Vifo vya wachezaji Tanzania, mamlaka zinachukua tahadhari zozote?

Vifo vya wachezaji Tanzania, mamlaka zinachukua tahadhari zozote?

benzemah

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2014
Posts
1,533
Reaction score
3,187
Jamii ya wapenda soka nchini ingali katika majonzi kufuatia kifo cha Mchezaji wa Mtibwa Sugar Iddy Mobby ambaye alifariki akiwa kwenye matibabu kwenye hospital ya Mkapa iliyopo mkoani Dodoma alipohamishiwa baada ya matibabu ya awali kwenye hospital ya kiwanda cha Mtibwa mkoani Morogoro.

Kwa mujibu wa taarifa toka Mtibwa Sugar, Iddy Mobby alianza kuumwa kichwa ghafla akiwa na wachezaji wenzake katika mazoezi binafsi (road work) na jitihada za matibabu sehemu mbalimbali hazikufanikiwa mpaka mauti yalipomkuta katika hospitali ya Benjamin Mkapa jijini Dodoma.

Hiki ni kifo cha pili kwa mwaka huu hapa nchini kwa wanasoka kufariki wakiwa katika maeneo yao kazi.
Mnamo January 19 mwaka huu, nahodha wa timu ya vijana chini ya umri wa miaka 17 wa Singida Big Stars Mohammed Banda alifariki. Banda alipoteza maisha alipofikishwa Hospitali ya Mkoa wa Singida muda mfupi baada ya kugongana kichwani na mchezaji mwenzake wakiwa mazoezini katika uwanja wa Magereza Singida

Ikumbukwe kwamba mwaka 2016 katika Ligi Kuu ya Vijana U-20 mchezaji wa Mbao Ismail Khalfan alifariki dunia Uwanja wa Kaitaba, Kagera pia Mshauri Salim wa Coastal Union U-20 alifariki dunia Uwanja wa Mkwakwani.
Japokuwa sote tunafahamu kuwa kifo ni mipango ya Mwenyezi Mungu lakini je mamalaka husika zinachukua hatua stahiki ili kupunguza madhara haya ama tutaendelea kusema kuwa ni mipango ya Mungu?

Mwenyezi Mungu aziweke roho za marehemu mahali pema peponi. Amen.
Screenshot 2023-03-07 at 15.22.50.png
 
Ukiacha hao wengine wa kugongana vichwa,suala la moyo kwa wachezaji uhusishwa na uvutaji wa bangi, mwenye elimu kuhusu Hilo atiririke
Kuna kipindi walisema watakuwa wanawapima sijui waliishia wapi?
 
Mimi nashauri wachezaji wawe wanapimwa afya zao mara kwa mara, na hasa kwenye hiki kipengele cha moyo. Maana kwa sasa vifo vya aina hii vimeongezeka duniani kote.
 
Iingilie kati nini?

Inajulikana mazoezi makali yanaua.Jipeni muda kuchunguza muone iwapo wachezaji huwa wanaishi miaka mingi kama Mzee Alli Hassan Mwinyi aliyelea kitambi akiwa Rais
 
Na mchezaji akifariki bongo hata hakumbukwi wenzetu kabla ya mechi hufanya hivyo huku ni mbele kwa mbele 🏌‍♂️
 
Mpira ni shughuli pevu cha kufuatilia ni lishe za wachezaji wetu.

Ni vizuri klabu zikiwapima wachezaji afya zao Kila mara.

Yule mchezaji wa zamani wa Yanga sijui nini kilimuondoa duniani, nani vile?
 
Tatizo hawajitunzi wenyewe pili hiv vilabu na viongoz wake n wanasiasa mpaka TFF nayo imejaa siasa tu Lishe tatu Lishe na usalama kwa wachezaji hamna unakuta mechi inachezwa liko li ambulance libovu liko kiushahidi tu
 
Kabla ya safari unacheki tairi, maji, breki, oil na kila kinachohitaji kuchekiwa still unapata breakdown, so acheni Mungu aitwe Mungu, kifo ni fumbo, huwezi kujihami nacho saa ikifika
 
Back
Top Bottom