Video: Hivi "vetting" hufanyika kweli kabla ya uteuzi wa viongozi? msikilize Kenani Kihongosi akitetea kitendo chake cha kucharaza viboko watu...

yaani utakua mtu moja arrogant,unayejichukulia juu saaana kuwa na guts za kumpiga mtu mzima mwenzio fimbo, ukimchunguza huyu mtu utakuta ni mjivuni sana,dharau na hana mahusiano mazuri na watu, hajui ukiwa kiongozi unahitaji ushirikiano kutoka walio chini yako na sio kuwafanya wawe na uoga.
 
Nimemuelewa sana kuna watu wanakera sana chapa tu, walichofanya hao jamaa ni ujinga unaokera mno.

Tena angewatandika na wire ndio ingefaa zaidi badala ya fimbo.
Chunguza vizuri kizazi chako huko nyuma, kuna uwezekano mkubwa sana una asili ya utumwa.
 
Sio mjivuni, ni asili ya utumwa kwenye chain ya kizazi huwa inaleta watu wa aina hii.
 
Mkuu mbona haya tulishayaandika kitambo... ya wenye mamlaka kufundisha raia kujichukulia sheria mikononi.
Dalili ilipojitokeza tulisema sasa inanyesha tusubiri mafuriko.
Ikiwa" wadhalilishwaji" hawatambui haki zao wala hawataki kuchukua hatua "woga" dhidi ya udhalilishaji ule. Mwadhani kelele zetu zasaidia nini?
Tuvumiliane tu... 5tena
 
Vetting huangalia historia na hutumika kutabiri tu kuwa huyu atatufaa na blaa blaa nyingine ila haijui future itakuwaje. Ndio maana watu hufanyiwa vetting ila baada ya madaraka watu hugeuka.
Kwa nini na yeye akigeuka asigeukwe?
 
Kwa hiyo tunafuata njia ya Argentina, right?

Kwa hiyo hata mungu aliyeiondoa CORONA kumbe ni mungu wa 666, right?

Duuh, mimi siko huko, sitaki kabisa kwenda huko...!
Hutuna mungu aliyeiondoka korona bali tunae Mungu, unaheshima jina la kolona kwa kuliandika kwa adabu zote ila Mungu unaandika mungu, ndo mana mleta mada kawaandika hayo, anamaana yake kwa watu kama ninyi
 
Kumtetea mkuu wa wilaya mpumbavu na mjinga kama yule ni kujipaka mavi zaidi, sheria na taratibu zilisha wekwa namna ya kushuhulika na wahalifu kwa kosa lolote lile

Hakuna utaratibu wa kuchapa viboko wahalifu hadharani mbele ya camera kama alivyo fanya Dc mpuuzi huyo

Kila mtu akisema afanye hivyo nadhani wenye hasira za kuua wangesha ua wengi sana ndio maana zikawekwa sheria
 
Kwa nini na yeye akigeuka asigeukwe?
Sasa hapo unafikiri kageuka au vetting ilizingatia utendaji kazi wa namna hiyo ama tuseme ilitaka awe hivyo ndio maana akachaguliwa
 
Ndio maana ata kwenye murder case hukumu zinatofautiana; kuna 1 degree murder, 2 degree murder and maslaughter. Na adhabu uwa tofauti either kunyongwa, kwenda jela maisha au kutumikia miaka kadhaa na kuachiwa.

Unaangukia wapi kwenye hukumu depends on the evidence of ‘malice aforethought’ on your actions. In others words mahakama pia inatambua sometimes ppl react abruptly when there is provocation that can be used as a ‘mitigation factor’ to reduce the punishment.

Tukumbuke sehemu kubwa ya criminal laws misingi yake ni morality vitu ambavyo jamii atuvikubali tumevirasimisha tu kwa sheria.

Kwa maana hiyo natambua kuna sheria Ila upuuzi wa wahusika unakera sana achilia tu wizi kuna swala la ‘menace’ corruption of the youth kwa kuwashirikisha watoto wadogo kuhujumu shule yao.

Ndio maana nimeelewa sana frustration yake mkuu wa wilaya mpaka kuwachapa viboko.

Binafsi ukiniuliza nadhani it’s just a petty crime where harsh punishment is not necessary. However the morality of it all is just too wrong.

Huku watu wanaangaika usiku na mchana kutatua tatizo la ukosefu wa madawati kila siku tunatembeza picha mitandaoni serikali aijali. Nchi yetu ni maskini kutatua ilo tatizo large chunk of financial resources za halmashauri zinapelekwa huko at the opportunity cost of other important services za jamii.

Halafu wewe unajifikiria mwenyewe tu ujali tena unashirikisha na watoto wadogo kutumiza agenda zako, usually I don’t support watu kujichukulia sheria mkononi naweza elewa desperation ya kibaka kama teja na watu wanaowachoma moto kuchukuliwa hatua.

Lakini hawa wa madawati I can also understand frustration ya mkuu wa wilaya na adhabu aliyoitoa sakata lote ukisikiliza given the government is trying hard to eliminate the problem; kwakweli wachapwe tu mbele ya camera.

Hii biashara ya chuma chakavu inaanza kuwa tatizo serikali ianze kufikiria kutoa adhabu kwa watu wanaonunua mali za wizi, kama ilo alifanyiki kwa sasa.
 
Ni kweli tendo si la kijinga tu bali la kihalifu pia. Unajua kwann matendo ya kihalifu yanafanyiwa uchunguzi na polisi? Sababu unaweza kugundua mambo mengine makubwa ya kihalifu. Sasa hapo baada ya fimbo shughuli inaishia hapo. Viongozi wasibebe majukumu yasiyo ya kwao.
 
Kazi ya polisi ni kuchukua criminal offence yoyote at any stage sio lazima mtu apeleke mashitaka kwao. Kila mtu kaona ilo kosa including polisi so if they are interest in investigating and prosecuting hakuna wakuwazuia.

Polisi wetu sometimes wanazingua tu sasa hivi nao wanajifanya wanaandamana kupinga ukatili wa wanawake ukiwauliza ni kesi ngapi ambazo victim hawaku report wao wamechukua hatua sidhani kama watakupa majibu. Hakuna ata efforts za kuitaka jamii kushiriki kutatua tatizo mfano kushawishi majirani kupiga simu kwao ku report domestic violence za nyumba ya pili ili wao kuchunguza na kuchukua hatua.

Wakati ni jukumu lao kuzuia criminal offence zote sio lazima mtu apeleke malalamiko, sometimes ni wasanii tu na wenyewe eti wanaandamana kupinga ukatili wa wanawake wakati efforts za kupunguza ilo tatizo atulioni.
 
Mkuu sijui kwann unatumia nguvu kuhalalisha alichokifanya DC. Alichokifanya ni kosa regadless ya udhaifu wa polisi au kiwango cha ujinga cha uhalifu uliofanyika. Kosa ni kosa boss na DC kafanya kosa kuchukua yale maamuzi mbele ya kamera. Just imagine kila kiongozi atandike watu viboko wakifanya uhalifu au makosa? Nn kitafuata? Unadhani ni raia wote ni wepesi wa kugeuza makalio waadhibiwe? RC alikosea, huenda alipitiwa sababu ya hasira ila alikosea na huenda hilo kosa asilirudie tena.
 
Chunguza lugha yangu kuanzia post ya kwanza ‘I can understand his frustration’ mi mwenyewe uwezi kuniambia nilale chini unitandike nikubali.

Ila ata hao jamaa wanajua walichofanya kinastahili bakora.
 
Waliokula bakora hawajala bakora kwa sababu ya majungu kama yale uliyoyaingiza wewe hapa.

Juzi tumeona uchaguzi ukinajisiwa, hao maDC ni sehemu ya hiyo najisi ya kimfumo kwenye uchaguzi huo. Je tuchukue hatua za kuwachapa? Mbona wao wanasisitiza kama haki haijatendeka watu waende mahakamani, ni kwanini walioona wizi wa kura hawajawachapa waliofanya hivyo? Usitetee ulevi wa madaraka.
 
Changuza lugha yangu kuanzia post ya kwanza ‘I can understand his frustration’ mi mwenyewe uwezi kuniambia nilale chini unitandike nikubali.

Ila ata hao jamaa wanajua walichofanya kinastahili bakora.

Kinastahili bakora kwa maagizo ya mahakama, na sio kwa kiburi cha madaraka.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…