Vijana rudini vijijini mkawasaidie wazee

Vijana rudini vijijini mkawasaidie wazee

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
33,679
Reaction score
49,841
Wazee wameachwa katika mazingira magumu huko vijijini, unakuta mzee mpaka mgongo umepinda analima shamba kubwa kwa jembe la mkono, anachunga mifugo, anapasua magogo ya kuni n.k Ukiwauliza kuhusu watoto/vijana wao, wanasema wamekimbilia mjini kutafuta maisha, na wengine wanazaidi ya miaka 10 hawajarudi vijijini.

Sasa ndugu zangu huu sio uungwana, kumuachia mzee wa miaka 75 shamba alime kwa jembe la mkono, wakati wewe kijana mwenye nguvu uko huko mjini unazunguka zunguka tu.

Kwa hiyo nawasisitiza, vijana rudini vijijini mkawasaidie wazee
 
𝗜𝗹𝗮 𝗧𝗮𝗻𝘇𝗮𝗻𝗶𝗮 𝗻𝗶 𝗻𝗰𝗵𝗶 𝗮𝗺𝗯𝗮𝘆𝗼 𝗶𝗺𝗲𝘀𝗵𝗶𝗻𝗱𝗶𝗸𝗮𝗻𝗮, 𝗸𝗶𝗹𝗮 𝗸𝘂𝗸𝗶𝗰𝗵𝗮 𝗺𝗻𝗮𝗳𝘂𝗻𝗴𝘂𝗮 𝗻𝘆𝘂𝘇𝗶 𝘇𝗮 𝗸𝘂𝘀𝗲𝗺𝗮 𝗸𝗶𝗷𝗮𝗻𝗮 𝘂𝘁𝗮𝗸𝗮𝗮𝗷𝗲 𝗵𝗼𝗺𝗲 𝗻𝗮 𝗸𝘂𝘀𝗲𝗺𝗮 𝗵𝘂𝗼 𝗻𝗶 𝘂𝗷𝗶𝗻𝗴𝗮 𝗹𝗲𝗼 𝗵𝗶𝗶 𝗻𝗮𝘄𝗲 𝘂𝗻𝗮𝗽𝗼𝗻𝗱𝗮 𝘁𝗲𝗻𝗮
 
Wazee wameachwa katika mazingira magumu huko vijijini, unakuta mzee mpaka mgongo umepinda analima shamba kubwa kwa jembe la mkono, anachunga mifugo, anapasua magogo ya kuni n.k Ukiwauliza kuhusu watoto/vijana wao, wanasema wamekimbilia mjini kutafuta maisha, na wengine wanazaidi ya miaka 10 hawajarudi vijijini.

Sasa ndugu zangu huu sio uungwana, kumuachia mzee wa miaka 75 shamba alime kwa jembe la mkono, wakati wewe kijana mwenye nguvu uko huko mjini unazunguka zunguka tu.

Kwa hiyo nawasisitiza, vijana rudini vijijini mkawasaidie wazee
Wewe uko mjini au kijijini? Tuanzie hapo.

Sent from my TECNO LA6 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom