VIDEO: Msanii Roma na wenzake warejea rasmi uraiani. Kufunguka Jumatatu

Kama leo wanaogopa kuongea kwa sababu ya makubaliano waliyoweka,ikifika jumatatu makubaliano yanaexpaya??
Ina maana hao walioweka makubaliano hawajui kama mtaongea jumatatu???
Ni hatari gani unayoiogopa leo ambayo jumatatu hutaiogopa tena????
 
Mwanasheria wake anasema Roma hayupo vzr kiafya. Wakati anashuka kwenye gari ni dhahiri kabisa roma anaonekana anachechemea. Ukija kwenye maelezo yake Roma anasema yupo vizuri kabisa.
Hii obviously, Roma alikuwa ameshikiliwa na vyombo nya dola, sasa watanzania tujiulize kwa nini? Je tufanye nini? Maana hata wabunge wetu ambao tumewachagua ( CCM) wanashindwa kusema chochote adharani kwa kuogopa.
 
Movie inatengenezwa na wamepewa warning wasiongee chochote sasa hivi mpaka watakapolishwa maneno.
wameambiwa hakuna uhuru usio na mpaka lakini wakaimbishwa na wauza ngada. kama huoni mpaka kaa mbali au utaishia lupango.
 
...Mkuu labda hayuko huru kuongea imebidi aseme hivyo japo inawezekana kabisa hakuna ukweli. Unakumbuka kutekwa kwa Dr Ulimboka na kudhani wamemuua? Alisema mengi sana wakati yuko hospitali na Watanzania wengi tulikuwa na shauku kubwa sana ya kumsikia aseme kila kitu mara baada ya kupata ahueni kufuatia matibabu yake kule RSA. Aliporudi na vitisho alivyopewa hakutaka hata kuzungumza kilichojiri hadi kuokotwa akiwa hoi bin taabani. Natumai hawa wataweza kuzungumza hiyo Jumatatu na kuwambia kila kitu. Ukiona siku hiyo imekatika bila kuwasikia hawa basi ujue nao wameshatishwa sana kuhusu kusema chochote kile kilichojiri.

Mzima kivipi wakati kapelekwa hospital
 
The guy is in shock, anaonekana psychological hayuko okey!!! Inaonekana hatutapata nafasi yakuujua ukweli, ukimsoma vizuri nikama kuna vitisho vikubwa sana kapewa!!!

Mwanashera wake anaonekana kama sio mkongwe sana thats why wame muweka pembeni wakati kisheria anayo room yakusikiliza mahojiano hayo wakati yanaedelea.

ila totaly nimejiridhisha kuwa kunamkono wa serikali ya mkoa katika hili 100% hiyo haikwepeki
 
Wote tukumbuke yupo Mungu kutokana na jinsi tukio hili la utekaji linavyozidi kushika kasi ktk Nchi inayoitwa kisima cha amani ,Ebu manusura mweke wazi tukio zima lilikuwaje bila kusingizia asiehusika semeni ukweli na Mungu awaongoze ,ila hayo makubaliani kama yana masharti ya kumuingiza asie husika Epukeni kusingizia ni Dhambi kubwa hasa U.K.linganisha na tukio lenyewe by aak
 
Yeye ansema ni mzima, mwingine ameongea anasema sio mzima na kaumia zaidi ya wenzake hadi ndani labda kaumizwa!!!.

Ruge wa Clouds mkurugenzi wake, ndie alikuwa nae/nao tangu asubuhi leo hii.

Hii movie bado bado
 
Dah! Wewe ni mzuri wa kusoma watu. Mie pia nimeona hilo la uso wake kuonyesha hofu kubwa. Ngoja tusubiri hiyi Jumatatu kama ataweza kufunguka na kusema kila kitu kilichojiri lakini kwa Serikali hii dhalimu wanaweza kupewa vitisho vya kufa mtu wasiseme chochote kilichojiri.

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…