Viongozi hawa kukaa kimya kuhusu suala la Bandari inaashiria nini?

Hennes kolon

JF-Expert Member
Joined
Jan 13, 2023
Posts
673
Reaction score
1,294
Wana bodi,

Kwa ukimya wa Askofu Gwajima kiasi hiki juu ya sakata la DP WORLD! amekuwa kimya Sana na mtulivu utadhani hayupo Tanganyika!

kabudi pia kawa kimya sana, utadhani hayupo Tanganyika.

yule mbunge wa iringa pia yuko kimya sana yaani nikama haishi Tanganyika kabisa. hatusikii maoni yao, inamaana wameamua kukaa na hekima zao vifuani mwao!?
 
Unaweza kuta kwa waumini wake anawaambia wapinge lakini akiingia mjengoni anaunga mkono hoja
 
Mbunge wa Isimani ameshasimama kuhesabiwa. Anaunga mkono mkataba
 
Ninashauri waendelee kukaa kimya maana ndio salama ya nafsi zao kwa kuwa wakithubutu kupanua kinywa haswa kama maoni yao yataenda kinyume na mwelekeo wa serikali ni watakutana na midomo miwili ya mamba 1) serikali itawakodolea macho 2) wananchi hawatawaelewa na wataghabika kupita maelezo. otherwise they may be fixed
 
Maslahi Binafsi, watahatarisha kazi zao... simple!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…