Crocodiletooth
JF-Expert Member
- Oct 28, 2012
- 20,561
- 24,428
C&P,
From;-
#Kigogo! a.k.a mzushi.
Taarifa za kuaminika kutoka chanzo chetu ndani ya mahakama kuu ni kuwa kesi ya ubabaishaji iliyofunguliwa na kundi la mawakili wakiongozwa na Boniface Mwabukusi inayotegemewa kutolewa hukumu hivi karibuni IMEFYEKELEWA MBALI kwa kukosa vigezo na hoja zake hazijakidhi vigezo vya kuwa kesi ya kikatiba na kuonekana haina mashiko na ni usumbufu na kupotezea mida mahakama tukufu.
Kesi hiyo iliyofadhiliwa na kundi la watu wanaopinga uwekezaji bandarini wakiwemo GSM na Al Hushoom na kutoa kiasi cha 400m TZS ili kufunguliwa kwa kesi hii , imepata kipigo hicho baada ya hoja zao zote kutupwa kufuatia umahiri wa timu ya upande wa serikali ukiongozwa na mwendesha mashtaka mahiri wa serikali msomi Edson Mweyungee kuzifafanya na kuzijibu kwa ustadi mkubwa sana.
Kutupiliwa mbali kwa kesi hiyo kunadhihirisha uovu wa kikundi kidogo cha watu hasa wamiliki wa ICDs ambao kwa hila wanataka mchakato wa uwekezaji bandarini uvurugike ili waendelee kulinyonya hili taifa na kunufaika wao kupitia kampuni yao na mshirika wao TICTS
Ikumbukwe kuwa TICTS na Karamagi wameendesha bandari ya Dar Es Salaam kwa miaka 27 bila mafanikio ya maana kwa taifa na watanzania hii ikijumuisha kuingia mkataba wa hovyo uliogubikwa na rushwa wa miaka 15 ambao bunge liliazimia ufutwe mwaka 2008 lakini kwa kuwa rushwa ilitawala waliachwa mpaka sasa mkataba wao ulipoisha na kupewa mkono wa kwaheri jambo ambalo bado hawataki kuondoka na wameamua kufadhili vurugu.
Tunasubiri uamuzi wa mahakama kwa hamu sana ili tusonge mbele na uwekezaji wenye tija na faida kwa watanzania ufanyike na siyo kikundi cha wachache kama ilivyokuwa kwa miaka hiyo 27.
N.B,IKUMBUKWE HUKUMU YA SHAURI HILI LILIHAIRISHWA.
From;-
#Kigogo! a.k.a mzushi.
Taarifa za kuaminika kutoka chanzo chetu ndani ya mahakama kuu ni kuwa kesi ya ubabaishaji iliyofunguliwa na kundi la mawakili wakiongozwa na Boniface Mwabukusi inayotegemewa kutolewa hukumu hivi karibuni IMEFYEKELEWA MBALI kwa kukosa vigezo na hoja zake hazijakidhi vigezo vya kuwa kesi ya kikatiba na kuonekana haina mashiko na ni usumbufu na kupotezea mida mahakama tukufu.
Kesi hiyo iliyofadhiliwa na kundi la watu wanaopinga uwekezaji bandarini wakiwemo GSM na Al Hushoom na kutoa kiasi cha 400m TZS ili kufunguliwa kwa kesi hii , imepata kipigo hicho baada ya hoja zao zote kutupwa kufuatia umahiri wa timu ya upande wa serikali ukiongozwa na mwendesha mashtaka mahiri wa serikali msomi Edson Mweyungee kuzifafanya na kuzijibu kwa ustadi mkubwa sana.
Kutupiliwa mbali kwa kesi hiyo kunadhihirisha uovu wa kikundi kidogo cha watu hasa wamiliki wa ICDs ambao kwa hila wanataka mchakato wa uwekezaji bandarini uvurugike ili waendelee kulinyonya hili taifa na kunufaika wao kupitia kampuni yao na mshirika wao TICTS
Ikumbukwe kuwa TICTS na Karamagi wameendesha bandari ya Dar Es Salaam kwa miaka 27 bila mafanikio ya maana kwa taifa na watanzania hii ikijumuisha kuingia mkataba wa hovyo uliogubikwa na rushwa wa miaka 15 ambao bunge liliazimia ufutwe mwaka 2008 lakini kwa kuwa rushwa ilitawala waliachwa mpaka sasa mkataba wao ulipoisha na kupewa mkono wa kwaheri jambo ambalo bado hawataki kuondoka na wameamua kufadhili vurugu.
Tunasubiri uamuzi wa mahakama kwa hamu sana ili tusonge mbele na uwekezaji wenye tija na faida kwa watanzania ufanyike na siyo kikundi cha wachache kama ilivyokuwa kwa miaka hiyo 27.
N.B,IKUMBUKWE HUKUMU YA SHAURI HILI LILIHAIRISHWA.