Nimeona kuna video inarekodi kijana amechanjiwa kinga huku mtaalam akiijaribu, ni aina ya kinga kwa huko Kongo lakini hata Kwa mikoa jirani hasa Kigoma wapo wataalam.
kuna huyu mpuuzi yupo na simu anarekodi sasa video imevuja mitandaoni, alichofanya ni ujinga uliopitiliza.
Ingekuwa ni ile ya kuweza kutafuna sindano na nyembe bila athari ni sawa tu na nadhani mshawahi kuwaona waliofanyiwa hizo dawa, ila hii ni ishu nyingine kabisa, hii ni kinga mtu anawekewa dhidi ya mapanga, visu, mkuki, risasi, n.k. lakini huwa ina mlango wa nyuma upo wazi kwajili ya kumuua mtu wa aina hii, maisha ya huyu kijana kwa sasa yanaweza kuwa hatarini sana endapo watu wakishawishika kutesti kuitegua.
View attachment 2633767