Vijana wengi wa Kitanzania ni wavivu kupindukia, wanataka mteremko

Vijana wengi wa Kitanzania ni wavivu kupindukia, wanataka mteremko

Mwaka 2015 nilifanya maamuzi ya kutafuta shamba, Mungu mwema nikapata ekari 3 na nusu. Tangia hapo mpaka leo nimehangaika na hilo shamba kulibadilisha from pori, visiki, miiba, kupishana na majoka humo na majanga mengine mengi. Nimelilima kwa maana ya kulisafisha sasa ni safi pyeeeeeeeeeeeee.

Kipindi hicho nanunua, alikuwepo rafiki yangu ambaye nilikuja kugundua baadaye kuwa japo tuna fursa wote, maana tumeajiriwa, tuna mitazamo tofauti. Yeye hakuona haja ya kujihangaisha kote huko. Anapenda maisha flani ya kufanikiwa kimishen town hivii. Baada ya kusafisha shamba, mwaka jana nikaanza ujenzi wa nyumba ndogo hapo, maana mimi siamini katika kilimo cha remote control. Nataka niishi hapo hapo, nilime na niliangalie shamba langu. Mwaka huu niko kwenye harakati za kutoboa maji chini (drill)... Mungu akipenda kabla ya April nitakuwa nimefanikisha.

Sasa jamaa yangu amenijia, anataka tulime kwa utaratibu wa ubia. Eti tuchangie gharama za kilimo(mbegu, mbolea, dawa, palizi etc). alafu tugawane mavuno ya hicho tutakachopanda (iwe ni nyanya, tikiti, vitunguu etc.). Nimemwangalia hata simmalizi yaani, natamani nimjibu nahisi naweza kumtukana. Wote tuna mishahara, na kila mmoja ana uwezo wa kuwekeza. Nimesota miaka yote minne nateketeza nguvu zangu, muda, hela na rasilimali zingine. Kuchimba maji kwa mashine ya drilling ni wastani wa 10m. nimejipinda mtu katulia tuliiii. Leo kumenoga yeye anataka kutia timu, alafu anajifanya mjuaji sana yaani kiherehere chake utadhani ndo shamba lake anavyokuja kunipangia cha kufanya. Bwege sana.

Watanzania tujifunze kujitesa kwa muda flani ili baadaye mambo yakunyookee. Ina gharama yake. Inaumiza sana watu kudanganywa na motivational speakers unasimuliwa jinsi kilimo kinavyolipa, lakini hutaki kujifikirisha pia jinsi kilimo kinavyohitaji sacrifice ya kutosha especially kipindi cha mwanzo. Unaposisimka pale unapoona mtu ana shamba la green house, au hata la nje lakini anamwagilia drip irrigation, anatoa magunia kibao ya vitunguu, nyanya au mazao mengine, unatakiwa ufikirie huyo mtu alifika fikaje hapo? Tusitake tu kuona shamba jeupe, kuna kisima cha maji, pampu na simtank alafu unasema sasa tukalime.

Picha kwanza mkuu!!
kusafisha shamba la heka 3 sio mchezo!! unastahili pongezi budah
 
Kichwa cha habari na habari ni mambo mawili tofauti
Unapopenda kuwa mkulima sio kila mtu atakuwa mkulima, sema ungesema unatueleza umefikia wapi juu ya mkakati wako wakulima na kuwekeza.
MKuu Usifikirie kukomaa sana ndio kufanikiwa
Maisha ni haya haya tu, Ukishindwa kula bata leo usitegemee kesho
Nina Usemi Mmoja tumia hela upate akili ya kutafuta hela nyingine,
Sinaga Upuuzi wa kuweka akiba hata siku moja, Wala siamini katika kuweka akiba,
but always naamini katika investment ila usiwe na akili za kitoto namna hivyo
Nina mashaka na namna unavyoendesha familia yako
 
Mkuu kwanza hongera kwa hatua uliofikia, umewekeza pesa nyingi mpaka hapo. Changamoto halisi za kilimo zinaanza rasmi wakati mkulima anaanza kulima. Unaweza kufanikiwa vizuri shambani lakini soko likakuangusha na kufanya juhudi, muda na mtaji ziwe sawa na kazi bure. Na shambani kunaweza kuharibika au kutoa mavuno yasiyotarajiwa lakini soko likawa baya.

Najua sana hayo unayosema na nina uzoefu halisi ambao nimeuishi na kuushuhudia. Pia nimetumia muda mwingi sana kutafuta maarifa mengi sana kuhusu kilimo na ufugaji, pia nimetembelea mashamba darasa idadi ya kutosha kabisa kama ni lecture nimepata za kutosha, jumlishia na background yangu mimi nimetokea familia ya wakulima japo kama unavyojua wazazi wetu walikuwa wanalima kienyeji sana. Ni muda wa mimi kufanya kitu tofauti. Sina papara ni muhimu kuwa na malengo, na ufurahi unapoona malengo yanatimia. Kuhusu changamoto ya soko na utunzaji shambani, falsafa yangu ni kuwa Mungu alituweka duniani tuitawale dunia... hata kilimo ni muhimu kutumia akili badala ya nguvu nyingi. Wengi wanalima kwa sababu kahamasishwa na flani au kaona mwenzake anafanya hivyo. Badala yake unatakiwa uwe na target yako wewe kama wewe, tumia akili. Mfano, mwaka jana sikulima mahindi hata punje baada ya kutafakari gharama na usumbufu ambao mkulima anapata, huku akitarajia mvua ndo avune. Sitaki kilimo cha kubahatisha nikasema nitanunua mahindi. Wengine wajinga wakanishangaa kuona nasafisha tu shamba natoa visiki alafu msimu wa mahindi sijapanda. Baadaye walikuja kuona nilitumia busara baada ya wao kujikuta wanauza mahindi gunia Tsh. 25000. Ukicheza katara vizuri utaokoka, ukizubaa utaliwa, lakini pia lazima ukubali wakati mwingine mahesabu yanaweza kugoma, lakini hayawezi kugoma kila siku. Go wisely
 
Kichwa cha habari na habari ni mambo mawili tofauti
Unapopenda kuwa mkulima sio kila mtu atakuwa mkulima, sema ungesema unatueleza umefikia wapi juu ya mkakati wako wakulima na kuwekeza.
MKuu Usifikirie kukomaa sana ndio kufanikiwa
Maisha ni haya haya tu, Ukishindwa kula bata leo usitegemee kesho
Nina Usemi Mmoja tumia hela upate akili ya kutafuta hela nyingine,
Sinaga Upuuzi wa kuweka akiba hata siku moja, Wala siamini katika kuweka akiba,
but always naamini katika investment ila usiwe na akili za kitoto namna hivyo
Nina mashaka na namna unavyoendesha familia yako

Siyo kila post lazima uchangie. ishi upendavyo acha wengine tuishi kivingine, ndo raha ya dunia
 
Najua sana hayo unayosema na nina uzoefu halisi ambao nimeuishi na kuushuhudia. Pia nimetumia muda mwingi sana kutafuta maarifa mengi sana kuhusu kilimo na ufugaji, pia nimetembelea mashamba darasa idadi ya kutosha kabisa kama ni lecture nimepata za kutosha, jumlishia na background yangu mimi nimetokea familia ya wakulima japo kama unavyojua wazazi wetu walikuwa wanalima kienyeji sana. Ni muda wa mimi kufanya kitu tofauti. Sina papara ni muhimu kuwa na malengo, na ufurahi unapoona malengo yanatimia. Kuhusu changamoto ya soko na utunzaji shambani, falsafa yangu ni kuwa Mungu alituweka duniani tuitawale dunia... hata kilimo ni muhimu kutumia akili badala ya nguvu nyingi. Wengi wanalima kwa sababu kahamasishwa na flani au kaona mwenzake anafanya hivyo. Badala yake unatakiwa uwe na target yako wewe kama wewe, tumia akili. Mfano, mwaka jana sikulima mahindi hata punje baada ya kutafakari gharama na usumbufu ambao mkulima anapata, huku akitarajia mvua ndo avune. Sitaki kilimo cha kubahatisha nikasema nitanunua mahindi. Wengine wajinga wakanishangaa kuona nasafisha tu shamba natoa visiki alafu msimu wa mahindi sijapanda. Baadaye walikuja kuona nilitumia busara baada ya wao kujikuta wanauza mahindi gunia Tsh. 25000. Ukicheza katara vizuri utaokoka, ukizubaa utaliwa, lakini pia lazima ukubali wakati mwingine mahesabu yanaweza kugoma, lakini hayawezi kugoma kila siku. Go wisely
Safi sana ndugu, umejieleza vizuri na kwa kupitia maelezo hayo nimefahamu yakuwa unafahamu na umetafiti vya kutosha kuhusu kilimo. Nakutakia kilimo chema.
 
Na kweli ni mvivu, uvivu namba moja ni kutaka kubanana kwenye ekari 3, hivi ekari 3 ni eneo kweli la kubanana watu wawili wanaotaka kufanya serious investment? Wakati mashamba yamejaa kibao kila pahala.
 
Mkuu sometimes inabidi kufikiria kwanza namna ya kumjibu, la sivyo ni rahisi kutukana. Ndo maana Mungu akatupa akili, na wanasaikolojia husema ukiwa na hasira usimjibu mtu. Unatulia kwanza alafu unashusha hasira kwanza. Maana yeye alitakiwa ajiongeze kichwani mwake walau hata awe na chembe ya aibu ili kuepusha mengine. Bado nafikiria namna ya kumjibu ila haya majibu ninayoandaa siku nikimjibu hatarudi kunisogelea.

sio kila mtu anaweza KUJIONGEZA
neno HAPANA watu wengi wanaona ugumu sana kulitumia
unapoteza muda kufikiria ambayo tayari umeshafikiria na ukaona HAIFAI hivyo ukijilazimisha kukubali kwa sababu ya urafiki ulionao ni mwanzo mzuri wa KUFELI
Sema HAPANA maana wewe una mipango tofauti ndio maana wakati wewe unaanza yeye hakutaka

sema HAPANA na acha kupeleka mbele maamuzi ambayo unaweza kuyafanya sasa unakaa unafikiria umjibuje mtu wakati jibu ni HAPANA na huna jibu jingine stong kuliko hilo
 
Back
Top Bottom