Video ya wasichana wa shule ‘wakinyunyiziwa’dawa ya kuua virusi' yawakera Wakenya

Video ya wasichana wa shule ‘wakinyunyiziwa’dawa ya kuua virusi' yawakera Wakenya

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191

Video inayoonesha wasichana wa shule wakiwa wamejipanga msururu kwa ajili ya kunyunyiziwa dawa kama sehemu ya hatua za kukabiliana na kusambaa kwa virusi vya corona imeleta mgawanyiko miongoni mwa Wakenya mtandaoni.


Video fupi ya sekunde 30 iliyopakuliwa kwenye Twitter na gazeti nchini humno inaonesha mwanaume aliyevalia mavazi ya kujikinga akiwanyunyizia kimiminika wasichana kwenye mikono, miguu na sare za shule:

Shirika la afya duniani halishauri kuwanyunyizia watu dawa ya kuua virusi na linasema inaweza kuleta madhara ‘’kimwili, na kisaikolojia’’
Shule zimefunguliwa Jumatatu nchini Kenya kwa ajili ya wanafunzi wanaohitimu huku miongozo ikitolewa kuhusu utoaji wa vitakasa mikono na mahala pa kunawa mikono na kuzingatiwa kwa sharti la kutosogeleana ili kuzuwia usambaaji wa virusi vya corona.

Wakenya kwenye mtandao wa kijamii wa Twitter wameelezea maoni yao tofauti kuhusu kunyunyiziwa kwa wanafunzi.
"Vitu kama hivyo na vifaa vya kunyunyiza vilipigwa marufuku na wizara ya afya Kwa vipi watu wazima wanakaa chini na kuamua kwamba kuwanyunyizia watoto kama hivi kutadhibiti #Covid19? Vipi kuhusu maji na sabuni ? " Dkt Mercy korir aliandika kwenye tweeter.

"Halafu kuanzia siku inayofuata tunakua na matatizo ya ngozi, kifua,maradhi ya pumu yote kwa sababu ya kisingizio cha pesa. Wazazi walilazimika kulipakwa ajili ya watoto wao ili wanyunyiziwe dawa kama ng’ombe ,"Phill Kamara aliandika tweeter.

"Sioni tatizo lolote kuhusu shughuli hii.. Ulitarajiwa watatakaswa vipi na maambukizi? .. Baadhi yenu ni waasi tu bila sababu," Denno Duevshi aliandika mtandaoni.
 
Kenya kuna mtifuano kuhusu matumizi ya fedha za mikopo waliyokopa kupambana na covid 19. Hapo wanataka kujustfy matumizi yake.
 
Wakenya, kuja huku TZ. Leta hiyo wasichana kwenye josho la ng'ombe tuuwe kupe. TZ ipo na mojosho mengi haitumiki. Ng'ombe imeshaoga mwezi huu.
 
Wakenya hamjielewi, mnapelekwa pelekwa tu na wazungu
Sio hawajielewi tu bali wameathirika kisaikolojia ,hivi unavaa vazi la kijikinga na korona kisha unawanyunyuzia dawa mkusanyiko wa watu hawajavaa hayo mavazi kisha huyo unaondoka .kuna maswali wanafunzi watakua nayo darasani wala hawatowaza kusoma :moja kama dawa ni kinga kwanini mnyinyiziaji alivaa mavazi ya kutenganisha Kati ya wanafunzi na yeye?

Pili wanafunzi watakua na msongo wa mawazo kama tupo sehem salama kwanini tunyunyuziwe dawa tena na mtu alivalia vazi maalum la kujikinga afadhar na hao wanafunzi wangepewa hayo mavazi wavae wangejiona kidogo wapo salama
 
Shukran sir"" God Nimezaliwa, , Bongo land A . K. A Mzizima**

Yaan"" Huku sis ni Maninja kuanzia Mtoto miaka 10.

Mpka mjumbe nyumba 10[emoji837]

So sad our ney!!bar"""" 254:
 
Back
Top Bottom