Video na Picha: Ushahidi kuhusu yaliyotokea kwa Jaji Warioba wakati na baada ya vurugu, Ubungo Plaza

Video na Picha: Ushahidi kuhusu yaliyotokea kwa Jaji Warioba wakati na baada ya vurugu, Ubungo Plaza

View attachment 1513236View attachment 1513231
MDAHALO wa kujadili Katiba inayopendekezwa ulioandaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere, jana ulivunjika baada ya kutokea vurugu ambako Mwenyekiti wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba, alipigwa vibao shingoni na watu wanaodaiwa kuwa wanachama wa CCM.

Hali hiyo ilijitokeza kwenye Hoteli ya Blue Pearl iliyopo Ubungo Dar es Salaam, baada ya kuvunjika mdahalo huo uliokuwa umehudhuriwa na mamia ya watu, wengi wao wakiwa vijana.

Baada ya vurugu hizo, waandaji waliamua kuwatoa nje ya ukumbi wasemaji wa mdahalo huo akiwamo Warioba, Mwenyekiti wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Joseph Butiku, Profesa Palamagamba Kabudi na Profesa Mwesiga Baregu.

Wengine waliokuwa wazungumze kwenye mdahalo huo ni Humphrey Polepole na Rais wa Chama cha Wanasheria Zanzibar, Awadhi Said, ambao wote walikuwa wajumbe wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba.

Warioba, aliyewahi kushika wadhifa wa Waziri Mkuu na Makamu wa Rais, alipigwa vibao viwili shingoni alipofika kwenye mlango kuu wa kutoka ukumbini ambako kulikuwa na msongamano mkubwa wa watu. Wakati huo, Warioba na viongozi wenzake walikuwa wakitolewa nje ya ukumbi huo.

Hatua hiyo ilifanya mlinzi wake na baadhi ya watu waliokuwa wakimtoa kiongozi huyo waongeze mwendo na kumkimbiza kiongozi huyo wa taifa kwenye chumba maalumu cha wageni wa heshima (VIP lounge), kilichoko ndani ya hoteli hiyo.

Wakati Warioba akipigwa vibao, miongoni mwa watu waliokuwa karibu nyuna yake ni Katibu wa Uhamasishaji wa UVCCM, Paul Makonda.

Kwa sababu hiyo, baadhi ya vijana walichangia kumpiga kada huyo wa UVCCM aliyekuwa amevalia shati jeupe, huku wakimzuia kuingia kwenye chumba cha VIP ambako Jaji Warioba alikuwa amepelekwa.

Kufanikiwa kwa vijana hao kumzuia Makonda kuingia kwenye chumba hicho, kulitoa fursa ya kuendelea kupigwa hadi alipoponyoka na kukimbilia katika ofisi moja katika jengo hilo na kujifungia.

Baada ya kujificha katika chumba hicho, vijana hao waliitana na kuhamasishana ili wavunje mlango huo na kumtoa Makonda.

Hata hivyo baada kufanikiwa kuvunja mlango huo, vijana hao hawakumuona Makonda hadi walinzi wa hoteli hiyo na askari kanzu walipofika hapo na kuwafukuza.

Vurugu zilivyoanza

Vurugu katika mdahalo huo zilianza muda mfupi kabla ya Jaji Warioba aliyekuwa msemaji wa kwanza, kumaliza hotuba yake.

Baada ya kumaliza kuichambua Katiba inayopendekezwa, Jaji Warioba alisema katika kuitetae katiba hiyo, baadhi ya watu wamekuwa wakimtumia Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Nyerere kuunga mkono hoja zao.

“Tunatumia jina la Mwalimu ili kuunga mkono hoja zetu wakati mwingine ninajiuliza hivi tunatumia Mwalimu yuleyule ama…

“Mwalimu amekufa akisema hajaona hata sehemu ya kutia koma katika Azimio la Arusha, kuna watu waliwahi kumletea Mwalimu barua wakimwambia afungue akaunti nje ya nchi ndiyo fedha zake zitakuwa salama… Mwalimu siyo tu alikataa lakini alitangaza kila kitu hadharani.

“Leo Mwalimu angekuwapo angekubali watu wafungue akaunti nje ya nchi, angekubali watu wapewe zawadi wakae nazo… nikasema huyo wao siyo Mwalimu, Mwalimu alikuwa ni mtu mwenye uwezo wa kufanya uamuzi mgumu hata unaomhusu yeye,” alisema Warioba.

Vijana na mabango

Baada ya maneno hayo, baadhi ya vijana takriban 20, walisimama na kunyanyua juu mabango yaliyokuwa na ujumbe mbalimbali wa kumtukana Jaji Warioba na mengine yakisifu Katiba inayopendekezwa.

Kitendo hicho kilifanya baadhi ya watu kujaribu kuwakalisha chini huku wengine wakichana mabango hayo hali iliyozusha vurugu.

Wakati wote huo Jaji Warioba alikuwa amesimama akijaribu kuwasihi watu hao kukaa chini, lakini hali hiyo ilionekana kutozaa matunda.

Baada ya muda vijana hao walijitenga pembeni karibu na jukwaa kuu huku wakiwa na mabango yao, wakiimba nyimbo mbalimbali za CCM.

Hali hiyo ilisababisha baadhi ya watu watoke ukumbini huku wengine wakiwa wanarudi kuketi kwenye viti vyao.

Wakati vurugu hizo zikiendelea, Profesa Kabudi na Butiku kwa nyakati tofauti, walionekana wakimtaka Makonda kuwatuliza vijana hao wa CCM ambao alidaiwa yeye yeye ndiye aliwaingiza katika ukumbi huo.

Wakati viongozi wakimtaka Makonda kufanya hayo, vijana wengine walionekana kumvuta Makonda wakitaka kumpiga hali iliyomlazima kumtumia kama kinga, Amon Mpanju, ambaye alikuwa Mjumbe wa Bunge Maalumu la Katiba akiwakilisha kundi la walemavu.

Hali iliendelea hivyo hadi baadhi ya vijana waliokuwa wamekaa walipohamasishana na kuwapiga wale waliokuwa na mabango, kwa kutumia viti hali iliyofanya wakimbie na kutoka nje ya ukumbi huo.

Baada ya vijana hao kutoka nje, hali iliwageukia Makonda na Mpanju ambao baada ya kuona hali imekuwa tete, walikimbilia kwenye jukwaa kuu na kukaa karibu na Jaji Warioba.

Huku hali ikiwa bado ya taharuki, viongozi hao (Warioba na wenzak) waliamua kutoka nje ya ukumbi na ndipo zahama ya kupigwa vibao kwa Jaji Warioba ilipojitokeza.

Wahuni wampiga Jaji Warioba Dar - Mtanzania
nani hasa aliyempiga warioba , nakala nzur ila bado inatuacha na maswali
 
Makonda ana mazuri mengi lkn pia nafikiri mabaya yake ya dhahiri na sirini ni mengi zaidi yamezidi hayo mazuri sasa ni muda wake kukumbana na Karma yake ni kikombe chake akipokee mpaka atoke kwenye kulipia udhalimu wake ndo atakuwa huru na hii ni kwa wote wanao ona hawata kuja kuguswa na sheria za maumbile

Unaweza kukimbia sheria za nchi/binaadam lkn sheria za maumbile hauwezi kuzi twist hata siku moja kuna siku utalipa au kulipwa kwa matendo yako afu ni hapa hapa ktk uso wa ardhi
 
Sijaona comment yako.
Sasa sijui ni funzo lipi mtu makini analoweza kutoka nalo kwenye somo hili.

1. Kumpiga Warioba - kukawafaidisha hao wahuni toka miaka hiyo. Kitendo hicho na mengine machafu yakawafanya waonekane hodari kwa watu waliopendezwa na tendo hilo. Hawa wenye madaraka wakawazawadia vyeo ambavyo wamefaidika navyo hadi wakati huu, na hakuna ajuaye kwamba hawataendelea kufaidika baada ya hapa.

Kwa hiyo uhuni unalipa? Hilo linaweza kuwa finzo kwa baadhi ya watu.

2. Ngoja funzo hili la pili niliweke kipolo kwa sasa.
 
View attachment 1513236
MDAHALO wa kujadili Katiba inayopendekezwa ulioandaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere, jana ulivunjika baada ya kutokea vurugu ambako Mwenyekiti wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba, alipigwa vibao shingoni na watu wanaodaiwa kuwa wanachama wa CCM.

Hali hiyo ilijitokeza kwenye Hoteli ya Blue Pearl iliyopo Ubungo Dar es Salaam, baada ya kuvunjika mdahalo huo uliokuwa umehudhuriwa na mamia ya watu, wengi wao wakiwa vijana.

Baada ya vurugu hizo, waandaji waliamua kuwatoa nje ya ukumbi wasemaji wa mdahalo huo akiwamo Warioba, Mwenyekiti wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Joseph Butiku, Profesa Palamagamba Kabudi na Profesa Mwesiga Baregu.

Wengine waliokuwa wazungumze kwenye mdahalo huo ni Humphrey Polepole na Rais wa Chama cha Wanasheria Zanzibar, Awadhi Said, ambao wote walikuwa wajumbe wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba.

Warioba, aliyewahi kushika wadhifa wa Waziri Mkuu na Makamu wa Rais, alipigwa vibao viwili shingoni alipofika kwenye mlango kuu wa kutoka ukumbini ambako kulikuwa na msongamano mkubwa wa watu. Wakati huo, Warioba na viongozi wenzake walikuwa wakitolewa nje ya ukumbi huo.

Hatua hiyo ilifanya mlinzi wake na baadhi ya watu waliokuwa wakimtoa kiongozi huyo waongeze mwendo na kumkimbiza kiongozi huyo wa taifa kwenye chumba maalumu cha wageni wa heshima (VIP lounge), kilichoko ndani ya hoteli hiyo.

Wakati Warioba akipigwa vibao, miongoni mwa watu waliokuwa karibu nyuna yake ni Katibu wa Uhamasishaji wa UVCCM, Paul Makonda.

Kwa sababu hiyo, baadhi ya vijana walichangia kumpiga kada huyo wa UVCCM aliyekuwa amevalia shati jeupe, huku wakimzuia kuingia kwenye chumba cha VIP ambako Jaji Warioba alikuwa amepelekwa.

Kufanikiwa kwa vijana hao kumzuia Makonda kuingia kwenye chumba hicho, kulitoa fursa ya kuendelea kupigwa hadi alipoponyoka na kukimbilia katika ofisi moja katika jengo hilo na kujifungia.

Baada ya kujificha katika chumba hicho, vijana hao waliitana na kuhamasishana ili wavunje mlango huo na kumtoa Makonda.

Hata hivyo baada kufanikiwa kuvunja mlango huo, vijana hao hawakumuona Makonda hadi walinzi wa hoteli hiyo na askari kanzu walipofika hapo na kuwafukuza.

Vurugu zilivyoanza

Vurugu katika mdahalo huo zilianza muda mfupi kabla ya Jaji Warioba aliyekuwa msemaji wa kwanza, kumaliza hotuba yake.

Baada ya kumaliza kuichambua Katiba inayopendekezwa, Jaji Warioba alisema katika kuitetae katiba hiyo, baadhi ya watu wamekuwa wakimtumia Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Nyerere kuunga mkono hoja zao.

“Tunatumia jina la Mwalimu ili kuunga mkono hoja zetu wakati mwingine ninajiuliza hivi tunatumia Mwalimu yuleyule ama…

“Mwalimu amekufa akisema hajaona hata sehemu ya kutia koma katika Azimio la Arusha, kuna watu waliwahi kumletea Mwalimu barua wakimwambia afungue akaunti nje ya nchi ndiyo fedha zake zitakuwa salama… Mwalimu siyo tu alikataa lakini alitangaza kila kitu hadharani.

“Leo Mwalimu angekuwapo angekubali watu wafungue akaunti nje ya nchi, angekubali watu wapewe zawadi wakae nazo… nikasema huyo wao siyo Mwalimu, Mwalimu alikuwa ni mtu mwenye uwezo wa kufanya uamuzi mgumu hata unaomhusu yeye,” alisema Warioba.

Vijana na mabango

Baada ya maneno hayo, baadhi ya vijana takriban 20, walisimama na kunyanyua juu mabango yaliyokuwa na ujumbe mbalimbali wa kumtukana Jaji Warioba na mengine yakisifu Katiba inayopendekezwa.

Kitendo hicho kilifanya baadhi ya watu kujaribu kuwakalisha chini huku wengine wakichana mabango hayo hali iliyozusha vurugu.

Wakati wote huo Jaji Warioba alikuwa amesimama akijaribu kuwasihi watu hao kukaa chini, lakini hali hiyo ilionekana kutozaa matunda.

Baada ya muda vijana hao walijitenga pembeni karibu na jukwaa kuu huku wakiwa na mabango yao, wakiimba nyimbo mbalimbali za CCM.

Hali hiyo ilisababisha baadhi ya watu watoke ukumbini huku wengine wakiwa wanarudi kuketi kwenye viti vyao.

Wakati vurugu hizo zikiendelea, Profesa Kabudi na Butiku kwa nyakati tofauti, walionekana wakimtaka Makonda kuwatuliza vijana hao wa CCM ambao alidaiwa yeye yeye ndiye aliwaingiza katika ukumbi huo.

Wakati viongozi wakimtaka Makonda kufanya hayo, vijana wengine walionekana kumvuta Makonda wakitaka kumpiga hali iliyomlazima kumtumia kama kinga, Amon Mpanju, ambaye alikuwa Mjumbe wa Bunge Maalumu la Katiba akiwakilisha kundi la walemavu.

Hali iliendelea hivyo hadi baadhi ya vijana waliokuwa wamekaa walipohamasishana na kuwapiga wale waliokuwa na mabango, kwa kutumia viti hali iliyofanya wakimbie na kutoka nje ya ukumbi huo.

Baada ya vijana hao kutoka nje, hali iliwageukia Makonda na Mpanju ambao baada ya kuona hali imekuwa tete, walikimbilia kwenye jukwaa kuu na kukaa karibu na Jaji Warioba.

Huku hali ikiwa bado ya taharuki, viongozi hao (Warioba na wenzak) waliamua kutoka nje ya ukumbi na ndipo zahama ya kupigwa vibao kwa Jaji Warioba ilipojitokeza.

Wahuni wampiga Jaji Warioba Dar - Mtanzania
ASANTE sana Mkuu kwa hii kitu..
Kigamboni mngezubaa tu mngempa Ubunge huyu muhuni Bashite.
 
Sasa sijui ni funzo lipi mtu makini analoweza kutoka nalo kwenye somo hili.

1. Kumpiga Warioba - kukawafaidisha hao wahuni toka miaka hiyo. Kitendo hicho na mengine machafu yakawafanya waonekane hodari kwa watu waliopendezwa na tendo hilo. Hawa wenye madaraka wakawazawadia vyeo ambavyo wamefaidika navyo hadi wakati huu, na hakuna ajuaye kwamba hawataendelea kufaidika baada ya hapa.

Kwa hiyo uhuni unalipa? Hilo linaweza kuwa finzo kwa baadhi ya watu.

2. Ngoja funzo hili la pili niliweke kipolo kwa sasa.
mkuu hapa duniani ukitaka kufanikiwa lazima ukufuru kwanza, (kafara tena ilionona) kupata vyeo na hata pesa, so Mzee warioba pia ilikua ni kafara ilionona!
 
Jamiiforums is where we dare to talk openly!



Kwa mwananchi yeyote ambaye hajafungwa kimawazo na kifikra, angalia vizuri hii video kwenye dakika ya 1:18 ili yale uliyoambiwa uchanganye naya kwako kuhusu tuhuma zinazoelekezwa kwa Paulo Makonda!.

Pix-1.JPG


Mtoa mada katika mdahalo wa kujadili Katiba Inayopendekezwa, Jaji Joseph Warioba akitoa mada kabla ya mkutano huo kuvunjika katika ukumbi wa Ubungo Plaza jijini Dar es Saam.
DSC_2016.JPG

Jaji Joseph Warioba akitoa mada katika kongamano kabla ya vurugu kutokea.
Pix-2.JPG

Baadhi ya vijana walioingia na mabango ndani ya ukumbi wa mkutano wakionyesha mabango yao.
Pix-4.JPG

Jaji Joseph Warioba akiangalia usalama wake kabla ya kuondolewa na mlinzi wake katika ukumbi wa Ubungo Plaza ambapo mdahalo wa kuijadili Katiba Inayopendekezwa ulikuwa ukifanyika kabla ya kuvunjika.


Pix-3.JPG

Mlinzi wa Jaji Joseph Warioba (kushoto) akimkinga kwa mikono ili asipate madhara baada ya kuanza vurugu katika mdahalo wa kujadili Katiba Inayopendekezwa.


Pix-5.JPG

Aliyekuwa mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Humphrey Polepole akiongea na mmoja wa vijana aliyekuwa na jazba mara baada ya kutokea kwa vurugu katika mdahalo wa kujadili Katiba Inayopendekeza.

Pix-6.JPG

Mkurugenzi wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere (MNF), Joseph Butiku (katikati) akisindikizwa kuingia katika chumba cha VIP mara baada ya kuvunjika kwa mdahalo wa kujadili Katiba Inayopendekezwa.


DSC_2069.JPG


DSC_2072.JPG

Baadhi ya vijana wakionyesha mabango yenye ujumbe mbali mbali
DSC_2135.JPG

Paulo Makonda akimsaidia mlemavu wa macho, Amon Mpanju baada ya vurugu kuanza kutokea ndani ya ukumbi wa Ubungo Plaza.
DSC_2163.JPG


DSC_2181.JPG

Baadhi ya viti vilivyotumika kama silaha na kinga kwenye vulugu

DSC_2263.JPG

Jaji Warioba akitoka katika ukumbi huku akisindikizwa na askari kanzu.
DSC_2268.JPG

Jaji Warioba akisindikizwa na makachero wa Polisi baada ya kuvunjika kwa mdahalo wa Katiba Inayopendekezwa
Pix-4.JPG

Ogopa internet
 
Back
Top Bottom