Mtambuzi kuna vifo vingi sana vya MANGULI ambavyo mpaka leo havijulikana vilitokeaje na kwa sababu zipi. Lakini, haraka haraka, na kwa kufikiri kipuuzi, nahisi kuwa vifo hivi hupangwa makusudi na makundi fulani fulani yenye interest fulani au yanayohisi kuwa uwepo wa watu fulani fulani unaweza kuhatarisha usalama wao au una interfere interest zao fulani!
Umewasahau akina Lucky Dube, aliyeuawa kwa risasi inasemakana na majambazi, lakini si kweli kwani hakuna kilichoibiwa wakati wa tukio na wengineo wengi. Hata hapa kwetu TZ kuna baadhi ya viongozi ambao pia vifo vyao vinanishangaza mpaka sasa. Mfano akina Daudi Balali, governor wa zamani wa bank kuu, Major General Imran Kombe, Hayati Horace Kolimba nk nk