Acheki kuvunja watu moyo, kama wewe umeona kuwa hiyo kazi haikufai kaa kimya, hata kama ingekuwa kazi ya kuuza maseni mbona kuna watu wanifanya?
Tuache tabia ya kudharau kazi, huwezi kujua kuwa ktk kazi hizo za kuuza vyombo ndio sehem wengine wanatokea.
Kuna jamaa yangu mmoja kule Mwanza wakati nasoma alini support sana. Yeye alianza ktk kampuni hizi za kuuza vyombo vya majumbani kama mechandizer yeye alichokifanya alichukua ile knowledge aliyoipata pale baada ya miezi mitatu akaacha ile kazi akawa anaenda kununua hivyo vyombo kwenye maduka ya jumla kisha anaenda anawauzia watu mtaani, baada ya muda mtaji ukakua akawa anapeleka vitu mikoa Mara, Bukoba na Shinyanga. Kwa sasa ni ana duka lake kubwa amejenga nyumba Mwanza anaishi huko.
Wito wangu: Tuache tabia ya kudharau kazi kama wewe unaona haikufai acha wengine wafanye.
Thanks