Vijana tulio kwenye ndoa tujifunze kusuluhisha ndoa zetu wenyewe

Vijana tulio kwenye ndoa tujifunze kusuluhisha ndoa zetu wenyewe

Librarian 105

JF-Expert Member
Joined
May 6, 2023
Posts
261
Reaction score
356
Hakuna ndoa isiyo na mitihani na mikwaruzano. Kinachovunja ndoa nyingi ni mke au mume kuwa kispika cha kueleza changamoto za mwenzi wake kwa ndugu na jamaa bila kujali wakati sahihi wa kufanya hivyo.

Akisahau hata huko anakokwenda kutafuta msaada nako huenda moto unawaka zaidi kuliko ndani ya kuta za chumba chenu Kwa baadhi ya nyakati. Ila watu hao huishia kusameheana na kuanza ukurasa mpya wa maisha yao.

Ndoa haiitaji ubabe na kiburi cha kuonyeshana umwamba au kuchuniana ndani ya nyumba moja huku kila mtu akishika hamsini zake Kwa kivuli cha watoto eti watataabika mkiachana.

Kabla ya kwenda kuanika siri za mke au mume wako tafakari dunia ya sasa jinsi ilivyojaa hasadi na unafiki hadi kwenye nyumba za ibada. Sio kila anayekusikitikia machoni ni vivyo hivyo alivyo moyoni mwake.

Tafakari : wazazi wetu waliishije kwenye ndoa zao hadi wengine kuzikana? Kanuni ni moja : kushikamana kwenye yale mazuri ya mwenzi wako na kurekebishana katika yale mapungufu yenu yasiyofungamana na matendo yenye kwenda kinyume na misingi ya kujenga ndoa.

Mwisho, basi na mkiamua kuachana, sitirianeni madhaifu yenu ili tujenge jamii isiyo na visasi, chuki na kikomoana.

Asanteni
 
Kinachovunja ndoa nyingi ni mke au mume kuwa kispika cha kueleza changamoto za mwenzi wake Kwa ndugu na jamaa bila kujali wakati sahihi wa kufanya hivyo.
NDOA za siku hizi ni NDOANO. Ni rahisi wapenzi kushikana ila ni ngumu kushikiana Simu.

Wanawake wamekuwa viburi na Wanaume wamekuwa kama Mabinti(kutwa wanalalamika kwenye vitu walivyotakiwa kufanya maamuzi").

Naungana na hoja yako ya wapenzi kusuluhisha matatizo yao wenyewe, na hili litawezekana endapo MWANAUME atakuwa ni mtu wa MAAMUZI katika NDOA yake.
 
Ni muhimu sana kufahamu madhaifu ya mwenza wako na kuyabeba, hii itasaidia kumsitiri ndani na nje.

Ni muhimu sana kufahamu kuwa kama wewe mhusika mkuu limekushinda basi hata huko unakoenda kutafuta msaada hutoupata na ukiupata hautokuwa umekidhi haja yako.

Ndoa ili iweze kutulia inahitaji msingi wa mapenzi na huruma.

Muhimu: Hakuna ndoa inayokosa changamoto.
 
Hakuna ndoa isiyo na mitihani na mikwaruzano. Kinachovunja ndoa nyingi ni mke au mume kuwa kispika cha kueleza changamoto za mwenzi wake kwa ndugu na jamaa bila kujali wakati sahihi wa kufanya hivyo.

Akisahau hata huko anakokwenda kutafuta msaada nako huenda moto unawaka zaidi kuliko ndani ya kuta za chumba chenu Kwa baadhi ya nyakati. Ila watu hao huishia kusameheana na kuanza ukurasa mpya wa maisha yao.

Ndoa haiitaji ubabe na kiburi cha kuonyeshana umwamba au kuchuniana ndani ya nyumba moja huku kila mtu akishika hamsini zake Kwa kivuli cha watoto eti watataabika mkiachana.

Kabla ya kwenda kuanika siri za mke au mume wako tafakari dunia ya sasa jinsi ilivyojaa hasadi na unafiki hadi kwenye nyumba za ibada. Sio kila anayekusikitikia machoni ni vivyo hivyo alivyo moyoni mwake.

Tafakari : wazazi wetu waliishije kwenye ndoa zao hadi wengine kuzikana? Kanuni ni moja : kushikamana kwenye yale mazuri ya mwenzi wako na kurekebishana katika yale mapungufu yenu yasiyofungamana na matendo yenye kwenda kinyume na misingi ya kujenga ndoa.

Mwisho, basi na mkiamua kuachana, sitirianeni madhaifu yenu ili tujenge jamii isiyo na visasi, chuki na kikomoana.

Asanteni
Hakika.Kama mmeshindwa usuluhishi ninyi mnaojuana kiundani zaidi Nani atakae wapatanisha? Jibu hakuna, kila mmoja awajibike katika nafasi yake ipasavyo. 🦅GirlTalk
 
Hakuna ndoa isiyo na mitihani na mikwaruzano. Kinachovunja ndoa nyingi ni mke au mume kuwa kispika cha kueleza changamoto za mwenzi wake kwa ndugu na jamaa bila kujali wakati sahihi wa kufanya hivyo.

Akisahau hata huko anakokwenda kutafuta msaada nako huenda moto unawaka zaidi kuliko ndani ya kuta za chumba chenu Kwa baadhi ya nyakati. Ila watu hao huishia kusameheana na kuanza ukurasa mpya wa maisha yao.

Ndoa haiitaji ubabe na kiburi cha kuonyeshana umwamba au kuchuniana ndani ya nyumba moja huku kila mtu akishika hamsini zake Kwa kivuli cha watoto eti watataabika mkiachana.

Kabla ya kwenda kuanika siri za mke au mume wako tafakari dunia ya sasa jinsi ilivyojaa hasadi na unafiki hadi kwenye nyumba za ibada. Sio kila anayekusikitikia machoni ni vivyo hivyo alivyo moyoni mwake.

Tafakari : wazazi wetu waliishije kwenye ndoa zao hadi wengine kuzikana? Kanuni ni moja : kushikamana kwenye yale mazuri ya mwenzi wako na kurekebishana katika yale mapungufu yenu yasiyofungamana na matendo yenye kwenda kinyume na misingi ya kujenga ndoa.

Mwisho, basi na mkiamua kuachana, sitirianeni madhaifu yenu ili tujenge jamii isiyo na visasi, chuki na kikomoana.

Asanteni
Sahihi.

Mke wa binadamu yangu alitoroka na kwenda Kwa kaka yake kisa binamu hakulala nyumbani kwake siku Moja tu!

Alipofika tu hata hajala Bado wifi yake (mke wa kaka yake) akaanza kumwambia wife ahsantee kabisa umekuja kaka Yako kashabarika Leo anaenda wiki bila kulala nyumbani anakuja tu kama mgeni akitoka harudi Tena.

Alisononeka sana moyoni mwako Wala hakumwambia kilicho mleta sana sana alijipongeza tu kumbe kwangu Kuna unafuu Hivi!!??


Mimi sijawahi piga wife....Kuna siku alizingua nilimuaru afate fimbo akafata nikamwambia lala nikuchalaze alipotii kulala nguvu za kumpiga ziliisha nikamwambia nyanyuka na usirudie Tena!

Hadi Leo ni mbunye mbune tu akoseka hata kidogo tu atahakikisha ameliweka sawaaaa.





Nje na maada una dasi hapo mkuu Hali sio rafiki Kwangu Leo?
 
Umeongea vyema sana,nijubu hili unaweza kufichaje siri ya mke wako anaekopa kopa hela kwa watu na kuomba omba ,pesa haileweki anapeleka wapi,muongo mkubwa,akiona fedha anachangany8kiwa,na habadiriki wala hana dalili ya kubadirika,ukikaa navyo moyoni si utakufa mapema tu.
 
Ni wanaume wachache sana watasamehe mke mgawaji, Nadhani Wanawake wamekuwa wagawaji mno. Kitu kidogo tu keshagawa kwa boss, mara kwa jirani kwa sababu za kijinga jinga tofauti kidogo na sisi wa wanawake wa zamani, Wanavumilika sababu hawafanyi kosa la kugawa hovyo akagundulika.

Sasa hv kijana analeta kesi amekuta sms za mahaba kwenye simu ya mkewe? Yaani mwanamke anakuwa jasiri kiasi kwamba hata sms hafuti.
 
Umeongea vyema sana,nijubu hili unaweza kufichaje siri ya mke wako anaekopa kopa hela kwa watu na kuomba omba ,pesa haileweki anapeleka wapi,muongo mkubwa,akiona fedha anachangany8kiwa,na habadiriki wala hana dalili ya kubadirika,ukikaa navyo moyoni si utakufa mapema
Sahihi kabisa. Ndio maana nimesema ni Kwa zile changamoto tu ambazo haziharibu misingi ya ndoa. Type hiyo, braza, utakuwa unaishi na mjasiriamali badala ya mwenzi.
 
Back
Top Bottom