VIDEO: Never Seen Anywhere in Afrika: Polisi Kenya wapevuka, Kijana wa Gen Z awapa somo na Uraia wamemuachia

VIDEO: Never Seen Anywhere in Afrika: Polisi Kenya wapevuka, Kijana wa Gen Z awapa somo na Uraia wamemuachia

Ahsante kwa kunirekebisha.

kiranga,

Unafikiri ni kwanini vyombo vya ulinzi vinatumiwa kufanya kazi chafu tofauti na miiko yake ya kazi?

Sheria zinawalinda vipi askari wa chini kutambua kwamba hii ni “abuse of power” na si “chain of command”?

Zipo sheria zinazowapa uhuru wa kupinga kwamba hii ni abuse of power hivyo siwezi kutii?

Rais wa zamani wa Burkina Faso, Captain Thomas Sankara aliwahi kusema kwamba, askari ambaye hana elimu ya kizalendo ya siasa anaweza kuwa mhalifu tu.

Nukuu yake ni hii "Without patriotic political education, a soldier is only a potential criminal.”

Mwanajeshi wanatakiwa kupewa elimu ya siasa, ya uraia, ya uzalendo, ya falsafa, ya mantiki, ajue maadili, ajue amri halali na isiyo halali.

Kuna sheria kama whistleblowers act zinamlinda askari kufanya kitu cha njama zisizo halali, lakini hata akilindwa na sheria, in practice ni vigumu sana ku survive hususan nchi zetu za Africa.

Ila sasa, kwa mfano kama Kenya, mwanajeshi akikataa kuua raia halafu raia wakabadiki utawala, mwanajeshi yuko safe. Ila mwanajeshi akikataa kuua raia halafu utawala uendelee ule ule, mwanajeshi anaweza kupata matatizo.

Egypt wanajeshi walikataa kutii amri za rais Hosni Mubarak kuua raia, lakini Mubarak akaondoleea wanajeshi wakawa salama.
 
Wote, kuanzia mabosi waliotoa amri mpaka askari wa kawaida waliotimiza amri.

Hao askari wa kawaida wakajitetea kwa hoja ya "sisi ni askari wa kawaida tu, tulitimiza amri kutoka juu tu, hatukutoa hizo amri".

Wakaambiwa kuwa, kutekeleza amri kutoka juu hakukuondolei hatia. Ukiikubali amri yenye kisa na kuitekeleza na wewe unakuwa na hatia.

hiyo ni mpya kwangu sikulijua hilo, what if you get fired kwa kukataa kutii amri, kuna haki yoyote ile unayoweza ipata hata mahakamani kutetea ajira yako kwani askari nao wanaitaji hiyo kazi ili waishi …
 
Kazi ya polisi ni kulinda raia na mali zao. Hao vijana wako kwenye maandamano, polisi walipaswa kuwalinda hao raia kwa gharama zote.

what if mkuu wa polisi akiwamlisha wawakamate au kuwapiga mabomu waandamanaji askari wanaweza kukataa kutii amri ya mkubwa wake?
 
what if mkuu wa polisi akiwamlisha wawakamate au kuwapiga mabomu waandamanaji askari wanaweza kukataa kutii amri ya mkubwa wake?
Kuandamana ni haki ya kikatiba na kazi ya polisi ni kuhakikisha kwamba waandamanaji wako salama. Huyo Mkuu wa Polisi anayewaamrisha polisi kuwakamata na kuwapiga waandamanaji bila sababu anatumia madaraka yake vibaya na anaweza akashtakiwa.
 
Mmh hii fursa bhana
JamiiForums-359572112.jpg
 
hiyo ni mpya kwangu sikulijua hilo, what if you get fired kwa kukataa kutii amri, kuna haki yoyote ile unayoweza ipata hata mahakamani kutetea ajira yako kwani askari nao wanaitaji hiyo kazi ili waishi …
In theory unaweza kushitaki na kushinda na kulipwa gharama na kurudishwa kazini.
 
Vipo vingi vya kujifunza huko kenya, hata askari awe na ujasiri wa namna gani lazima angerudi nyuma tu! Ameongea kwa hisia mno.
 
Naam na hashtags zinatembea hasa huko X na TikTok, alafu kuna mzee mmoja anaitwa Miguna huyu mzee anachochea sana vijana wa Gz wamng'oe mtukufu rais Ruto.

Anatumia hashtags hizi #RutoMustGo
#RutoMustGoNow
#RutoMustResign
#FreshElections
Sijui kama hilo litawezekana ngoja tuone leo itakuaje.
 
Back
Top Bottom