Vijana wataka umri wa kustaafu upunguzwe hadi miaka 50

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Wakati suala la ajira, kuboresha elimu, matumizi ya teknolojia vikitawala, vijana wametaka dira ya Taifa 2050 ipunguze umri wa watu kustaafu kwa lazima hadi kufikia miaka 55 kutoka 60.

Hayo yamesemwa leo Desemba 18, 2024 wakati vijana wakitoa maoni yao kwenye rasimu ya Dira ya Taifa 2050 iliyozinduliwa Desemba 11, 2024 na Rais wa Zanzibar, Dk Hussein Mwinyi.

Akizungumza katika kongamano hilo, mratibu wa makongamano ya ukusanyaji maoni Sera ya Vijana, Omary Pumzi amesema katika mikutano mingi iliyofanyika, vijana wametaka kuona umri huo unapungua ili kuacha fursa kwao.

“Sasa hivi umri wa kustaafu ni miaka 55 kwa hiari na 60 kwa lazima, vijana wanataka umri huo ushuke hadi miaka 55 kwa lazima na 50 kwa hiari, hii miaka michache inayobakia vijana waitumie kufanya kazi na kujipatia kipato,” amesema.
 
55 bado ni mingi, iwe 50. Ili mpishano wa nafasi za kazi uongezeke.
 
Kupunguza miaka ya kustaafu haisaidii wasio na ajira wakazibe nafasi zao....hao wanaofikisha miaka 50 kwa nchi nzima wanaweza wasikifike hata 5000 na wanaohitaji ajira kwa mwaka ni zaidi ya laki moja....la kufanya ni kuweka Sera nzuri na sheria zinazotekelezeka za kuwasaidia vijana kujiajiri.
 
Jiajirini mbwa nyinyi mbona wengine hatujawahi kuajiriwa licha ya kuwa tulimaliza vyuo fresh ondokaneni na hiyo mindset ya kuajiriwa mtakuja kunishukuru ngiri nyinyi
Kiburi ama EGO yako Iko kichwani mwako so unajiona u mjanja kuliko ambao hawajakufanana.
Elewa ulivyoumbwa kichwani mwako ni tofauti na wengine walivyo.

Maturity is respecting our differences.
Unajiona kuwa ni akili zako ndizo zimekufikisha hapo unajua ni wangapi wanaweka mahali Ila haizai na inakufa since none knows tomorrow
 
Miaka 50 nikikukaba koo huchomoki
Tukale wapi sasa
Vijana nyie ndio wa kubuni ajira kama wenzenu wa nchi zilizoendelea kwani ajira nyingi watu ndio wanabuni na sio serikali kama mnavyojiaminisha
Kila unachoona kimebuniwa
Kwa sasa tunaenda kwenye Xmas na mwaka mpya kuna makampuni nje wana mchango mkubwa kwenye kodi
Kadi zinachapishwa kibao kuanzia Xmas, New Year, halafu inakuja Valentine zote hizo ni akili za ubunifu wa vijana wa nje
Sasa nyie mnawaza kustaafisha watu badala ya kuvumbua vitu ili ajira zipatikane kwa wingi
Nilipo kuna ajira zaidi ya 250,000 kwa siku za kila aina
Sasa sijui nyie mna ajira ngapi zinazotoka kila siku

Amkeni mtafakari mnakwama wapi
Ajira sio Boda tu
 
Jiajirini mbwa nyinyi mbona wengine hatujawahi kuajiriwa licha ya kuwa tulimaliza vyuo fresh ondokaneni na hiyo mindset ya kuajiriwa mtakuja kunishukuru ngiri nyinyi
Kama wewe umejiajiri kwa povu hili basi kiukweli TZ ni chaneli ya vichekesho mbinguni,

Ubinadamu ni kazi/The humanity is work.
 
umeongea point sana mkuu, tatizo watu wanafikiri serikalini ndio kuna ajira nyingi wkt unakuta wafanyakazi wa serikali kwa nchi nzima hawafiki hata milioni moja
 
Point ya msingi inatakiwa wanasiasa ndio wastaafu na miaka 50 kwa sababu wao sio wataalam
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…