Video: Wanafunzi wa chuo kikuu Dodoma hawajui nini maana ya neno 'Tarakimu'

Video: Wanafunzi wa chuo kikuu Dodoma hawajui nini maana ya neno 'Tarakimu'

ninauhakika waliojibu kwa ufasaha kwenye hiyo video hawajarushwa hewani..lengo ni kukuza onlinetv na nadhani lengo limetimia..udom inawanafunzi wengi sana hao w4 hawawezi kuonyesha mustakabali wa wanafunzi wote.
 
Andika million sita na laki sita kwa tarakimu,Hua kuna watu wanapenda sana kulalia vichwa,
Waliwahi kuulizwa Wanaija hivi...The nationality of the person from Tanzania is a Tanzanians,How about the one's from England,hehehe majibu yake nilicheka sana mtu anajibu Englana[emoji28][emoji28]

Sent using Jamii Forums mobile app
6,600,000
 
Unaenda kwa mzungu kufanya kazi?? Hoja yako ni nini?
Goo
Good morning sir/madam can I clean your car and tend your garden? How much will you pay me? Four hundread thousand T. shillings? Is that ok sir/madam?
 
Ndio maana wale waliomaliza masomo ya shule ya msingi Tz huwa hawajui hata kuandika majina yao. Ukiwauliza wanaitwaje watakuambia eti wanaitwa baba na kamum, wakati ni vijana ambao tayari wameshabalekhe. [emoji38]
😀😀
 
Siku zote Watanzania humu JF hutuambia wao hawataki kuongea Kingereza kisa ni cha wakoloni, kwamba watakomaa na Kiswahili, ila mimi husema ziku zote humu, ni uzembe na uvivu wa kutokutaka kuchosha akili kwenye kujifunza lugha, hamna cha uzalendo wala utumwa wala ukoloni wala nini maana hata Kiswahili wanachojivunia huwa kinawapa matatizo haswa ikija kwenye matumizi rasmi ya kiuandishi na elimu.
Pia ukifuatilia hata uandishi wao humu, utaona matatizo makubwa sana, hamna lugha hata moja wanayoimudu ipasavyo.

Tazama hii video, jamaa amewaibukia wanafunzi wengi chuo kikuu cha Dodoma na kila mmoja ameshindwa nini maana ya neno 'tarakimu', yaani mwanafunzi amesoma chekechea akamaliza, akamaliza shule ya msingi, akapitia shule ya upili hadi kidato cha nne, akaendelea na kumaliza kidato cha sita na hatimaye akajiunga chuo kikuu, lakini neno la msingi kwenye shughuli za elimu linamshinda, halafu huyo ndio utakuta anahitimu shahada ya uhandisi na kuingia kitaa kusaka ajira.




Heheee mademu wametisha kweli. Wanaume wa tz ni vichwa maji. Matusi ndio tu wamejaza kwa kichwa
 
Back
Top Bottom