video nimeiona..
kwa analysis yangu, hii video ni low quality!! kama kweli imekuwa produced na huyo sony, basi nahisi amemuibia rose kwa kiwango fulani! ukichunguza, karibu nusu nzima ya video, imeshutiwa eneo moja tu, mavazi ni yale yale karibu robo tatu ya video, uchanganyaji wa picha nao ni wa kawaida sana!!!
kwa jinsi huyu sony pictures anavyosifiwa, sidhani kama video ilitakiwa kuonekana kwa jinsi nilivyoiona youtube.. la sivyo atoe sababu ya msingi iliyomfanya iwe hivi.. kama si ulipuaji wa kazi ni nini sasa!! kitendo cha kutumia vazi la aina moja kwa 90% ya video nzima, inakosesha sana ladha ya video kwa watazamaji wake.. abadilishe hilo tafadhali!
video kama hii sioni kama ina viwango hasa vya kutazamwa kimataifa..!! haina tofauti na video zilizoshutiwa na camera ndogo hizi za kupigia picha.. 14mp, 5x zoom..!