wa vizazi vyetu vya baadae wapate kuishi Tanzania iliyo Salama" Amina.
 
Back
Top Bottom