Vilabu Vya Mpira Mitaani Vimekwenda Wapi?

Vilabu Vya Mpira Mitaani Vimekwenda Wapi?

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
VILABU VYA MPIRA MITAANI VIMEKWENDA WAPI?
Dar es Salaam tuliyokulia sisi katika 1960s hakuna ambae alikuwa hachezi mpira.

Kutoka Upanga hadi kufika Kidongo Chekundu kulikuwa na viwanja zaidi ya 10.
Tukifanya mazoezi kila siku mwaka mzima.

Jangwani kulikuwa na viwanja hata idadi yake sijui kama kuna mtu anajua.
Yanga na Sunderland (Simba) na Cosmopolitan pamoja na club ndogo za mitaani kama Young Boys, New Port, Young Kenya kwa kutaja chache walikuwa na viwanja vyao Jangwani.

Leo hakuna kiwanja hata kimoja.

Moyo wangu unavuja damu ninapoona watoto wanacheza mpira wa makaratasi barabarani miguu chini.

Kucheza mpira mzuri kulikuwa kunanyanyua heshima yako.
Angalia picha yangu hapo chini tukivaa viatu na ''shin guards.''

Nini kimetokea?

321500571_694592908687013_4609708744052501902_n.jpg
 
Kipindi hicho nilikuwa nakipiga na Arsenal ..nilikuwa nakichafua balaa nikicheza nyuma ya straika..

Sema najiuliza hivi hawa jamaa kwa nini waliamua kujiita Arsenal..si tuingejiita tu mtaa mchafu fc?..
 
Viwanja vya mtaani hususan Dar Es Salaam vimegeuzwa yard na wenye mamlaka.
Watoto na vijana hawana pakwenda kucheza mpira haya ndio matokeo yake ya kufa kwa vilabu vya mitaani
 
Wahindi, Waarabu &Co. wameiharibu Tanzania yetu kabisa, mimi Timu yangu ilikuwa Kagera rangers ilikuwa daraja la 4 lkn tulikuwa nayo pamoja hatukushobokea Yanga, Simba au hata Pan Afrikan
Mambo yalianza kuharibika wacheza cricket walivyoingilia Soka akina Gulamali, hii nchi tumepotea njia leo hii wote wanawaambudu Dewji au sijui Waarabu gani, kila mtu ni Yanga au Simba mtu yuko Mikoani lkn anashabikia Yanga au Simba wakati kwenye Mkoa wake kuna Timu badala ya kuwa mwanachama wa timu ya Mkoa wake anataka kuwa Yanga/Simba.

Hii nchi tulishaipoteza zamani kabisa, …
 
Baba yangu eeh.sasa ni akhir zaman kwisha tena.mim nakumbuka marehem babu alikua anatuhadithia jins inspector wa kiingereza anapita madukan kukagua bidhaa zilizopo na kujua kama zimepitwa na muda.leo hii masuper maekert makubwa yanauza kitu mpaka kime expire wanauza unakuta sale kumbe vimeisha muda.zaman watu walikua hawana watumbo tumbo kama leo na soda zilikuwepo nashangaa sasa hiv wanaweka nini
 
Kipindi hicho nilikuwa nakipiga na Arsenal ..nilikuwa nakichafua balaa nikicheza nyuma ya straika..

Sema najiuliza hivi hawa jamaa kwa nini waliamua kujiita Arsenal..si tuingejiita tu mtaa mchafu fc?..
Dar...
Siku zile ukoloni ukitawala na katika mpira ligi tuliyokuwa tunaifahamu ni ya Uingereza na tukitukuza kila kitu cha Malkia.

Imetuchukua muda kujinasua.
 
SIYO ZAMANI TU HATA SASA VILABU VINGI VIMEKUFA. MFANO HAI, TEGETA TIMU YANGU YA VIA IMEKUFA. LIMEBAKI JINA. AFRICAN TEGETA (TIMU YA KUDURA OMARI, MCHEZAJI WA ZAMANI WA YANGA) IMEKUFA. KUNDUCHI SPORTS, KILL FC, KILOMONI FC, GENEVA FC YA BUNJU. MATIKITI FC TIMU YA ABDALLAH MAJURA. NYUKI FC, KAWE RANGER, VINYAGO FC YA MWENGE, ABAJALO FC, BOMU BOMU FC. READS UNITED TIMU YA MTAANI KWANGU, TEMEKE MWISHO MTAA HIMO NA KITOMONDO. SIFA POLITAN, BEILA FC TIMU YA SHULE KWANGU MTONI KWA MAMA MERE. HIZO TIMU ZOTE KIUHALISIA ZIMEKUFA. YAMEBAKI MAJINA TU
 
Back
Top Bottom