Video: Mtangazaji akatisha taarifa ya habari na kufunguka kuwa hajalipwa

Video: Mtangazaji akatisha taarifa ya habari na kufunguka kuwa hajalipwa

Sam Gidori

Senior Member
Joined
Sep 7, 2020
Posts
165
Reaction score
417
Mtangazaji wa Kituo cha Runinga cha KBN nchini Zambia amefunguka kuwa yeye na wenzake hawajalipwa mishahara yao.

Kalimina Kabinda alikatisha taarifa ya habari na kuwaumbua waajiri wake mubashara, na kisha kuichapisha video hiyo katika mtandao wa kijamii wa Facebook.


Pamoja na video hiyo, Kabinda aliandika, “Ndiyo, nilifanya hivyo kwenye matangazo mbashara ya TV kwa sababu waandishi wengi wa habari wanaogopa kuongea, haimaanishi waandishi wa habari hawapaswi kuongea.”

Baada ya video hiyo kuzua gumzo, Mkuu wa Kituo hicho cha Runinga, Kennedy Mambwe alimlaumu Kabinda akisema alikuwa amelewa wakati alipokuwa akisoma taarifa ya habari, lakini hakuzungumzia madai yake.

“KBN ina mfumo mzuri wa kuwasilisha malalamiko ya wafanyakazi wake, hivyo tabia ya Kabinda ni kinyume na maadili tunayosimamia kama Kituo,” taarifa ya Mkuu wa Kituo hicho ilieleza, ikitaja kuchukua hatua za kuwanidhamisha wote wanaohusika.
 
“KBN ina mfumo mzuri wa kuwasilisha malalamiko ya wafanyakazi wake, hivyo tabia ya Kabinda ni kinyume na maadili tunayosimamia kama Kituo,” taarifa ya Mkuu wa Kituo hicho ilieleza, ikitaja kuchukua hatua za kuwanidhamisha wote wanaohusika.

Huenda ni kweli Jamaa alikula masanga ili apate ujasiri Wa kuyatoa hayo ya moyoni.

Huyu Mkuu mpumbavu angekuwa amewalipa mishahara yao wala haya yasingetokea.

Unataka kuchukua hatua za kinidhamu ilhali wewe ndiye umesababisha mpaka mtu akukosee hiyo nidhamu?

Pathetic!
 
Mtangazaji wa Kituo cha Runinga cha KBN nchini Zambia amefunguka kuwa yeye na wenzake hawajalipwa mishahara yao.

Kalimina Kabinda alikatisha taarifa ya habari na kuwaumbua waajiri wake mubashara, na kisha kuichapisha video hiyo katika mtandao wa kijamii wa Facebook.

View attachment 1830202

Pamoja na video hiyo, Kabinda aliandika, “Ndiyo, nilifanya hivyo kwenye matangazo mbashara ya TV kwa sababu waandishi wengi wa habari wanaogopa kuongea, haimaanishi waandishi wa habari hawapaswi kuongea.”

Baada ya video hiyo kuzua gumzo, Mkuu wa Kituo hicho cha Runinga, Kennedy Mambwe alimlaumu Kabinda akisema alikuwa amelewa wakati alipokuwa akisoma taarifa ya habari, lakini hakuzungumzia madai yake.

“KBN ina mfumo mzuri wa kuwasilisha malalamiko ya wafanyakazi wake, hivyo tabia ya Kabinda ni kinyume na maadili tunayosimamia kama Kituo,” taarifa ya Mkuu wa Kituo hicho ilieleza, ikitaja kuchukua hatua za kuwanidhamisha wote wanaohusika.
Alaaaaaa, hajakamatwa na kunyongwa kweli?
 
Hiyo ya kulewa sio pointi ya msingi, inaonesha walipanga wote wanaohusika na kurusha habari. Ingekuwa kama hawakukubaliana, matangazo yangekatwa mara tu alipoanza kuzungumza.
 
Mtangazaji wa Kituo cha Runinga cha KBN nchini Zambia amefunguka kuwa yeye na wenzake hawajalipwa mishahara yao.

Kalimina Kabinda alikatisha taarifa ya habari na kuwaumbua waajiri wake mubashara, na kisha kuichapisha video hiyo katika mtandao wa kijamii wa Facebook.


Pamoja na video hiyo, Kabinda aliandika, “Ndiyo, nilifanya hivyo kwenye matangazo mbashara ya TV kwa sababu waandishi wengi wa habari wanaogopa kuongea, haimaanishi waandishi wa habari hawapaswi kuongea.”

Baada ya video hiyo kuzua gumzo, Mkuu wa Kituo hicho cha Runinga, Kennedy Mambwe alimlaumu Kabinda akisema alikuwa amelewa wakati alipokuwa akisoma taarifa ya habari, lakini hakuzungumzia madai yake.

“KBN ina mfumo mzuri wa kuwasilisha malalamiko ya wafanyakazi wake, hivyo tabia ya Kabinda ni kinyume na maadili tunayosimamia kama Kituo,” taarifa ya Mkuu wa Kituo hicho ilieleza, ikitaja kuchukua hatua za kuwanidhamisha wote wanaohusika.
Sanaaa ndgu...Kama hulipwi hamna motisha ya kazi
 
Mtangazaji wa Kituo cha Runinga cha KBN nchini Zambia amefunguka kuwa yeye na wenzake hawajalipwa mishahara yao.

Kalimina Kabinda alikatisha taarifa ya habari na kuwaumbua waajiri wake mubashara, na kisha kuichapisha video hiyo katika mtandao wa kijamii wa Facebook.


Pamoja na video hiyo, Kabinda aliandika, “Ndiyo, nilifanya hivyo kwenye matangazo mbashara ya TV kwa sababu waandishi wengi wa habari wanaogopa kuongea, haimaanishi waandishi wa habari hawapaswi kuongea.”

Baada ya video hiyo kuzua gumzo, Mkuu wa Kituo hicho cha Runinga, Kennedy Mambwe alimlaumu Kabinda akisema alikuwa amelewa wakati alipokuwa akisoma taarifa ya habari, lakini hakuzungumzia madai yake.

“KBN ina mfumo mzuri wa kuwasilisha malalamiko ya wafanyakazi wake, hivyo tabia ya Kabinda ni kinyume na maadili tunayosimamia kama Kituo,” taarifa ya Mkuu wa Kituo hicho ilieleza, ikitaja kuchukua hatua za kuwanidhamisha wote wanaohusika.
Ni aibu mtu una chombo cha kazi halafu hukitumii kufikisha kero zako mwenyewe, somo kwa wafanyakazi RFA na sister station StarTV huwa wanatumia watu wa pembeni kudai hawajalipwa
 
Utovu wa nidhamu! Na pia ni tangazo la kumuharibia career yake mwenyewe forever Worldwide
 
Nilishafanya kazi media moja hivi hapa TZ, mshahara tulikua tunapewa tarehe 40 mpaka 50. Kwenye medias hii ni kawaida sana.
 
Huenda ni kweli Jamaa alikula masanga ili apate ujasiri Wa kuyatoa hayo ya moyoni.

Huyu Mkuu mpumbavu angekuwa amewalipa mishahara yao wala haya yasingetokea.

Unataka kuchukua hatua za kinidhamu ilhali wewe ndiye umesababisha mpaka mtu akukosee hiyo nidhamu?

Pathetic!
Ukiona pale nyumbani ni ugali maharage mwezi mzima ujue hali ya kifedha ya baba siyo nzuri kule kazini. Ukipayuka mitaani hovyo hovyo ujue unamvunjia heshima baba yako!!
 
Kazi za media ni ngumu sana, tena siku hizi ndo kabisa niliamua kuacha mwenyewe
Nilishafanya kazi media moja hivi hapa TZ, mshahara tulikua tunapewa tarehe 40 mpaka 50. Kwenye medias hii ni kawaida sana.
 
Ukiona pale nyumbani ni ugali maharage mwezi mzima ujue hali ya kifedha ya baba siyo nzuri kule kazini. Ukipayuka mitaani hovyo hovyo ujue unamvunjia heshima baba yako!!
Mwajiri wako siyo Baba yako.
Ukiona mpaka mtu ameamua kusema hadharani ujue kuna maswaibu mengi amekumbana nayo, na huenda hata kuna dalili za kutokulipwa kabisa.
 
Back
Top Bottom