Vinywaji na vyakula vinavyochangia kuporomoka kwa kinga ya mwili:

Vinywaji na vyakula vinavyochangia kuporomoka kwa kinga ya mwili:

mleta mada usichanganye mambo. JIPANGE UPYA[/QUOTE]

'....huyu hajui ULABU unaongeza damu kwa afya,tuache'
 
Gomba hatari,maziwa hatari,nyama nyekundu(Red meat)hatari,kitimoto hatari,kuku wa kisasa hatari,chinese hatari,Dr manyaunyau naye kasema maharage ya soya yanalaza---Asante kwa kulikashfu jina langu,mimi ni Phone Dr,nilijikuta tu naitwa hivyo baada ya kuwatengenezea (kimagumashi)watu simu zao za tochi.---Hutaki sasa?
 
Mkuu,
Kwahiyo ukamdharau dr. Ndodi?, unadhani aliamka tu siku 1 akawa tayari anaitwa dr. Ndodi? kama ulivyoamka wewe siku 1 tu ukajiunga jf ukajiita imani ernest badala ya Imani Ernest?.

Ni kweli kama ulivyosema dr. Ndodi amesema kunywa maji ukiwa umesimama ni hatari. Ni hivi: "Kamwe usinywe zaidi ya aunsi 33.8 (lita moja) za maji kwa wakati mmoja ukiwa umekaa au umesimama".

Soma maelezo mengine HAPA
Kwa hiyo umekubali hoja ya Copy&paste aliyoitoa msela hapo juu?
 
Nani awaache? kwani nani amekuambia USINYWE POMBE?. SOMA VIZURI KATIKATI YA MAANDISHI. WE KAMA UNAONA INAKUONGEZEA DAMU, BASI ELEZEA NI KWA NAMNA NA MECHANISM IPI, siyo unaamka tu toka huko ulikofumaniwa.



@Nduki "'....huyu hajui ULABU unaongeza damu kwa afya,tuache'"
 
Wewe siyo "Phone Dr", wewe ni imani ernest,full stop. Nani amekuambia kitimoto ni hatari? simulia kidogo kuhusu kitimoto na red meat.

Gomba hatari,maziwa hatari,nyama nyekundu(Red meat)hatari,kitimoto hatari,kuku wa kisasa hatari,chinese hatari,Dr manyaunyau naye kasema maharage ya soya yanalaza---Asante kwa kulikashfu jina langu,mimi ni Phone Dr,nilijikuta tu naitwa hivyo baada ya kuwatengenezea (kimagumashi)watu simu zao za tochi.---Hutaki sasa?
 
Inahusiana na nini hapa?. Mkuu HAKUNA PUMBA PROJECT (HPP) hapa. Lete hoja kama ulivyozianzisha usikimbilie kwa masela, njoo mwenyewe kama ulivyokuja. Huyo msela wako si unaona amesizi?. Njoo mwenyewe uso kwa uso na wala usilete mizinguo hapa.

Kwa hiyo umekubali hoja ya Copy&paste aliyoitoa msela hapo juu?
 
Wewe siyo "Phone Dr", wewe ni imani ernest,full stop. Nani amekuambia kitimoto ni hatari? simulia kidogo kuhusu kitimoto na red meat.

Umejuaje kuwa mimi ndiye Imani Ernest?au na wewe ni Dr wa hoja mbadala? Mi nimekwambia naitwa -----sijakwambia najiita,hao ma doctor unao wa entertain wengi ni kama wapiga ramli tu,wanaunda hoja kwenye vichwa vyao wanamwagia mdomoni nyingine zinasambaa humu kwenye mitandao,Vipi mkuu ile tiba ya ndodi ya malimao 120 kama dozi ya malaria umewahi kuitumia? Naomba uzoefu wako,Kamishna Manumba malaria inataka kumtoa roho unaweza kusaidia!!naaaaa ndodi alisema ulaji wa chakula cha usiku huchangia kuota ndoto za majinamizi,imekaaje hii?vipi ule mwendo aliokuwa anatufundisha kutembea baada ya kula,umeshawahi kujaribu?bwahahahahahaha,poor mind is the home of all fallacies ptuuu.
 
Nasikia hata "chakula cha usiku" kina shusha kinga za mwili..teh teh teh kaazi kweli kweli........

inategemea unakuala nini na saa ngapi, ideal ni ule not later than saa 1 usiku chakula heavy baada ya hapo ni snacks ndo afya hiyo
 
Watachaguaje vyakula wakati hawana MACHAGUO?. Ili uchaguwe kitu inahitajika kuwe na vitu vingine vingi kama hivyo. Mtanzania atachaguaje kula dona wakati maduka yote yanauza sembe tu?. Isitoshe watz wengi tunakula mlo mmoja tu kwa siku kwa sababu sisi ni maskini.

Tunachotaka hapa ni kwamba HATA KAMA NITAKULA MARA 1, BASI NIWE NIMEKULA AFYA NA SIYO TAKATAKA.

watanzania hawana shida na kuchagua chakula...
 
1. Umejuaje kuwa mimi ndiye Imani Ernest?
JIBU: Kwani we ni nani mkuu?, naomba basi tafadhari nitajie jina lako.

2. na wewe ni Dr wa hoja mbadala?
JIBU: Hakuna hoja mbadala hapa. Kwanini unadhani ni hoja mbadala?, kwanza ni hoja gani hiyo unayosema ni mbadala?.

3. Mi nimekwambia naitwa -----
JIBU: Unaitwa imani ernest

4. hao ma doctor unao wa entertain wengi ni kama wapiga ramli tu
JIBU: Hakuna doctor hata mmoja ninayemu-entertain hapa. Nitajie majina yao hao wapiga ramli tafadhari.

5. wanaunda hoja kwenye vichwa vyao wanamwagia mdomoni nyingine zinasambaa humu kwenye mitandao,Vipi mkuu ile tiba ya ndodi ya malimao 120 kama dozi ya malaria umewahi kuitumia? Naomba uzoefu wako.
JIBU: Ulishawahi kuwaona? unaifahamu mitandao wewe?. kwanini unaweweseka na ndodi?, wewe weweseka na malimao na siyo na ndodi, ndodi ni nani kwani? usiweweseke na ndodi, we weweseka na hayo malimao. Uzoefu jitafutie mwenyewe usisubiri uzoefu wangu tafadhari.

6. Kamishna Manumba malaria inataka kumtoa roho unaweza kusaidia!!
JIBU: Manumba yeye ni mlinzi, huwa anakaa macho usiku nje huku wewe umelala, kwahiyo anang'atwa na mbu zaidi kuliko wewe ndiyo maana lazima auguwe malaria. Wewe umemuona Manumba tu ndiye anayeuguwa malaria hapa tz na ndiye anayehitaji msaada wangu?.

7. naaaaa ndodi alisema ulaji wa chakula cha usiku huchangia kuota ndoto za majinamizi,imekaaje hii?
JIBU: Ni kweli kama unakula kila siku nafikiri alimaanisha hivi sema we hukumwelewa maana we nimegunduwa unachelewa sana kuelewa.

8. vipi ule mwendo aliokuwa anatufundisha kutembea baada ya kula,umeshawahi kujaribu?
JIBU: Sijawahi. wewe ulishawahi?.

9. bwahahahahahaha,poor mind is the home of all fallacies ptuuu.
JIBU: TRUE. LIKE YOURS.


Umejuaje kuwa mimi ndiye Imani Ernest?au na wewe ni Dr wa hoja mbadala? Mi nimekwambia naitwa -----sijakwambia najiita,hao ma doctor unao wa entertain wengi ni kama wapiga ramli tu,wanaunda hoja kwenye vichwa vyao wanamwagia mdomoni nyingine zinasambaa humu kwenye mitandao,Vipi mkuu ile tiba ya ndodi ya malimao 120 kama dozi ya malaria umewahi kuitumia? Naomba uzoefu wako,Kamishna Manumba malaria inataka kumtoa roho unaweza kusaidia!!naaaaa ndodi alisema ulaji wa chakula cha usiku huchangia kuota ndoto za majinamizi,imekaaje hii?vipi ule mwendo aliokuwa anatufundisha kutembea baada ya kula,umeshawahi kujaribu?bwahahahahahaha,poor mind is the home of all fallacies ptuuu.
 
Namba 7 lete ufafanuzi, sababu ugali unakwenda na mboga mboga.

i can try 2 ma best level about this
Sembe kinachoifanya isiwe nzuri ni kwamba..kwenye muhindi vitu vyenye virutubisho ni ganda na kiin basi, but sembe imekobolewa na ukikoboa mahindi unaondoa vitu hvyo yaan, kiin na ganda, unabaki na makapi...so yale makapi unapoyala yanaweza kukuletea hata ugonjwa wa kusahausahau
 
Inahusiana na nini hapa?. Mkuu HAKUNA PUMBA PROJECT (HPP) hapa. Lete hoja kama ulivyozianzisha usikimbilie kwa masela, njoo mwenyewe kama ulivyokuja. Huyo msela wako si unaona amesizi?. Njoo mwenyewe uso kwa uso na wala usilete mizinguo hapa.

Ernest unachanganya, xo we uko upande gan? Coz kila sehem upo, so kumbe hata ile haina uthibitisho wowote coz ww n phone dr. Na sio dr. Kama nliyemfikiria mm, sio?
 
Dah! Kama (Ugali) Sembe umeingia kwenye hii orodha, basi naomba tutaje vyakula vinanavyojenga hiyo kinga badala ya vinavyopunguza.
 
VINYWAJI NA VYAKULA VINAVYOCHANGIA KUPOROMOKA AU KUSHUKA KWA KINGA YA MWILI:


1: CHAI NA KAHAWA:
Pengine hili linaweza kuwashtuwa watu wengine kwakuwa chai ni kinywaji ambacho kimezoeleka katika familia nyingi kama kinywaji cha kawaida na wengi wetu hatujuwi kama kinaweza kuwa na madhara katika miili yetu.


Kama nilivyosema katika post namba 14, angalizo hili la kuacha kunywa chai ya rangi na kahawa ni mhimu kwa mtu ambaye tayari kinga yake imeanza kuleta matatizo kwahiyo ili kujiokoa itakulazimu kuachana na aina hii ya chai na kahawa kwa ujumla.


Kuna nini kibaya kwenye CHAI na KAHAWA?:
Kwenye chai na kahawa kuna kitu kinaitwa CAFFEINA/KAFEINA. Kafeina ni nini?:
1. Kafeina ni madawa ya kulevya kundi la stimulants drugs. Utashangaa. Habari ndiyo hii, watu wengi wanatumia madawa ya kulevya kila siku pasipo wao kufahamu. Hii ndiyo sababu kwa mtu aliyezoea kunywa chai hii kila siku au kahawa, siku asipokunywa kichwa humuuma, ni kwa sababu amekuwa mtegemezi au teja wa kafeina. Kafeina ni kiungo mhimu karibu katika soda zote zenye rangi nyeusi; cocacola, pepsi, sayona nyeusi, azam cola n.k, kafeina huongezwa pia katika red bull na malta. Kaffeina huongezwa pia katika baadhi ya dawa za kupunguza maumivu mwilini. Kwahiyo Kafeina ambayo hupatikana katika chai na kahawa ni aina mojawapo ya madawa ya kulevya.


2. Kafeina ni kikojoshi (diuretics). Kafeina ni dawa ya kukufanya ukojowe. Ukinywa kikombe kimoja cha kinywaji chenye kafeina yaani chai au kahawa, basi muda si mrefu utaenda kukojoa vikombe viwili. Kwa sababu kafeina ni sumu isiyotakiwa mwilini, mwili utafanya kila uwezalo ikibidi ujikamuwe wenyewe kupata maji ya ziada kuweza kuitoa sumu/kafeina hii uliyoinywa kwa kisingizio cha chai/kahawa au soda. Madhara yake ni nini?, moja kama unakunywa kinywaji na muda si mrefu unalazimika kwenda kukitoa inamaanisha kinywaji hicho hakikutumika vema na mwili, pili kumbuka ulikunywa kikombe 1 na umeenda kutoa 2 hivyo umekopwa maji mwilini mwako na ukumbuke kuwa MAJI NI UHAI.


3. Kafeina husababisha KANSA. Seli ndani ya mwili lazima zibaki katika kiasi kidogo cha alkalini kutoka 7.2 mpaka 7.4, wakati 7.0 ni ya kati au husemwa sifuri katika kipimo cha PH (potential hydrogen). Chini ya 7.0 ni asidi na juu ya 7.0 ni alkalini. Kafeina yenyewe ni asidi, hivyo ikiwa mtu anafanya chai au kahawa ndivyo vinywaji vyake vya kila siku basi mtu huyo lazima atakuja kupatwa na kansa katika siku za usoni kwakuwa seli za kansa huishi katika hali ya uasidi pekee na kafeina ndimo mazingira mazuri ya kuishi asidi.


Jarida moja la afya la Uingereza, ‘The British Medical Journal Lancet', limeripoti uhusiano mkubwa uliopo baina ya utumiaji wa kahawa na kansa ya kibofu cha mkojo na kupungua kwa uzarishwaji wa mkojo.




4. Kaffeina huchangia upotevu wa madini na vitamin mhimu mwilini. Kafeina ambayo ni kikojoshi, huyalazimisha maji kukimbia nje ya mwili kwa haraka na kuziacha seli bila muda wa kutosha kuyatumia maji hayo, maji yanapokimbia kwa haraka nje ya mwili huyakimbiza pia madini mhimu nje ya miili yetu.


5. Kaffeina husababisha kisukari. Mwili una vyanzo 3 vya nguvu ambavyo ni Sukari, Mafuta, na Maji/Chumvi. Tumesema kaffeina ni kikojoshi, hivyo kaffeina hupelekea upotevu usio wa lazima wa maji mwilini, mwili unapokosa maji kama chanzo chake cha nguvu, moja kwa moja huhamia kuitegemea sukari kama chanzo chake cha nguvu na mwishowe kisukari lazima kitokee.


6. Uchovu sugu. Mateja wa chai ya rangi na kahawa mara nyingi wanapojisikia uchovu hukimbilia kikombe cha kahawa au chai. Kaffeina iliyomo katika chai au kahawa huenda kuiamsha na kuitumia nguvu iliyokuwa imehifadhiwa na mwili kwa ajili ya matendo ya dharura na kukuacha wewe ukiwa huna nguvu ya ziada kwa ajili ya kazi za dharura, matokeo yake ni mwili unakuwa upo katika hali ya msukosuko muda wote.

Utolewaji wa sukari iliyokuwa imehifadhiwa, kunapelekea mfadhaiko mkubwa kwenye mfumo wa dharura wa mwili. Unaposhitushwa kidogo tu, unakuwa na nguvu za haraka (Unahamaki) kushughurika na tatizo. Hali hii hatimaye inawezapelekea kukauka kwa tezi ya adreno kutakakosababisha damu chache yenye sukari (hypoglycemia), udhaifu, na kuumwa sana iwapo sukari haitachukuliwa mapema kupandisha juu damu sukari.


Kwa sababu ya biashara kuunda vyakula vyetu vyote maalumu na vinywaji vyenye radha mpya, radha nzuri na nguvu ya kutosha kwa kutumia kafeina toka katika mimea na mitishamba kama vile ginseng kuisisimua tezi ya adreno, kunasababisha Ini kutoa sukari iliyokuwa imehifadhiwa mwilini kwa ajili ya matumizi ya dharura ya mwili.


Hakuna nguvu iliyomo kwenye kafeina au ginseng. Kuna majina mengine mengi ya visisimuwaji hivi kama vile, kokwa za guru, kokwa za cola na mfalme wa yote ni guarana. Mbegu za guarana zina kiasi cha kafeina mara tatu zaidi ya zile za kahawa, na hawatakiwi kuliorodhesha neno kafeina kwenye vifungashio (packages) au kontena.


Ungaunga wa guarana hutumika kutengenezea vidonge vya kupunguza uzito kwa sababu kafeina itazisambaratisha hisia za njaa, lakini hakuna mahala neno kafeina linaonekana kwenye vifungashio vya dawa hizi.


Kuna mimea, kokwa na kemikali nyingi ambazo zitaisisimua tezi ya adreno na kusababisha ini kuitoa sukari iliyokuwa imehifadhiwa au hata kuitengeneza toka tishu za mwili wenyewe '(gluconeogenesis)'.


Imethibitika pia kuwa kafeina imekuwa ikiingilia na kuathiri unakilishaji wa kinasaba (DNA), namna ambavyo seli mpya hutengenezwa. Kafeina inaweza kusababisha upotevu toka mwilini wa vitamini nyingi za kundi B, kundi C, zinki, potasiamu na madini mengine. Kahawa huongeza hali ya uasidi kwenye utumbo mdogo.


Kafeina inaweza kusababisha msukosuko ndani ya mwili.


Kafeina siyo kwamba tu huimaliza nguvu iliyokuwa imehifadhiwa kwenye ubongo, bali pia huzuia mfumo vimeng'enya katika kutengeneza kumbukumbu kwenye ubongo.


Kituo cha sayansi kwa masirahi ya umma (Center for science in public interest) kimewashauri kinamama wajawazito kukaa mbali na kafeina kwa kuwa tafiti zimeonesha kwamba kiasi cha kafeina kilichomo kwenye vikombe 4 vya kahawa kwa siku kinaweza kusababisha matatizo wakati wa kujifungua kama yalivyoonwa katika majaribio kwa wanyama.


‘Madawa na wewe', kwa mjibu wa Dr. Earl Mindell, mwandishi wa kitabu; ‘Earl Mindell's New Vitamin Bible' (zaidi ya nakala milioni 10), anasema katika ukurasa wa 414 wa kitabu hicho kuwa ‘kafeina ni dawa yenye nguvu kubwa, uwezekano ni kuwa, hauifurahii tu kahawa au cola yako ya kila siku, bali umekuwa mtegemezi/teja (addicted) kwavyo'.

HITIMISHO:
Madhara ya chai ya rangi na kahawa mwilini ni mengi sana na tatizo moja litapelekea lingine na orodha inakuwa haiishi.


Tumezoea kunywa chai kila siku tutafanyaje sasa?. Kama nilivyosema kuwa hili ni mhimu kwa mtu ambaye kinga yake ya mwili imeshashuka na anahitaji kuipandisha na kuirudisha mahala pake ama kwa mtu ambaye tu yeye kuuguwauguwa ni kitu asichokipenda maishani mwake.

Kwahiyo badala ya kutumia majani hayo ya chai meusi, wewe chemsha maji yako ya chai kama kawaida na unaweza kutumia vifuatavyo kukamilisha chai yako; unaweza kutumia tangawizi na kumbuka pia tangawizi ni dawa ya magonjwa zaidi ya 72 kwahiyo unapoinywa chai ya tangawizi siyo tu unaepuka madhara ya kaffeina tu, bali pia unakuwa umekunywa dawa ya zaidi ya magonjwa 72 mwilini, unaweza pia kuweka mdalasini, unaweza pia kutumia mchaichai, unaweza pia kukamulia ndimu, pia unaweza kutumia mchanganyiko wa viungo vingi vya chai (spiced tea) ambavyo vinapatikana kwa wingi katika soko la kariakoo dsm na Zanzibar.


Kama kinga ya mwili imeanza kuleta shida, unashauriwa kukaa mbali na vinywaji nilivyovijadili katika makala hii ya chai na kahawa.

maajabu ya maji
 
Back
Top Bottom