Vijana wa kiume kuweni makini na style za nywele mnazonyoa

Juzi hapo Mlimani kwenye graduu ya Chuo cha WDMI mgeni rasmi Waziri wa Maji, Jumaa Oweso, anaitwa wakaitwa madogo watunukiwe kaja dogo amempiga kiduku sio cha nchi hii.

Mh mbona alimtolea uvivu. Mbele za wageni, hightable watu wakajua dogo ataambiwa wewe utagraduate mwakani. Ila jamaa akamtunuku na yeye.

Kunyoa sawa ila kuna baadhi ya matukio bora kustay low.
 
Mi nasema huo ni wivu tu nyie wazee mnaona kwa vijana, staili ya nywele ina impact gani kwenye maisha ya mtu?. Alafu style ya nywele inaendana na kazi ya mtu huwezi nambia fundi welding, boda boda, fundi ujenzi au mpiga debe eti anyoe kama wakili, mwalimu and other professional careers. Nasema hvi wazee acheni wivu ,kubalini hali zenu. Mbona vijana wamekaa kimya hawasemi topolo zenu mnazofanya katika jamii ...........
 
Dah... Huu ndiyo ukandamizaji ambao CDM wanapigia kelele kila siku… kila mmoja anahaki ya kuweka kichwa chake vile ambavyo anataka kwani haimuathiri yoyote...denge langu hili nimeanza kulinyoa tokea mwanzoni mwa miaka ya 50s...hakuna aliyewahi kuniuliza...Sasa wewe ni nani hasa hadi uanze kupigia kelele stail za minyoo ya watu?......Acha ukoloni 😎
 
Mtoto umfundishe kuhesabu machungwa.

Unampa kazi ya kuhesabu machungwa anakwambia hajui.

Ndivyo uombavyo picha kwenye uzi uliojitosheleza maelezo yake.
Weka picha ya kijana aliyenyoa kihuni na mm nikulipe ya mzee aliyenyoa ivoivo,nyie wazee wa sikuhizi mnashindana na vijana kwenye almost kila kitu sio wanawake sio nini,ukiona amekuzidi kete sehemu unatafuta namna ya kulalamika,..oooh sijui vijana wa sikuhizi wahuni,ebu zeekeni asee
 
Sasa kama huyu akikua utamlaumu kijana wakati baba yake ana miaka zaidi ya 45 na anamnyoa hivi
 
Fundisha watoto wako. Wengine waache.

Nchi ina mamilioni ya watoto, ukiumiza kichwa kwa mambo ya watu baki, shughuli zako utanya saa ngapi?
Duh,
Sasa ikiwa ivi, ni uchoyo wa maarifa semea pale inapowezekana.
 
tunalaumiwa vijana ila ukienda kwenye jeshi la polisi utakuta asilimia kubwa ya wazeee huko wana viduku, afro na ma-panki!.

Your Era is gone elders! Leave Us in Peace, we will handle our era in our own modern ways!..

Imagine Kim Jong Ur ana kiduku, trump anacho ila kwakua si wazee wetu mkizeeka mnatoka upaa basi mnatung'ong'a kinoma utafikiri si ndo tumewaletea huo upaa!.. na yanavong'aaga ntakuja kumtia kibao mmoja akinidiss sana.

Anyway hua tunawaheshimu tu, ila haimaanishi tunawaogopa.
Jaribuni kuelewa kua these arent your times!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Maelezo na picha
 
Mtoto wa miaka miwili ananyokewa kiduuku na wei juu
 
“Kumbukeni nguvu ya elimu uonekana pale inapotumika kwako na kwa watu wengine” Ahsante.
 
wahenga mnatakiwa mtambue..huo ndo utandawaz hata nyie enz zenu mlikua mnavaa mawigi.surual za kubana chini zinamwaga kama hz wanazovaa akina dada waleo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…