Vioja vya majibu ya barua ya posa 'UZARAMONI'

Gazeti ukisikia mkaja kwa pwani ni kama vile 'mkanda' au belt.

Mkaja wa mama ni pale baada ya kujifungua hujifunga tumbo kwa kanga au kitenge ili lisilegee. Hiyo ni mila sijui kama inasaidia au la lakini ile kanga/kitenge hukunjwa vizuri kama belti na mzazi hujifunga tumbo lake.

Mkaja wa baba sina hakika sana lakini zamani vile vile baba walikuwa wanajifunga kitu kama belti kuzuia kikoi (munaita msuli). Kwenye hilo belti kuna sehemu ya kuwekea coins ambazo zamani ndiyo zilikuwa fedha nyingi sana.

Sasa hivo unalipishwa kama ni shukurani kwa wazee kumlea mtoto wao vizuri.

Hivyo vya babu na bibi nadhani sasa ndiyo vimebadilishwa kidogo.
 
Asa hyo mahari mbona ni sawa na umepewa mke kama sadaka tu mkuu..,kinachokulalamisha hasa ni nin kwan?ebu nenda uchagan uone ka utaweza kuoa!
Hizo gharama ni nje ya mahari, hata hivyo bado mahari haikuwa kubwa
nimevutiwa na kuingiwa na udadisi na gharama za ziada kwani kwangu
ilikuwa kama burudani fulani ya aina yake.
 
Dah, nimekuelewa vizuri. Ahsante sana!
 
itakuwa kiwembe cha kunyolea ndevu babaake hicho..... just guessing
 
mi nikijakuoa nkatajiwa mahari kubwa basi ntamtia mimba binti wao kwanza alafu ntarudi kwa mara ya 2 kuomba nipunguziwe.
 
 
Majibu yote yamenikosha roho, wazaramo wakwe zangu.
 
Wazaramo ni progressive kwa msingi huu. Mahari ni "token" of appreciation, sio kama bei ya kununua mtumwa.
Nakubaliana nawe kabisa mkuu. Nimewahi kuona wana vitu vidogo vidogo vingi lakini vyote ni 'symbolic'. Halafu ni wakarimu sana kwa wakwe zao.
Nadhani inatakiwa iwe hivyo tofauti na kule Isenye(Musoma) tulipokwenda kumsindikiza mtarajiwa tukiwa na ka-double cabin,tuliposomewa mahari tulitamani tuwakabidhi hako ka gari ili yaishe! Tulirudi tukiwa tumetawanyika.




...........
.




...
 
koma kabisa, weee! shika adabu yako eboooooooo!
Usibishe mkuu kuna mtu kule kaoa kwa NOKIA ya Mchina
kama huamini nenda Mbagala Magengeni uliza kwa mzee
Athumani Lukundu, huyo jamaa anaitwa Jabiri Chikandanga.
 
nimecheka leo jaman ....makabila yanamambo
 
Kuoa Uzaramoni mbona safi sana, wenyewe wanataka mdundo mkali wa muziki, hata ukiwapa maandazi mawilimawili hawana noma

weeeeeeeeeeee ubwabwa lazima umlishe nani maandazi siku ya shughuri!!!mdundo mkali wa mziki ndio mpango mzima
 
Mie nimependa kisamvula ndevu. Hata mie mwanangu akiposwa nitaomba kisamvula ndevu hata kama si Mzaramo. Mambo ya utandawazi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…