Vijana angalieni fursa hii

Vijana angalieni fursa hii

Leo ningependa kuwapa zawadi vijana wenzangu watizame hii fursa watakuja kunishukuru badaye.

Tatizo la vijana tulio wengi ni kuharakia maisha tunapenda kupata leo leo, jambo ambalo linapelekea kua na maisha magumu sana kila siku na tunaishia kufa maskini.

Ni wachache sana wanaofanikiwa kwa shortcut na shortcut zinatugharimu sanna kwanini usitumie hii fursa.

Maeneo ya kusini heka kumi nimenunua kwa million 1 tu.

Nilichofanya nimesafisha shamba na kupanda mikorosho 490.

Kisha nikawakatia vipande wana kijiji nikawambia limeni eneo hili bure kwa lengo la kulinda mikorosho.

mwaka jana ndio ilikua mwaka wa nne tangu nipande mikorosho, nimekwenda kuvuna korosho tani 17 na nikauza kwa bei ya elf 1500 kuwauzia serikali ambao hua na maghala ya kununua korosho karibu na shamba langu la mikorosho nimelipwa mil 25.

Nimewaza sanna tunahangaika na kutaka kukaa mjini tu ila fursa zipo na zipo nyingi zinazofanana na hizi.

Asanteni
Hongera sana sana mkuu, kuna 75% ya andiko kwenda katika ukweli ila kuna mambo kama mdau au mtaalamu ninaona kama haujaweka sawa, sasa ni aidha sio taaluma yako au kuna kitu unaficha.
Nitapita baadhi ya maswali
 
Ekari inachukua mikorosho mingapi?
Mikorosho ya kizamani inaingia kuanzia mikorosho 28 ikiwa utatumia space ya 12mx12m au mikorosho 40 ikiwa unatumia 10mx10m

Ila kama una mbegu za kisasa ambazo ni dwarf na unaweza kuuproot/kupogolea baadhi ya miti unaweza kiweka haya miti 100 ikiwa utatumia space ya 5mx8m au miti 63 ikiwa utatumia 8mx8m.
 
Kwa kua umeamua kutupa dili basi fafanua vizuri ili tujue tunaanzia wapi,
Shamba umesema Milion 1
Mbegu?
Mbolea?
Palizi?
Dawa?
Muda wa kupanda?
Muda wa Mavuno?
Tupe mchanganuo mzuri tujiandae.
kuhusu mbegu nilikwenda kuangalia shmaba lipi linazaa sana nikachukua korosho nikaenda kupanda, sikutumia mbolea wala dawa isipokua baada ya kupanda niliwapa wanakijiji wanotaka kulima mazao yao walime bure ili niweze kuilinda miche ya mikorosho
muda wa mavuno ni mara moja inakua mwezi wa tisa mpaka mwezi wa 12
 
kwa mwaka jana bei ya korosho haikua nzuri na pia mikorosho bado haijawa mikubwa hivyo mwakani inshaallah bei ikiwa nzuri na mikorosho itazaa zaidi hivyo naweza pata zaidi ya mil 25
Korosho ghafi haijawahi kuwa stsble na msimu wetu uko kipindi kibaya sana kuliko mataifa mengine.
 
kuhusu mbegu nilikwenda kuangalia shmaba lipi linazaa sana nikachukua korosho nikaenda kupanda, sikutumia mbolea wala dawa isipokua baada ya kupanda niliwapa wanakijiji wanotaka kulima mazao yao walime bure ili niweze kuilinda miche ya mikorosho
muda wa mavuno ni mara moja inakua mwezi wa tisa mpaka mwezi wa 12
Hapa ndio kwenye majibu tata kuhusu harvest brother.
 
Hapana nakukatalia na mbaya zaidi umetumia local seeds. Ungekwenda Naliendele aidha kupata certified seeds au kupata utaalamu wa kubebesha ungeweka hizi namba
kwa taarifa huku vijijini wanatumia mbinu zao na hawafuati kilimo cha kisasa nilitaka kufanya kilimo cha kisasa ila niksjiiza mbona hawa wanafanimiwa kjna watu wanamikorosho inazaa mpaka 60 kg kwa kila mkorosho mmoja
 
Back
Top Bottom