Vijana tukumbushane kama sio kuelimishana maana Giza lipo karibu

Vijana tukumbushane kama sio kuelimishana maana Giza lipo karibu

mriringa

JF-Expert Member
Joined
Jan 17, 2017
Posts
663
Reaction score
714
Wakati unamlaumu mzazi kuwa maskini jiulize wewe hadi Sasa unapambanaje na umaskini hasa wa familia Yako au nawewe unasubiri uje usemwe na wanao??

Tanzania tumejaliwa kuwa na maeneo mengi ya kilimo kwa kila mkoa lakini maeneo hayo yapo wazi hakuna zao lolote. Ngoja niwasanue vijana wenzangu baada ya miaka 10 ijayo kupata ardhi hata eka 5 itakuwa ngumu sana.

Nini Cha kufanya?? Kama kwenu Kuna maeneo ya familia anza kuwekeza hata kwa kupanda miti au mazao ya kudumu yatakusaidia baadae na bado utakuwa unalinda ardhi Yako.

Najua hatuna mitaji SAWA ila kama afya unayo ya kutosha basi huo ni mtaji mkubwa sana kwenye uwekezaji mdogo mdogo.

Vijana tupambane kumiliki ardhi Giza likitanda tutakuja kulia na kusaga meno. Kula ujana leo ila kumbuka na kesho.
 
Wakati unamlaumu mzazi kuwa maskini jiulize wewe hadi Sasa unapambanaje na umaskini hasa wa familia Yako au nawewe unasubiri uje usemwe na wanao??

Tanzania tumejaliwa kuwa na maeneo mengi ya kilimo kwa kila mkoa lakini maeneo hayo yapo wazi hakuna zao lolote. Ngoja niwasanue vijana wenzangu baada ya miaka 10 ijayo kupata ardhi hata eka 5 itakuwa ngumu sana.

Nini Cha kufanya?? Kama kwenu Kuna maeneo ya familia anza kuwekeza hata kwa kupanda miti au mazao ya kudumu yatakusaidia baadae na bado utakuwa unalinda ardhi Yako.

Najua hatuna mitaji SAWA ila kama afya unayo ya kutosha basi huo ni mtaji mkubwa sana kwenye uwekezaji mdogo mdogo.

Vijana tupambane kumiliki ardhi Giza likitanda tutakuja kulia na kusaga meno. Kula ujana leo ila kumbuka na kesho.
Huu Uzi vijana tunaukwepa sana ila muda ni rafiki
 
Umasikini Ambao upo Tanzania ni imaskini wa Bandia.

MTU yeyote mwenye Afya ya mwili na akili then akawa masikini basi either the system is leak . mfumo aliopo unavuja .
 
Back
Top Bottom