Vinywaji hivi ni vya majambazi/wezi.

Redbull ndani yake ina kaffeina, kaffeina inapatikana pia katika chai ya rangi, kahawa na soda zote zenye rangi nyeusi. Kaffeina ni madawa ya kulevya kundi la stimulant drugs, hivyo redbull nayo si salama hasa kwa watoto wanaosoma.

Fadhili Paulo katika hali ya kawaida tunaposema kilevi tunamaanisha alcohol sasa we sijui umeyatoa wapi hayo ya caffeine
 
Last edited by a moderator:
mie huwa najinywea tu hata sijui kama ni vya majambaz au lah
 
Mkuu ni kweli kabisa lakini najua wengi watapinga .
Tatizo lako hukusikiliza mazungumzo mpaka mwisho mbona ungepata jibu kamili.
Kwa wale vijana wa mjini washaelewa vinywaji hivyo hutumiwa na majambazi au wezi wa aina gani??.

Kama ni mtu wa kuluka majoka hakika lazima utakuwa umekutana na hawa wezi.
Hapa jamaa walikuwa wanawazungumzia wanawake wale matapeli wa mapenzi.
Usidhubutu kukutana nao wanajifanya ni mahodari kweli wa vinywaji hivi na ukiwacheki hata hawafananii kwao ni maji mrembuo/kandoro na azam cola na vileo vyao ni banana.
Ila isiombe uingue anga zao.
 
By MamaBeata

redis ndio kinywaji gani? Kama ulimaanisha redds basi hiyo redds kwa taarifa ina kilevi. Kama redbull sawa hiyo haina kilevi.

Redbull ndani yake ina kaffeina, kaffeina inapatikana pia katika chai ya rangi, kahawa na soda zote zenye rangi nyeusi. Kaffeina ni madawa ya kulevya kundi la stimulant drugs, hivyo redbull nayo si salama hasa kwa watoto wanaosoma.

Redbull kama jina lake lilivyo ni pombe hatari sana. Origin yake ilikuwa ni Jeshini wakati wa Vita ilikuweza kuwaliwaza wanajeshi. Ni pombe hatari sana na imepigwa marufuku baadhi ya nchi.
 
Redbull kama jina lake lilivyo ni pombe hatari sana. Origin yake ilikuwa ni Jeshini wakati wa Vita ilikuweza kuwaliwaza wanajeshi. Ni pombe hatari sana na imepigwa marufuku baadhi ya nchi.

Sasa kama ni hivo mbona huku kwetu zinaruhusiwa.
 

Ongeza Grand Malt, Vita Malt Plus eksetra!!!!!!!
 
Sijawahi kumsikia Kova akitangaza kuwa majambazi yalikutwa na silaha aina ya redbull na bavaria.

Nakuunga mguu Mkuu, hata bia wala soda sijawahi sikia. Huwa nasikia Kova akitaja Gongo na Bangi pekee. Kwa hiyo Gongo na Bange ndiyo starehei ya majambazi!
 
Nakuunga mguu Mkuu, hata bia wala soda sijawahi sikia. Huwa nasikia Kova akitaja Gongo na Bangi pekee. Kwa hiyo Gongo na Bange ndiyo starehei ya majambazi!

Kwanza umenikumbisha ngoja nikavute bange
 
Kwanza umenikumbisha ngoja nikavute bange

Baada ya kuvuta bangi, je umepata jibu sahihi juu ya mada?
Inawezekana kabisa hao jamaa walikuwa wanaongelea wezi wa mapenzi, wengi wao wakiwa wasichana na wamama waliokubuhu.
Hakuna uhusiano wa maoja kwa moja, tena usiotiliwa mashaka, baina ya aina ya kinywaji na wizi. Ninachoamino ni kwamba kuna uhusiano wa kutumia madawa ya kulevya na wizi.
 
Redbull kama jina lake lilivyo ni pombe hatari sana. Origin yake ilikuwa ni Jeshini wakati wa Vita ilikuweza kuwaliwaza wanajeshi. Ni pombe hatari sana na imepigwa marufuku baadhi ya nchi.

Mkuu ni kweli hiki kinywaji kimepigwa marufuku baadhi ya nchi za Ilaya na nchi zingine kuna tahadhar ya hali ya juu kuhusu matumizi ya hiki kinywaji, Na kuna aina ya makundi ya watu hawatakiwi kutumia Redbull
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…