Vikwazo Vinavyozuia Ukuaji wa Kilimo Tanzania

NIASILAA

New Member
Joined
Jan 6, 2011
Posts
4
Reaction score
0
whats are the "barriers" facing the growth of "tanzanian" farmers
 
  1. elimu duni ya wakulima
  2. mipango duni ya serikali ya kumkomboa mkulima
  3. watanzania bado hawajachukulia kilimo kama ni kazi
  4. uhaba wa miundo mbinu
  5. ruzuku kutoka serikalini hazitoshi
  6. viongozi wa juu/serikalini wanakula pesa zote wenyewe
  7. pesa/misaada haiwafikii walengwa
  8. wakulima wengi wa tanzania wanalima bila mipango
  9. uhaba wa maji
  10. uhaba wa tekinologia ya kilimo
  11. kilimo cha kutegemea mvua ni tatizo kubwa sana kwa tz
  12. hakuna soko la uhakika kwa mazao m.f mkulima analima na anauza ila walanguzi ndio wanaofaidika. kwahiyo hakuna sababu ya kulima acha wote tuwe walanguzi
  13. etc......
 

Soko ni tatizo la kwanza. Kungekuwa na soko la mazao yetu, watu wangetafuta shule zaidi ya kilimo, wangejenga mifereji wenyewe, wangevuna maji ya mvua bila taabu nk.
 
whats are the "barriers" facing the growth of "tanzanian" farmers
teh teh, yaani hii ni topic yako ya kwanza? Nadhani wewe ni dent na hii ni homework yako umepewa 🙂 Naona mzee unadesa mpaka jf....
 
am doing a research on this topics and i would like my fellow tanzanians to comment so as to get solution to increase growth of farming industry!!!


determine the process / barriers which they face that prevent them from being competitive growing
 
Vikwazo vingine ni Ardhi

Tatizo la ardhi ni kubwa sana.

unakuta mashamba yenye rutuba wanagaiwa wawekezaji halafu wazawa wanakuwa vibarua. kwani nini mzawa asitumie nguvu kazi yake kujiajiri katika ardhi yake kama heka 5 au 10?

unakuta viongozi wa serikali wanahodhi ardhi heka 500 au elfu - pengine unakuta mwekezaji anapewa ardhi hekari 5000 mpaka 100000.

Watanzania hatuna haki ya kugawiwa ardhi.
 
oh, i see...
would you mind if i ask you what is your goal and scope of your study? is your study a topdown or bottom up? any system boundary? you know, before starting a reasearch you should have some background information (literature review) and a problem statement/rationale of the proposed study...(i assume that you have)...as you see, what is your expected result?
 
Soko ni tatizo la kwanza. Kungekuwa na soko la mazao yetu, watu wangetafuta shule zaidi ya kilimo, wangejenga mifereji wenyewe, wangevuna maji ya mvua bila taabu nk.
soko bila mindo mbinu (infrastructure) ni sawa na siasa za ccm! utawezaje kuwa na mifereji na kukusanya maji ya mvua wakati mvua zenyewe hakuna? mfano; tunahitaji kuwa na wakulima ambao hawategemei mvua!!!! pia, kama madai yako ni sahihi; tatizo lingine ni utaalamu wa kumwagilia! sijawahi kuona tz wakulima wakitumia 'drip irrigation' bali wengi wao wanatumia 'flooding'....unajua ni maji kiasi gani yanapotea kwa kumwagilia kwa mtindo wa mafuriko?
 
ukulima si lazima uwe na acres 500...mfano mimi nina acres 3 tu na mambo ninayotoa shambani hapo si mchezo! tunahitaji kulima kitaalamu zaidi na sio ubabaishaji tu! mbegu duni unapanda unategemea nini?
 
Soko ni tatizo la kwanza. Kungekuwa na soko la mazao yetu, watu wangetafuta shule zaidi ya kilimo, wangejenga mifereji wenyewe, wangevuna maji ya mvua bila taabu nk.

Malila na kubaliana kwa kiasi na hili lakini si moja kwa moja. Soko la wezaje kuwa tatizo kwa nchi yenye population ya watu zaidi ya 40M? Ni soko au ni strategy za kutengeneza masoko ndo tatizo? Angalia policy za wenzetu za Agriculture zinavyo create internal market na kuongeza internal prices ndipo sasa hasa wanapo pata uwezo wa ku influence world markets. Hivi China walifanyaje kwanza kabla ya kuteka soko la dunia? Walianza na soko lanje kabla ya kujizatiti kwanza ndani? It is the law of nature for internal forces to influence external forces...

Programming yetu katika kilimo bado haiko comprehensive wala siyo strategic. Huwezi kuanzisha uzalishaji bila kumfikiria mlaji ni nani na yuko wapi na anauwezo gani katika kusustain hiyo production.

Mfano watu wanalima mahindi wanafikiria tu wanunuzi wambali wakati jirani hapo kuna ngo'mbe wanakufa kwa kukosa machungio...watu wakikubaliana imformally kwamba nipe shamba lako nilishe ng'ombe zangu technocrats kwakupenda rushwa wanaingilia hizo negotiation na kusababisha conflicts badala ya ku enhace hayo mawazo na kuyaboresha.

For me its more of attitude than markets... Say why mahindi si lazima yawe kwaajili ya kula ugali tu kwa sababu traditionally ndo staple food. Pumba za faa kulisha kuku mabua yana value etc so mkulima yeye ka crame tu akilima mahindi basi auze kwaajili ya kusaga unga tu by products zote zinatupwa wakati hapo zinge mwezesha kuwa inputs katika associated projects..Worse enough mmoja akilima mahindi basi kijiji kizima wanalima mahindi hakuna mlaji na competition inakuwa kubwa huku price ikienda chini.

Je kwa mfano Wangelima watano kijijini wengine wakawa vibarua wengine wakawa na mashine za kukoboa na kusaga wengine wakafuga mbuzi wengine kuku, wenigne wakalima mboga wengine wakafyatua matofali na kuchoma na pumba hapo kuna swala la soko? Inamaana waliolima mahindi watawauzia wengine hapo ili wapate staple food ugali, mwenye ugali atanunua mboga kwa mkulima wa mgoga, wenye mahindi watakuwa wateja wa wenye mashine za kusaga na kukoboa, pumba kwaajili ya kuchoma matofali, kulisha mifugo ambayo itatoa mbolea kwaajili ya mashamba na bio gas kwaajili ya umeme hapo kijijini etc so unatengeneza market hapo hapo kijijini ni surplus tu ndo inauzwa nje tena bei itakuwa ya juu maana soko lipo hapo hapo kijijini. Simple model tu inamaliza tatizo la market at farm gate level alafu utashangaa ooh hakuna soko? Ya kweli hayo?

Constraint kubwa kwa mkulima wa kawaida ni ambayo ipo kidogo nje ya uwezo wake ni weather na siyo soko pamoja na jinsi ya ku program kilimo. Kilimo kuendeshwa na population yote ya kijiji ni pathetic marginal productivity ni zero maana labour input ni kubwa kuliko out put.

Kazi ya kutengeneza hizo quotas ndo ya serikali through sera na strategies...pale ambapo weather inakuwa otherwise subsidies ndo zina ingia hapo pamoja na installation za Biogas facilities sio ooh vocha za mbolea huku wanufaikaji ni walanguzi. Ukiwa coordinate wakulima vizuri hawahitajiwakala wa voucher za mbolea watajua inapopatikana na watanunua wenyewe for it pays to invest in that input, otherwise hawezi risk eti aweke mbolea wakti hana uhakika na hali ya hewa yeye mwenyewe atamsaidia mlanguzi wa voucher kupata pesa za serikali.
 
whats are the "barriers" facing the growth of "tanzanian" farmers
You know plants have varying Kc 'crop coeffiecients values' throughout the growing stages. There are short duration crops (3-4 months) that need about 200-240 mm of water for irrigation (one standing crop) throughout their growing season. Therefore, if you have about 200 crops then you will need about 200 times the amount of water needed by one crop, let say 400-480mm of water for irrigation. Rember, there is evapontranspiration. What I am trying to say is we need expert to od all the feasibility studies as far as the agriculture is concerned.

I once visited rice farmers somewhere in TZ. It was during harvesting. The fields were too dry. I mean they harvested very late while the moisture content was less than lets say 10%. That is to say 'most of the rice fell down' i.e kuck of knowledge on when to harvest. Some farmers stores their cerelas while having very high moisture content let say 25-30%....what do you expect?

The GoT need to help these poor farmers to raise their agricultural skills etc!
 
*this topic is wide! i can end up writing a 2nd thesis! Mungu ibariki Tanzania na watu wake...
 
Mkuu CBZ ni kwamba badala ya Kiongozi kuhodhi au kushikilia heka 500 au mwekezaji, wananchi wangegaiwa angalau hekari 2 mpaka 10 kadri ya uwezo wa kuhudumia.

Kwa hiyo nina maanisha kuliko mtu mmoja kumiliki hekari 500 mwenyewe, wananchi wengi wangegaiwa.
 
Mimi sioni kama ni tatizo kwa mtu mmoja kuwa na acres 500 na kulazimisha kwamba zigawiwe kwa wananchi acres 2-10 kila mtu! Mashamba mbona bado yapo meeeengi tu. Mimi nadhani watanzania wengi ni wavivu na hasa kwa kilimo chetu cha jembe la mkono! Hat kupanda mpunga tu tunatumia mikono! What if you have 200 acres za mpunga?

Mimi nadhani inabidi tubadili mbinu za kiukulima kwanza, mengine yatafuatia tu taratiiiibu 🙂
 
Malila all the points ulizoweka ziko valida hasa swala la soko ,na swala la mechanised farming ,jembe la mkono halitamtoa mkulima ktk umasikini,serikali inabidi itoe kipaumbele ktk kujenga kiwanda cha Tractors,combine harverster etc,kuweka kodi kubwa sana ktk kuimport chakula kodi iwe juu sana ili wafanyabiashara wawekeze ktk kilimo withing TZ.
2-Social image ya kuwa mkulima ibadilike,we need farmers Facelift ili kuwa mkulima iwe kazi ya hadhi yake kama nchi zingine utaona mkulima anasimama with pride kwani yeye anajijua anamchango mkubwa ktk kulisha taifa(food Security)

enzi zile nipo shule mtu akichemka utamuita Mshamba ikimaanisha limbukeni zimbukuku ulimwengu uko huko,na mtu akifanya kitu kizuri,anakuwa kama mzungu,au kitu cha ulaya,sasa unategemea ukimaliza shule,then unagraduate hata kama ni degree ya kilimo ,unadhani utaenda shamba kuwa MSHAMBA. the answer is no.utaenda mjini na kutafuta kazi ya kizungu,white collar job,or worse become a bank teller at barclays,nbc ,crdb etc, na degree yako ya SUA ya kilimo,
serikali na jamii inabidi ifanye kilimo kionekane ni Fani ,kazi nzuri ya maana,na kuanzisha programmes za kusafisha[kuondoa BrainWash] iliyofanywa for the past 50years.
only then kilimo kitapewa kipaumbele,masoko ya mazao yatakuwa mikoani na sio Dar peke yake,Extensio officers watakuwa proud na kazi zao,na MKULIMA (Mshamba) atakuwa proud kusimama hadharani na kujifu kuwa ni mkulima, ikifika mahali kuwa ukiuliza mtoto wa miaka5 what do u want to be when you grow up, anakwambia i want to be a Big Farmer like Mr.Malila :wink2:. and JF Farmers
 
Hakuna sera nzuri za kilimo,hakuna mikakati,nia na dhamira ya kweli ya kuwasaidia wakulima wa Tanzania kutoka kwa serikali......kungekuwa na sera nzuri,hayo masuala ya masoko,miundombinu,pembejeo,elimu,umwagiliaji, kwa wakulima yote yangeshughulikiwa.Sipendi kulaumu serikali ila nafikiri haijatimiza wajibu wake kwa wakulima matokeo yake wanakata tamaa kila siku.
 

Asante dada, ulipotelea wapi? huu mjadala ni mzuri na hautakuwa na jibu moja kwa kila eneo la kilimo. Mazao kama pareto yameanguka kwa sababu ya mabadiliko ya teknolojia, vipi mkonge ulivyoanguka miaka ile.

Nasisitiza kuwa soko likiwa la nguvu linachangia mambo mengi kwenda vizuri,miundo mbinu ni muhimu sana na sera imara zinasaidia.
 

Bado hata flooding irrigation ingefanyika ipasavyo bado tungevuna na kupata ziada zaidi.
 
Kikwazo Kikubwa ni CCM yenyewe wala msitafute kitu kingine. Kinawafanya wafanyabiashara wanunue mazao kwa bei ya chini kwa kuwalazimisha wachangie shughuli zake za siasa, viongozi wake wanakula vocha za pembejeo na ndiyo wateule wa mwenyekiti wa chama chao, unategemea kilimo kikue hapo??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…