Vijana wengi tunaibiwa kwa uvivu kupitia nafasi za ufadhili wa masomo nje

Vijana wengi tunaibiwa kwa uvivu kupitia nafasi za ufadhili wa masomo nje

Prezoo255

New Member
Joined
Oct 2, 2018
Posts
2
Reaction score
2
Kuna wimbi la watu wengi wanaelezwa juu ya nafasi za ufadhili wa masomo ya juu kwa ngazi tofauti na mashirika mbali mbali.

Mara nyingi kwa kutumia lugha za biashara mfano
"Scholarship opportunities upto 50%"

Watu wamekuwa wakikimbilia fursa hizi na kupatiwa nafasi vyuo mbali mbali nje ya nchi na kuwalipa mashirika yale yanayowapatia nafasi hizo.

Naweza kusema vijana wengi tumekua wavivu kufanya utafiti wa vyuo hivi au hata kutafta kujua kama scholarship hizi ni za kweli, hali hii inapelekea vijana wengi kwenda kati vyuo hivi na kuwapa mzigo familia zao kwa gharama ambazo ni sawa na kusomea nchini tu tena kwa amani

Kwani kiuhalisia hizi 50% scholarships sio za kwel kwani unakuta hio gharama unazoambiwa ni 50% ndizo gharama halisi za vyuo hivyo na unajikuta umemlipa mtu kwa ajili ya kukufanyia application ambayo ungeweza kufanya mwenyewe kwa kuwasiliana na vyuo husika.

Vijana tujitahidi kutumia mitandao kwa ajili ya kujisaidia na tusiwe wavivu na walimbukeni wa mitandao na teknolojia kwani tunakua tumesoma ila hatujaelimika .

#prezoo255
 
Basi sawa link za scholarship hizi hapa anza kufanya maombi:
 
Back
Top Bottom