Vijana na afya: Tufike miaka 90+

Vijana na afya: Tufike miaka 90+

Termux

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2017
Posts
429
Reaction score
1,031
Babu yangu is now 90+, alipataga stroke lakini aliwahiwa ikapona kabisa sahiv anakata majani analisha ng'ombe zake mzima kabisa.

Kwasababu ya umri tu, masikio yana shida lakn ukiongea kwa sauti anakusikia na stori zinaendelea vizuri tu...

Nikamuuliza babu Zaman mliishije (chakula)
akasema sisi hatukuwa tunajua vitafunwa vyenu vya sasa... asubuhi unakula viazi/ viazi vitamu/ mihogo/ magimbi/ karanga/ maboga mchemsho na maziwa fresh/ mtindi/ uji wa ulezi/ dona.

Kama ni chai basi ni majani ya mchaichai,limao,mchungwa, tangawizi, au mizizi na ladha ya asali...unaenda zako shamba au shughuli zako kawaida, mchana mnakula ugali wa dona/ mtama/ muhogo na mboga za majani nyingii, mtindi, mboga zinaungwa kwa mafuta ya mawese au makweme au karanga za kupondwa..
Wali tunakutana nao pasaka kwa Christmas.

Ebu angalia ninyi sahiv mnavyokula, ngano iliyokobolewa maandazi/chapati/n.k... ndo asubuhi hio..unategemea akili itapata wapi afya yakufikiria mambo?

Mchana mnakula sembe chips wali na masoda yenu hayo... mwili utapata wapi nguvu ya kufanya kazi, mnaishia mmekaa kutwa nzima mnaangalia T.V mnaharibu miili yenu bila sababu, kesho na kesho kutwa pressure, moyo, mifupa vinaanza kuwasumbua. Mnachakaa mapema, mnazeeka mapema mnachoka mapema kabisa.

Lakini mimi na hii98 yangu, macho yangu mazima, meno yangu yapo yote, masikio ndo yanashida kidogo lkn nasikia, nakumbuka vizuri tu, badilishen mtindo wenu wa maisha ya mezani 🤔☹️
 
Mkuu siku hizi shida sio chakula tu, kuna vitu vingi vinavyoharibu afya zetu ukiringanisha na zamani

-Magonjwa: kuna magonjwa mapya mengi sana pia ni sugu kutibika sio sawa na zamani. Mfano ma-UTI, sjui Gonnorea

-Madawa yanayotumika tu kutibu magonjwa mbalimbali hospital ni sumu kwa namna moja au nyingine. Mfano dawa za UTI na Zile mseto sjui za Malaria, kama ushawahi tumia utajua ni nn nazungumzia

-pia baadhi ya njia za matibabu eg X ray and ultrasound na tiba zinazohusisha mionzi pia zina athiri Afya zetu indirectly

-Dawa za meno, mafuta ya ngozi, sabuni tunazotumia n.k vyote hivyo ni kemikali zinazoathiri afya zetu.

-Electromagnetic waves: Mionzi ya mitandao ya simu na redio inaleta athari kwenye afya zetu bila sisi kujua.

-Matumizi ya mbolea za kisasa na pesticides za kuua wadudu mashambani zinapelekea vyakula tunavyokula kuwa na kemikali sumu nyingi tu zinazoathiri afya zetu.

-Maji tu unayotumia bombani yanafanyiwa chlorination (uongezwaji wa kemikali za kuua vijidudu) kemikali hizi pia zinaweza kua na athari kwenye miili yetu.

Hvyo ukibase kwenye chakula tu unakua unakosea, kuna factors nyingi sana zinazosababisha kizazi hiki kuwa na afya duni au maisha mafupi ukilinganisha na miaka ya zamani.
 
Mkuu siku hizi shida sio chakula tu, kuna vitu vingi vinavyoharibu afya zetu ukiringanisha na zamani

-Magonjwa: kuna magonjwa mapya mengi sana pia ni sugu kutibika sio sawa na zamani. Mfano ma-UTI, sjui Gonnorea..
Asante boss naona umenifumbua kitu kingine hapa ambacho sikukifikilia mwanzo, asante sana ndugu
 
Asante boss naona umenifumbua kitu kingine hapa ambacho sikukifikilia mwanzo, asante sana ndugu
Mambo ni mengi sana dunia ya sasa!

Unaweza sema ule mihogo ma magimbi tu kumbe yamejaa kemikali za mboleaa😂😂
 
Back
Top Bottom