Shujaa Mwendazake
JF-Expert Member
- Jul 11, 2015
- 4,016
- 6,759
Hawa maaskari kutoka Bahi wanakera sana, unalazimishaje kuingia kwenye gari ya mtu na kutaka kuchomoa funguo? Gari yenyewe hata kukukimbia haiwezi, gari ina mali za mamilioni ya wafanyabiashara.
Rais kupitia kwa Inspekta Jenerali wa Polisi, sisi madereva tunakuomba uunde timu ya uchunguzi kufuatilia nyendo za Askari Trafiki wanaohudumu katika eneo hili la bahi. Wamejaa ubambikizi, ubabe, Rushwa na manyanyaso kwa madereva.
Sasa askari na mamlaka yote uliyonayo unashindana na kujibizana na dereva kama vile na wewe ni mpiga debe, iko wapi heshima na nidhamu ya jeshi la polisi?
Mwisho ukiona mpaka inafikia hivi dereva kuamua kulete vurugu hivi basi tutafakari kuwa kuna jambo halipo sawa mahala husika, hata hivyo malalamiko ni mengi sana kuhusu eneo hilo.
Swali la kujiuliza hapo ni kwanini Bahi tu na siyo Manyoni, Tinde ama Gairo? Kwani huko kote hakuna maokoto, si yapo na amani imetawala? Kinacholalamikiwa ni kuwa hapa kuna maokoto ya kulazimishwa, siyo yale ya fairplay.
Kwako Madam President,
Nakala kwa Mh. Masauni,
Inspekta Jenerali wa Polisi,
Kamanda wa Trafiki nchini.
Rais kupitia kwa Inspekta Jenerali wa Polisi, sisi madereva tunakuomba uunde timu ya uchunguzi kufuatilia nyendo za Askari Trafiki wanaohudumu katika eneo hili la bahi. Wamejaa ubambikizi, ubabe, Rushwa na manyanyaso kwa madereva.
Sasa askari na mamlaka yote uliyonayo unashindana na kujibizana na dereva kama vile na wewe ni mpiga debe, iko wapi heshima na nidhamu ya jeshi la polisi?
Mwisho ukiona mpaka inafikia hivi dereva kuamua kulete vurugu hivi basi tutafakari kuwa kuna jambo halipo sawa mahala husika, hata hivyo malalamiko ni mengi sana kuhusu eneo hilo.
Swali la kujiuliza hapo ni kwanini Bahi tu na siyo Manyoni, Tinde ama Gairo? Kwani huko kote hakuna maokoto, si yapo na amani imetawala? Kinacholalamikiwa ni kuwa hapa kuna maokoto ya kulazimishwa, siyo yale ya fairplay.
Kwako Madam President,
Nakala kwa Mh. Masauni,
Inspekta Jenerali wa Polisi,
Kamanda wa Trafiki nchini.