vidonda mji wa uzazi

vidonda mji wa uzazi

tunyi

Member
Joined
Jan 24, 2012
Posts
15
Reaction score
2
mke wangu alijifungua mtoto mkubwa 5.5kg bahati mbaya, toka december 2011, anasema kuna mabadiliko asiyoelewa kama: 1)akikaribia kupata hedhi joto linapanda sana na anajisikia kama anaumwa akipima malaria hana
2)masaa machache kabla ya hedhi anajisikia kama kuna kitu kinajizungusha chini ya kitovu ambayo yana ambatana na maumivu
3)siku 3 za mwanzoni anatokwa na damu nyingi siku ya 4 na kwendelea damu inatoka kidogo kidogo yaani haikatiki, alipima hospitali akaambiwa ana vidonda kwenye mji wa uzazi akapewa dawa ya kumeza hedhi ikakatika, tatizo la hedhi mda mrefu lilijitokeza mwezi wa 5 na huu mwezi wa 6 anasema tatizo limerudi, hii ni siku ya7 damu inatoka kidogo kidogo haikatiki, na anapata maumivu chini ya kitovu. yanakuja na kupotea, kwa sasa hajatumia dawa yoyote
SWALI: je hili tatizo linatibika na linaweza kuathiri uwezekano wa mke wangu kupata uja uzito? Tupo mwanza, naomba msaada tafadhali.
 
Nakushauri uende ukamuone daktari wa magonjwa ya wanawake (Gynacologist) ili amuevaluate vizuri mkeo. Maumivu ya tumbo la hedhi ni kitu cha kawaida, kwa wanawake wengine si makali lakini kwa wengine ni makali sana, pia hedhi kutoka kwa wingi kwa siku 3 za mwanzo kisha kufuatiwa na kidogo kidogo ni jambo la kawaida...wanawake wengine wanakauka haraka na wengine mpk siku 7..ni tofauti tu za kimaumbile.

Sijawahi kusikia tatizo la kuwa na 'vidonda' kwenye mji wa uzazi au kizazi na kusababisha maumivu makali wkt wa hedhi au hedhi kuwa kwa siku nyingi...mpeleke shemeji kwa daktari wa wanawake akachunguzwe na kupatiwa ushauri/matibabu huskika.
 
asante sana Dr. Riwa kwa ushauri wako ninaimani muhusiaka atachukua ushauri wako na kuufanyia kazi
 
mke wangu alijifungua mtoto mkubwa 5.5kg bahati mbaya, toka december 2011, anasema kuna mabadiliko asiyoelewa kama: 1)akikaribia kupata hedhi joto linapanda sana na anajisikia kama anaumwa akipima malaria hana
2)masaa machache kabla ya hedhi anajisikia kama kuna kitu kinajizungusha chini ya kitovu ambayo yana ambatana na maumivu
3)siku 3 za mwanzoni anatokwa na damu nyingi siku ya 4 na kwendelea damu inatoka kidogo kidogo yaani haikatiki, alipima hospitali akaambiwa ana vidonda kwenye mji wa uzazi akapewa dawa ya kumeza hedhi ikakatika, tatizo la hedhi mda mrefu lilijitokeza mwezi wa 5 na huu mwezi wa 6 anasema tatizo limerudi, hii ni siku ya7 damu inatoka kidogo kidogo haikatiki, na anapata maumivu chini ya kitovu. yanakuja na kupotea, kwa sasa hajatumia dawa yoyote
SWALI: je hili tatizo linatibika na linaweza kuathiri uwezekano wa mke wangu kupata uja uzito? Tupo mwanza, naomba msaada tafadhali.


Tafadhali kwa maswali na majibu ya kitaalam tembelea hii website: Wanetu.com :: Elimu kuhusu Ujauzito na Uzazi, Malezi na makuzi ya watoto, Afya ya watoto, Saikoljia, Tabia na Haki za Watoto
 
Back
Top Bottom