Viongozi imara vs Taasisi imara

Viongozi imara vs Taasisi imara

Shayu

Platinum Member
Joined
May 24, 2011
Posts
608
Reaction score
1,655
Napenda kuomba radhi mwanzoni kitu nilichokuwa nimedhamiria hakikuweza kuwafikia kama nilivyotaka badala yake yalitokea maandishi mafupi tu, yasiyo na tafakuri yeyote. Hata hivyo hii hapa chini ndio tafakuri yangu na linki ya audio kutoka Youtube ipo hapo.

Kumekuwepo na mjadala mpana sana kuhusu ni nini Afrika wanahitaji kati ya viongozi imara na taasisi imara. Mjadala huu umekuja haswa mara tu ya aliyekuwa raisi wa marekani kuongea yakuwa:: Kwamba afrika haihitaji strong leaders bali strong institutions ili iendelee. Kwa siku za hivi karibuni mjadala huu umechagizwa zaidi na aliyekuwa Mkaguzi muu wa serikali ya jamhuri ya muungano wa Tanzania kusema neno kama hilo akimnukuu tajiri mmoja wa kimarekani aitwaye Buffet.

Napenda kutofautiana kidogo na watu wanaosema afrika haihitaji strong leaders bali strong institution. Vitu hivi viwili vinahusiano wa karibu sana. Huwezi kuwa na taasisi imara kama huna viongozi imara. Tunamahitaji makubwa mno ya viongozi imara. Na sio viongozi imara pekee, bali viongozi wenye maono, hekima na busara kuweza kujenga na kusimamia taasisi hizi. Tunapozungumza viongozi imara hatuzungumzii viongozi wabinafsi, madikteta na wanao kandamiza na kuonea watu. Bali viongozi ambao wako pale kwaajili ya kuhudumia watu na sio tyrants. Kwakuwa tyrants wakishika nchi wanatenda kwaaajili ya manufaa yao na sio kwa manufaa ya taifa. Kwahiyo ninapozungumzia strong leader sizungumzii tyrant bali yule ambaye yuko kwa maslahi ya wananchi na ambaye anayalinda na kuyatetea kwa nguvu zake zote.

Na wale tusujidanganye taifa likiwa na viongozi weak na wasio na maarifa na busara ya kutosha nchi na taasisi zitakuwa hivyo hivyo. Kwahiyo tunahitaji kiongozi ambaye ata elevate na kuwaempower watu na kuwa raise their consciousness kwa utaifa na uwajibikaji. Kwahiyo kiongozi imara hatotaka watu wake wawe dhaifu, atataka wawe kama yeye alivyo ili wa serve nchi yao vyema.

Na wala sizungumzii kiongozi ambaye anataka kuonekana yeye tu, bal ikiongozi ambaye atajenga mfumo imara na kujenga pia watu wake kuwa bora ili waendeshe taasisi hizo pia ziwe bora na ziishi kwa muda mrefu. Kwakuwa taasisi nazo zinakufaga na zinategemea ubora wa watu walionao ili zi serve watu vyema, Na watu wanapokuwa corrupt na taasisi pia zinakuwa corrupt. Taasisi zinategemea watu moja kwa moja. Ubora wa watu ndio ubora wa taasisi. Kwahiyo kiongozi imara lazima awekeze kwa watu na anafahamu huwezi kubadilisha nchi pasipo kuwekeza kwa watu na kuwafanya watu kuwa bora. Kwahiyo anajua nguvu yake na ya taifa lake inategemea ubora wa watu wake. Ni tyrant pekee anataka watu wake wawe weak na yeye awe Strong ili aendelee kuwanyonya. Na tryant sio lazima awe mtu kinaweza kuwa chama. Lakini a strong leader Nguvu yake iko kwa wananchi na mipaka ya nguvu yake haishii kwenye nchi yake pekee husambaa kwasababu nguvu yake hategemei jeshi lake pekee bali pia umma.

Tabia za wananchi katika nchi husika huonyesha dira ya taifa hilo ikoje. Na hiki ndicho kiongozi imara anatakiwa ajenge na taasisi za nchi hutegemea sana kuhusu hilo. Miongoni mwa tabia hizo bora ni nidhamu na kupenda kufanya kazi. Kunapopungikiwa na nidhamu katika nchi maendeleo huwa shida na kunakuwepo hakuna kusikilizana na hata uongozi unakuwa shida na hivyo taifa hukosa dira. KIla mtu atakuwa mkuu, kila mtu mjuzi, watu wataongea bila kufikiri na wala kujali impact ya maneno yao na order katika nchi huwa ndogo.

Barack obama anasahau kwamba waliojenga Marekani hawakuwa watu dhaifu naongelea their founding fathers. Walikuwa ni watu wenye busara na nguvu. Vitu viwili muhimu kwa kiongozi. Kwasababu nguvu lazima iwe regulate by wisdom ile iwe efficiency. Tujue kwamba taasisi haziwezi kujiendesha zenyewe lazima ziendeshwe na watu na inategemea sana watu hao wana maarifa na busara kiasi gani ili taasisi hizo ziendelee kudumu and if they are fool hata watengeneze sheria nzuri kiasi gani na taratibu haziwezi kuwasaidia. Kwahiyo kama tuna problem katika Afrika problem ni sisi wenyewe let us eveluate ourselves. Ni ujinga kusema tunahitaji taasisi imara kama vile zitajiendesha zenyewe na sisi tutasimama kufikiri huku taasisi zikifikiri kwa niaba yetu. Taasisi zinatutegemea sisi kuziendesha zitakuwa bota kama sisi ni bora. Zinahitaji busara na hekima zetu ili ziendelee. Sisi ndio wenye matatizo na cha ajabu hatutaki kujichunguza sisi watu tukibadilika tutabadilisha kila kitu.


 
Last edited:
Kwa uzi huu, Mkuu, unatafuta sababu za kuchomolewa kwenye jukwaa hili. Jukwaa hili ni maalumu kwa hoja zenye kuleta hamasa ya tafakuri tunduizi. Vinginevyo utuahidi kuwa muda fulani utatoa maoni yako juu ya mjadala wenye kichwa cha habari cha uzi huu jambo ambalo halionekani kwenye 'post' ya kwanza ya uzi huu.
 
Shayu

Kuna misconception kati ya strong institutions na strong leaders
Ni muhimu kuangalia historia ya dunia kabla ya kuchukua upande au mtazamo

Kiongozi strong ni nani? Ni Josip Broz Tito wa Yugoslavia au Nelson Mandela wa Afrika kusini?

Tito aliweza kuziweka nchi ''nne'' kama nchi moja kwa mkono wa chuma kwa miaka zaidi ya 40
Baada ya kuondoka, Yugoslavia ikapaganyika kwa damu kila upande ukijitoa
Uwepo wa Yugoslavia ulitegemea 'strong leader' kama Josip Tito. Je, alikuwa strong, jibu ni yes.
Kwanini nchi iliparaganyika baada yake, jibu ni kuwa Tito kama mtu alikuwa ''strong institutions'' bila uwepo wa institutions

Mandela: Akiwa gerezani alikataa 'kutolewa' kwa masharti akiamini kufia gerezani kwa alichoamini ini sahihi. Alipoachiwa akakataa uenyekiti wa ANC kwa kutambua mchango na uwepo wa Tambo na ANC. Aliwakatalia Umkhonto Weswize ombi lao la kufyeka makaburu
Akamwachia Urais Mongusto Buthelezi aliposafiri. Akaunda tume ya Maridhiano ya kitaifa. Mandela akaacha uongozi baada ya kipindi kimoja tu. Haya ni kwa uchache

Je alikuwa strong leader, jibu ni ndiyo kwasababu aliamini katika utaifa na si yeye

Tofauti ya Tito na Mandela ni moja. Tito aliamini yeye ni taasisi kamili, Mandela aliamini uwepo wa Taasisi. Hata baada ya kufariki Afrika kusini imesimama imara licha ya kutabiriwa mabaya

Kwanini iwe South Africa na si Yugoslavia?
Jibu, South Africa ipo kwasababu ya uwepo wa strong institutions siyo strong leader

Hivyo kinachoanza ni strong leader anayeweza kujenga strong institution.
Miaka 50 ya mataifa ya Afrika kujitawala, muda wa kuwa na strong leaders umekwisha

Tunahitaji uwepo wa strong institutions zitakazoweza kutupa strong leaders.
Uwepo wa institutions imara ni kiungo muhimu cha 'vetting' ya strong leaders.
Hata ikitokea ''weak leader'' strong institutions zinachukua nafasi ya kuzibwa litakalotokea

Kama hatuna strong institutions, kila siku tutafanya 'lottery' ya kupata strong leaders
Afrika inahitaji strong institutions ili kupata strong leaders watakaotumikia institutions zilizopo
 
Shayu

Kuna misconception kati ya strong institutions na strong leaders
Ni muhimu kuangalia historia ya dunia kabla ya kuchukua upande au mtazamo

Kiongozi strong ni nani? Ni Josip Broz Tito wa Yugoslavia au Nelson Mandela wa Afrika kusini?

Tito aliweza kuziweka nchi ''nne'' kama nchi moja kwa mkono wa chuma kwa miaka zaidi ya 40
Baada ya kuondoka, Yugoslavia ikapaganyika kwa damu kila upande ukijitoa
Uwepo wa Yugoslavia ulitegemea 'strong leader' kama Josip Tito. Je, alikuwa strong, jibu ni yes.
Kwanini nchi iliparaganyika baada yake, jibu ni kuwa Tito kama mtu alikuwa ''strong institutions'' bila uwepo wa institutions

Mandela: Akiwa gerezani alikataa 'kutolewa' kwa masharti akiamini kufia gerezani kwa alichoamini ini sahihi. Alipoachiwa akakataa uenyekiti wa ANC kwa kutambua mchango na uwepo wa Tambo na ANC. Aliwakatalia Umkhonto Weswize ombi lao la kufyeka makaburu
Akamwachia Urais Mongusto Buthelezi aliposafiri. Akaunda tume ya Maridhiano ya kitaifa. Mandela akaacha uongozi baada ya kipindi kimoja tu. Haya ni kwa uchache

Je alikuwa strong leader, jibu ni ndiyo kwasababu aliamini katika utaifa na si yeye

Tofauti ya Tito na Mandela ni moja. Tito aliamini yeye ni taasisi kamili, Mandela aliamini uwepo wa Taasisi. Hata baada ya kufariki Afrika kusini imesimama imara licha ya kutabiriwa mabaya

Kwanini iwe South Africa na si Yugoslavia?
Jibu, South Africa ipo kwasababu ya uwepo wa strong institutions siyo strong leader

Hivyo kinachoanza ni strong leader anayeweza kujenga strong institution.
Miaka 50 ya mataifa ya Afrika kujitawala, muda wa kuwa na strong leaders umekwisha

Tunahitaji uwepo wa strong institutions zitakazoweza kutupa strong leaders.
Uwepo wa institutions imara ni kiungo muhimu cha 'vetting' ya strong leaders.
Hata ikitokea ''weak leader'' strong institutions zinachukua nafasi ya kuzibwa litakalotokea

Kama hatuna strong institutions, kila siku tutafanya 'lottery' ya kupata strong leaders
Afrika inahitaji strong institutions ili kupata strong leaders watakaotumikia institutions zilizopo
Huyo Tito alikuwa dikteta. Kama nilivyozungumza hapo mwanzo sizungumzii madikteta. Ambao hawaoni unuhimu wa kujenga strong institutions ambazo zitamsaidia hata kwenye kuongoza.

Madikteta na tyrants lengo lao si kuhudumia watu bali kujihudumia wenyewe na wananchi kuwa watwana. Hivyo institutions kuwa dhaifu kwao si tija. Tukumbuke taasisi huendeshwa na watu.

But again watu ndio wanafanya institution ziwe weak au strong. Ndio maana nikauliza uwekezaji wetu katika kuwajengea watu uwezo ukoje?
 
Huyo Tito alikuwa dikteta. Kama nilivyozungumza hapo mwanzo sizungumzii madikteta. Ambao hawaoni unuhimu wa kujenga strong institutions ambazo zitamsaidia hata kwenye kuongoza.

Madikteta na tyrants lengo lao si kuhudumia watu bali kujihudumia wenyewe na wananchi kuwa watwana. Hivyo institutions kuwa dhaifu kwao si tija. Tukumbuke taasisi huendeshwa na watu.

But again watu ndio wanafanya institution ziwe weak au strong. Ndio maana nikauliza uwekezaji wetu katika kuwajengea watu uwezo ukoje?
Hapa kuna tatizo la maana ya strong leader

Tunapoongelea strong leader hatuna maana nyingine zaidi ya leader anayechukua maamuzi hata kama yanakinzana na masilahi yake au kundi lake kwa masilahi mapana ya Umma .
Kiongozi mwenye maono (vision) na matamanio kwa jamii inayomhusu

Strong leader siyo lazima awe popular, kinachomtambulisha ni uwezo wa kupambanua mambo na kuyaweka katika muktadha sahihi kwa maslahi ya jamii husika

Nimekuonyesha Tito na Mandela makusudi kabisa uone maana ya strong leader

Hata kama utakuwa na kiongozi mzuri kiasi gani, kama hakuna strong institutions hakuna matokeo mazuri. Charisma ya kiongozi huyo itafunika responsibilities za institutions

Kinachotakiwa ni insitutions ambazo kiongozi yoyote awaye madarakani atasimama juu yake
Yaani insitutions ndizo zinamsimamisha na kumwelekeza kiongozi na si kinyume chake

Kuna mifano ninayoirudia sana ya mataifa yanayoendesha nchi bila kujali uwepo wa kiongozi

Nilivutiwa sana na UK kutokuwa na PM kwa wiki tatu bila kuathiri maisha.
Hii ni kwasababu institutions zinatimiza majukumu yake kwa misingi iliyoziweka na si personality

Likewise India, ilikaa miezi 3 bila PM na maisha yaliendelea kama kama vile hakuna kilichotokea
Hii ni kwasababu institutions zilikuwa imara zikitimiza majukumu yake bila kutegemea personality

Japan, PM ni mtumishi wa kawaida tu, anaweza kuingia ofisini asubuhi kama PM akatoka kama Raia. Ni suala la masaa tu. Kwa miaka 10 wamebadili PM zaidi ya 5
Maisha yanaendelea bila kujali nani amekalia kiti kwasababu institutions zinatimiza majukumu

Ujerumani, Angela Merkel ni weak kwasababu ya siasa za ndani hasa uundwaji wa serikali
Ujerumani hiyo hiyo inaongoza EU kwavile institutions zinafunika matatizo ya ndani

Nchi za Scandinavia ni stable sana, nikikuuliza kiongozi mmoja tu huenda usimfahamu
Lakini nchi hizo hazina matatizo kwasababu ya strong institutions na siyo personality

Tunahitaji strong institutions ili zitupe strong leader kwa ''vetting'' kwa maana ya uimara wa institutions ndio utatoa kiongozi imara na si kutegemea kupata strong leader kwa ''lottery''
 
Hapa kuna tatizo la maana ya strong leader

Tunapoongelea strong leader hatuna maana nyingine zaidi ya leader anayechukua maamuzi hata kama yanakinzana na masilahi yake au kundi lake kwa masilahi mapana ya Umma .
Kiongozi mwenye maono (vision) na matamanio kwa jamii inayomhusu

Strong leader siyo lazima awe popular, kinachomtambulisha ni uwezo wa kupambanua mambo na kuyaweka katika muktadha sahihi kwa maslahi ya jamii husika

Nimekuonyesha Tito na Mandela makusudi kabisa uone maana ya strong leader

Hata kama utakuwa na kiongozi mzuri kiasi gani, kama hakuna strong institutions hakuna matokeo mazuri. Charisma ya kiongozi huyo itafunika responsibilities za institutions

Kinachotakiwa ni insitutions ambazo kiongozi yoyote awaye madarakani atasimama juu yake
Yaani insitutions ndizo zinamsimamisha na kumwelekeza kiongozi na si kinyume chake

Kuna mifano ninayoirudia sana ya mataifa yanayoendesha nchi bila kujali uwepo wa kiongozi

Nilivutiwa sana na UK kutokuwa na PM kwa wiki tatu bila kuathiri maisha.
Hii ni kwasababu institutions zinatimiza majukumu yake kwa misingi iliyoziweka na si personality

Likewise India, ilikaa miezi 3 bila PM na maisha yaliendelea kama kama vile hakuna kilichotokea
Hii ni kwasababu institutions zilikuwa imara zikitimiza majukumu yake bila kutegemea personality

Japan, PM ni mtumishi wa kawaida tu, anaweza kuingia ofisini asubuhi kama PM akatoka kama Raia. Ni suala la masaa tu. Kwa miaka 10 wamebadili PM zaidi ya 5
Maisha yanaendelea bila kujali nani amekalia kiti kwasababu institutions zinatimiza majukumu

Ujerumani, Angela Merkel ni weak kwasababu ya siasa za ndani hasa uundwaji wa serikali
Ujerumani hiyo hiyo inaongoza EU kwavile institutions zinafunika matatizo ya ndani

Nchi za Scandinavia ni stable sana, nikikuuliza kiongozi mmoja tu huenda usimfahamu
Lakini nchi hizo hazina matatizo kwasababu ya strong institutions na siyo personality

Tunahitaji strong institutions ili zitupe strong leader kwa ''vetting'' kwa maana ya uimara wa institutions ndio utatoa kiongozi imara na si kutegemea kupata strong leader kwa ''lottery''
Unadhani watu waliojenga europe na kutayarisha misingi ya hawa waliopo walikuwa weak? Wote walikuwa very strong leaders. Ndio maana wakajenga taasisi imara. Hakuna strong leader ambaye ataingia kwenye madaraka na kuacha kujenga strong institutions. Na hizo strong institution pia zinategemea quality za watu. Na hazijiendeshi zenyewe bali watu. Institution zinamsaidia tu raisi kuleta informations ili aweze kufanya maamuzi sahihi. Lakini role ya kiongozi mwenye nguvu si nguvu tu hata busara iko pale pale hata kwa taifa la marekani. Leadership is about decision na mtu anaye determine future ya nchi ni raisi kwa maamuzi yake. Iwe kuhusu mahusiano ya kimataifa au mahusiano ya ndani na hata sera za kiuchumi. Policy za obama, bush na Trump sio sawa. Bush na chama chake waliwapeleka watu kwenye vita baadhi waliona haikuwa sahihi wengine waliona ok. Na policy mara nyingi zinabadilika kulingana na kiongozi aliyejuu na institutions kazi yake ni kumsaidia raisi kufikia malengo. Tusijidanganye kwamba tunaweza kutengeneza mifumo au institutions ambazo hata fool anaweza kuongoza NO. Tunahitaji kiongozi mwenye nguvu sio nguvu tu na busara. But siongelea kiongozi asiyeona umuhimu wa kujenga mifumo na kutaka kuonekana yeye tu ( one man show game) . Uongozi wa namna hii hauwezi kufika mbali. Lazima tujue kiongozi ni mtawala na ana mamlaka hata kwa hizo institutions na kama viongozi ni weak iwe raisi au bunge lenye viongozi weak na wasio na vision automaticaly nchi inakuwa haina dira. Kwahiyo mfano unataka kusema institution zetu ni weak ndio maana nchi masikini au tuna uhaba wa viongozi wenye busara na maono ya kutupeleka tunapotaka kwenda? Kipi kinaanza strong institution au strong leader? Again usiongelee tyrants and dictators ambao dhamira yao sio ku serve watu. Katika kesi ya Mandela sio yeye aliyejenga misingi na taasisi za Afrika kusini alikuta nchi ishajengwa labda harakati za kuondoa ubaguzi wa rangi tu.
 
Shayu nilitegemea ungeeleza kuhusu UK, Japan, India na jinsi nchi zilivyoweza kubaki imara hata pale kulipoonekana hakuna uongozi.
Mifumo imara ya taasisi inamsaidia kiongozi katika kutawala, lakini pia inamweka sawa kiongozi pale anapopotoka. Seneti ya Marekani imekataa kauli za Trump kuhusu EU na kupiga kura 98-100

Sheria anazotaka kuweka Trump zinagonga mwamba, kwasasa wanamjadala wa national debt
Jenerali wa Jeshi la US aliwahi kusimama na kutoa msimamo wa taasisi hiyo kuhusu kauli za kibaguzi anazotoa Rais Trump. Mahakama ingawa zimejigawa kiitikadi bado zinasimamia mifumo mingine. Intel community zinasimama na misimamo tofauti na ule wa Rais

Nikakupa mfano wa Japan ambako PM anaingia ofisini anatoka kama raia na nchi inaendelea
Hii maana yake ni kuwa insitutions zipo na zinafanya kazi bila kujali ''bright or fool in the office''

Kuna thin line between strong leader na Tyrant. Kuna tofauti ya wise leader na Dictator
Hatuhitaji kwenda mbali, hapa Tanzani, Mwalimu Nyerere baada ya Uhuru alijitahidi kujenga taasisi imara. Ingawa hakufanikiwa sana ni muhimu kusema 'taasisi' imara aliyojenga ni ya 'utaifa' Hili limetuweka pamoja hata anapotokea mtu wa kutugawa

Yes ni lazima upate kingozi imara wa kusimamia uundwaji wa taasisi imara, hata hivyo, miaka 50 baada ya uhuru hatupo katika stage hiyo.
Kwasasa tunahitaji institutions imara zitakazotusaidia tusirudi nyuma miaka 50 tuliyopita.

Tayari tume experience na kubaini tatizo letu ni taasisi imara. Hicho ndicho cha kufanyia kazi kwani uwezekano wa kupata strong leader si suala la kubahatisha, wapo kwa maelefu

Muhimu kujua ni kwamba strong leader anatakiwa awe na strong institutions na hapo ndipo pa kuanzia. Tujenge institutions imara, hatuna uhaba wa strong leaders
 
Shayu nilitegemea ungeeleza kuhusu UK, Japan, India na jinsi nchi zilivyoweza kubaki imara hata pale kulipoonekana hakuna uongozi.
Mifumo imara ya taasisi inamsaidia kiongozi katika kutawala, lakini pia inamweka sawa kiongozi pale anapopotoka. Seneti ya Marekani imekataa kauli za Trump kuhusu EU na kupiga kura 98-100
undefined
Sheria anazotaka kuweka Trump zinagonga mwamba, kwasasa wanamjadala wa national debt
Jenerali wa Jeshi la US aliwahi kusimama na kutoa msimamo wa taasisi hiyo kuhusu kauli za kibaguzi anazotoa Rais Trump. Mahakama ingawa zimejigawa kiitikadi bado zinasimamia mifumo mingine. Intel community zinasimama na misimamo tofauti na ule wa Rais
undefined
Nikakupa mfano wa Japan ambako PM anaingia ofisini anatoka kama raia na nchi inaendelea
Hii maana yake ni kuwa insitutions zipo na zinafanya kazi bila kujali ''bright or fool in the office''
undefined
Kuna thin line between strong leader na Tyrant. Kuna tofauti ya wise leader na Dictator
Hatuhitaji kwenda mbali, hapa Tanzani, Mwalimu Nyerere baada ya Uhuru alijitahidi kujenga taasisi imara. Ingawa hakufanikiwa sana ni muhimu kusema 'taasisi' imara aliyojenga ni ya 'utaifa' Hili limetuweka pamoja hata anapotokea mtu wa kutugawa
undefined
Yes ni lazima upate kingozi imara wa kusimamia uundwaji wa taasisi imara, hata hivyo, miaka 50 baada ya uhuru hatupo katika stage hiyo.
Kwasasa tunahitaji institutions imara zitakazotusaidia tusirudi nyuma miaka 50 tuliyopita.
undefined
Tayari tume experience na kubaini tatizo letu ni taasisi imara. Hicho ndicho cha kufanyia kazi kwani uwezekano wa kupata strong leader si suala la kubahatisha, wapo kwa maelefu
undefined
undefined
Problem sio taasisi imara tatizo ni jinsi gani tuna wa groom watu wetu kuingia kwenye utumishi wa umma na katika taasisi zetu. Viongozi wetu tunawatayarishaje? a strong leader hutayarisha watu wake na future ya taifa lolote imelala kwa watu wake, Na kwambia tena kama watu wakiwa corrupt hakuna taasisi itakayokuwa imara, ikiwa watu hawana principals hakuna kitakachojengeka. Nadhani huu ni ukweli usiopingika. Future ya taifa hili inategemea how well we trained our people especial youth. Kwahiyo matayarisho haya lazima yafanywe kwa makini kwasababu kizazi chetu kisipokuwa bora tusitegemee kizazi kijacho kitakuwa bora unless we change. Taifa huwa strong as well as its institution kutegemea watu wao ni bora kiasi gani. Nikimaanisha intelligence zao, maadili yao na how well we are organized. Pia inategemea institutions zetu zina zinasimamia values kiasi gani na hizo values zinakuwa manifested kwa watu? We need strong leader with good ideas. Ambaye atatengeneza strong institutions na ku instill values kwenye taifa letu. Without values taifa letu halitakuwa na dira watu watajifanyia tu wanayotaka. Institutions za Japan na nchi unazosema ni bora kwa kuwa wametrain watu wao na walikuwa na strong leaders walioweka misingi kwa mataifa yao. Huwezi kufananisha mataifa yao ambayo tayari yako well grounded na mataifa yetu. Kwa mataifa yetu ambayo still weak na institutions zetu bado ni very weak tunahitaji strong leaders. Watu wetu wanahitaji kukua bado na hata katika umoja bado hatujafikia kiwango cha juu cha umoja wetu. Kwa nchi kama zetu kauli ya Obama hai apply. People are still ignorant and selfish na watu utaifa finyu. And as a nation we lack a sense of purpose and direction. Bado naamini tunahitaji a strong and wise leader not a weak kwasababu bado hatuko well grounded. We need a leader with the superior intellect. We are poor because we lack knowledge. And if we want to move forward we must pursue knowledge. We must pursue knowledge to help the nation. We need our people to be moral na kama tukijenga institutions zet kuwa na watu ambao ni moral, watu wetu automatic watakuwa moral, kwasababu values za institutions zitakuwa reflected katika jamii, through education,religion, laws na makuzi katika familia hivi vitu vina co relate. Na kama watu wetu wakiwa moral na wakiwa wana values watahoji kila jambo baya atakalofanya kiongozi. Katika mfumo mzuri ni vigumu kiongozi mbaya kupita kwasababu watu watakuwa grounded kwenye moral values zao. Kinyume chake ni kweli kama sisi sio moral tusitegemee viongozi moral. Na tusitegemee kuwa na institution imara kama watu wetu sio moral. Wenye uwezo wa kusema hiki ndio au hiki hapana hakina interest kwa taifa letu na jamii yetu. Ama sivyo tutakuwa wana viongozi matapeli tu. Kwa mazingira ya nchi yetu na mataifa mengi ya afrika bado tunahitaji strong leaders. Again kama mnavyosema kiongozi mpumbavu ataingiaje madarakani katika nchi yenye mifumo mizuri na institution bora? Eg mifumo mizuri ya elimu na ya kufanya vetting kwa viongozi? If people are good automatic we will get good leaders. Nenda kasome federalist pepars za akina James madison na hamilton signatories wa declaration of America independence na constitution of AMERICA. Wanasema kabisa kama wamarekani watakuwa sio moral people au wakaacha values za ambazo zimewaunganisha hata katiba yao haitafunction na kama haitafunction that means hata institution zao zitakuwa weak. There is deterioration of institutions and even for strong nations what make them deterioriate? Kukiuka misingi ambayo imejenga nchi hizo. kukiuka values ambazo zimejenga mataifa hayo. When countries do good things yanakuwa and when they fail to hold on what is good they fall down.
undefined
undefined
undefined
Muhimu kujua ni kwamba strong leader anatakiwa awe na strong institutions na hapo ndipo pa kuanzia. Tujenge institutions imara, hatuna uhaba wa strong leaders
undefined
 
Problem sio strong leader tatizo ni jinsi gani tuna wa groom watu wetu kuingia kwenye utumishi wa umma na katika taasisi zetu. Viongozi wetu tunawatayarishaje? a strong leader hutayarisha watu wake na future ya taifa lolote imelala kwa watu wake, Na kwambia tena kama watu wakiwa corrupt hakuna taasisi itakayokuwa imara, ikiwa watu hawana principals hakuna kitakachojengeka. Nadhani huu ni ukweli usiopingika. Future ya taifa hili inategemea how well we trained our people especial youth. Kwahiyo matayarisho haya lazima yafanywe kwa makini kwasababu kizazi chetu kisipokuwa bora tusitegemee kizazi kijacho kitakuwa bora unless we change. Taifa huwa strong as well as its institution kutegemea watu wao ni bora kiasi gani. Nikimaanisha intelligence zao, maadili yao na how well we are organized. Pia inategemea institutions zetu zina zinasimamia values kiasi gani na hizo values zinakuwa manifested kwa watu? We need strong leader with good ideas. Ambaye atatengeneza strong institutions na ku instill values kwenye taifa letu. Without values taifa letu halitakuwa na dira watu watajifanyia tu wanayotaka. Institutions za Japan na nchi unazosema ni bora kwa kuwa wametrain watu wao na walikuwa na strong leaders walioweka misingi kwa mataifa yao. Huwezi kufananisha mataifa yao ambayo tayari yako well grounded na mataifa yetu. Kwa mataifa yetu ambayo still weak na institutions zetu bado ni very weak tunahitaji strong leaders. Watu wetu wanahitaji kukua bado na hata katika umoja bado hatujafikia kiwango cha juu cha umoja wetu. Kwa nchi kama zetu kauli ya Obama hai apply. People are still ignorant and selfish na watu utaifa finyu. And as a nation we lack a sense of purpose and direction. Bado naamini tunahitaji a strong and wise leader not a weak kwasababu bado hatuko well grounded. We need a leader with the superior intellect. We are poor because we lack knowledge. And if we want to move forward we must pursue knowledge. We must pursue knowledge to help the nation. We need our people to be moral na kama tukijenga institutions zet kuwa na watu ambao ni moral, watu wetu automatic watakuwa moral, kwasababu values za institutions zitakuwa reflected katika jamii, through education,religion, laws na makuzi katika familia hivi vitu vina co relate. Na kama watu wetu wakiwa moral na wakiwa wana values watahoji kila jambo baya atakalofanya kiongozi. Katika mfumo mzuri ni vigumu kiongozi mbaya kupita kwasababu watu watakuwa grounded kwenye moral values zao. Kinyume chake ni kweli kama sisi sio moral tusitegemee viongozi moral. Na tusitegemee kuwa na institution imara kama watu wetu sio moral. Wenye uwezo wa kusema hiki ndio au hiki hapana hakina interest kwa taifa letu na jamii yetu. Ama sivyo tutakuwa wana viongozi matapeli tu. Kwa mazingira ya nchi yetu na mataifa mengi ya afrika bado tunahitaji strong leaders. Again kama mnavyosema kiongozi mpumbavu ataingiaje madarakani katika nchi yenye mifumo mizuri na institution bora? Eg mifumo mizuri ya elimu na ya kufanya vetting kwa viongozi? If people are good automatic we will get good leaders. Nenda kasome federalist pepars za akina James madison na hamilton signatories wa declaration of America independence na constitution of AMERICA. Wanasema kabisa kama wamarekani watakuwa sio moral people au wakaacha values za ambazo zimewaunganisha hata katiba yao haitafunction na kama haitafunction that means hata institution zao zitakuwa weak. There is deterioration of institutions and even for strong nations what make them deterioriate? Kukiuka misingi ambayo imejenga nchi hizo. kukiuka values ambazo zimejenga mataifa hayo. When countries do good things yanakuwa and when they fail to hold on what is good they fall down.
undefinedundefined
 
Hi Shayu
Sijui una maana gani kwa neno 'undefined', hasa sisi tulioishia std VII C.
Tunaweza kuwa na civil discussions without demeaning each other. Maana halisi ya mjadala ni kuwa na maoni hata kama hayafanani. Maoni ni haki ya mtu lakini si facts. Anyways
"Shayu, post: 27824850, member: 44491"]Problem sio strong leader tatizo ni jinsi gani tuna wa groom watu wetu kuingia kwenye utumishi wa umma na katika taasisi zetu. Viongozi wetu tunawatayarishaje?
Na hapa kuna mfano mzuri. Chuo kikuu Dar es Salaam nyakati za Mwalimu kilikuwa chemchem ya fikra kitaifa na kimataifa.

Haya siyasemi mimi waulize akina Walter Rodney, Oliver Tambo, Mbeki,Museveni, Eriya Kategaya, Garang na wengi tu kwa idadi kubwa

Ilikuwa institution iliyoandaa watu katika utumishi wa umma kwa ujumla wake
UDSM ilifanya hayo kama 'strong institution' ikibeba jukumu la kuaanda viongozi kama ulivyosema.

Kuna kesi inayoendelea ya kijana mmoja kutuhumiwa kutenda kosa. Kilichoshangaza ni UDSM ikutelekeza jukumu lake kama 'institution' na kuchukua maamuzi katika mtazamo wa kisiasa. Kwamba, seneti ya chuo, na 'sheria za chuo(by law)' hazikuzingatiwa.

Kwa mfano huo, udhaifu wa institution kama UDSM utazaa viongozi dhaifu and it gonna be a vicious circle. Hilo linaonekana pia katika institution zingine Bunge likiwemo. Niachie hapo
a strong leader hutayarisha watu wake na future ya taifa lolote imelala kwa watu wake, watu wakiwa corrupt hakuna taasisi itakayokuwa imara, ikiwa watu hawana principals hakuna kitakachojengeka. Nadhani huu ni ukweli usiopingika.
Watu hawawezi kuwa na principals bila kuwa na institution zinazojenga na kusimamia principals.

Ukiwa na weak institution huwezi kuwa na watu wenye principals. Ukisoma historia ya kuanzishwa kwa baadhi ya institutions msingi mkubwa ulikuwa kusimamia principals za jamii

Tulikuwa na strong leader Sokoine aliyetaka kumaliza corruption nchini. Jitihada zilionekana hata hivyo hazikuwa sustainable. Baada yake rushwa ilichanua zaidi. Hii ni kwasababu hakukuwepo strong institutions za kusimamia idea na project ikawa unsustainable
Future ya taifa hili inategemea how well we trained our people especial youth. matayarisho haya lazima yafanywe kwa makini izazi chetu kisipokuwa bora tusitegemee kizazi kijacho kitakuwa bora unless we change. Taifa huwa strong as well as its institution kutegemea watu wao ni bora kiasi gani. Nikimaanisha intelligence zao, maadili yao na how well we are organized. Pia inategemea institutions zetu zina zinasimamia values kiasi gani na hizo values zinakuwa manifested kwa watu?
Nakubaliana nawe kuhusu kizazi kijacho na kilichopo
Sikubaliani nawe kuhusu Taifa kuwa strong ili kuwa na strong institutions, the opposite is true
Huwezi kusimamia values ukiwa na weak institutions, ni lazima uanze na strong institutions ili ujenge strong nation'
We need strong leader with good ideas. Ambaye atatengeneza strong institutions na ku instill values kwenye taifa letu. Without values taifa letu halitakuwa na dira watu watajifanyia tu wanayotaka.
Tunahitaji strong institutions zitakazotuongoza kutengeneza dira ya taifa zikiwemo values ambazo viongozi watawajibika kuzisimamia.
Institutions za Japan na nchi unazosema ni bora kwa kuwa wametrain watu wao na walikuwa na strong leaders walioweka misingi kwa mataifa yao. Huwezi kufananisha mataifa yao ambayo tayari yako well grounded na mataifa yetu.
Hili ni kosa, lazima tujifananishe nao kwasababu sisi ni Taifa kama wao. In fact tulipaswa tuwe mbele yao kwasababu wametutengenezea 'template' sisi hatuwezi kuitumia. Tukijaribu kufanya yetu kama tunaishia kwa yale ya Katiba mpya. Tunazunguka na kurudi pale pale hatuna strong institutions zinazotusimamia sisi kama wananchi
And as a nation we lack a sense of purpose and direction.
Sababu kubwa ni kukosekana kwa strong institutions zinazoweza kusimama kwa niaba ya wananchi
Sense of purpose and directions haitoki kwa mtu inatoka kwa wananchi.
Institutions zetu zimekuwa subdued na kushindwa ku 'deliver' hasakatika vetting ya kupata strong leaders. Hatuna uhaba wa strong leaders Shayu, tuna ubaya wa vetting unaosababishwa na weak institutions. Tukifanikiwa kuziimarisha tutapiga hatua

Nikuache na kamfano tu, tumeshindwa kuandika katiba mpya kwasababu moja, tulitegemea viongozi waendeshe machakato na si institutions. Yalipotokea matatizo hakukuwepo institutions za ku rectify the situation.

Wazo la katiba mpya siyo la kiongozi, yalikuwa mawazo ya wananchi ambayo kwa bahati nzuri kiongozi aliyekuwepo aliyasikia. Mchakato wa katiba ulishindikana kwasababu haukusimamiwa na institutions bali matakwa ya watu wachache

Jambo la muhimu katika mapendekezo ya katiba ilikuwa kujenga strong institutions
Ukisoma ile rasimu utaona sehemu kubwa ilikuwa kuwapa wananchi madaraka kupitia institution imara ikiwaacha viongozi kama wasimamizi wa institutions hizo
 
Hi Shayu
Sijui una maana gani kwa neno 'undefined', hasa sisi tulioishia std VII C.
Tunaweza kuwa na civil discussions without demeaning each other. Maana halisi ya mjadala ni kuwa na maoni hata kama hayafanani. Maoni ni haki ya mtu lakini si facts. Anyways
Na hapa kuna mfano mzuri. Chuo kikuu Dar es Salaam nyakati za Mwalimu kilikuwa chemchem ya fikra kitaifa na kimataifa.

Haya siyasemi mimi waulize akina Walter Rodney, Oliver Tambo, Mbeki,Museveni, Eriya Kategaya, Garang na wengi tu kwa idadi kubwa

Ilikuwa institution iliyoandaa watu katika utumishi wa umma kwa ujumla wake
UDSM ilifanya hayo kama 'strong institution' ikibeba jukumu la kuaanda viongozi kama ulivyosema.

Kuna kesi inayoendelea ya kijana mmoja kutuhumiwa kutenda kosa. Kilichoshangaza ni UDSM ikutelekeza jukumu lake kama 'institution' na kuchukua maamuzi katika mtazamo wa kisiasa. Kwamba, seneti ya chuo, na 'sheria za chuo(by law)' hazikuzingatiwa.

Kwa mfano huo, udhaifu wa institution kama UDSM utazaa viongozi dhaifu and it gonna be a vicious circle. Hilo linaonekana pia katika institution zingine Bunge likiwemo. Niachie hapo Watu hawawezi kuwa na principals bila kuwa na institution zinazojenga na kusimamia principals.

Ukiwa na weak institution huwezi kuwa na watu wenye principals. Ukisoma historia ya kuanzishwa kwa baadhi ya institutions msingi mkubwa ulikuwa kusimamia principals za jamii

Tulikuwa na strong leader Sokoine aliyetaka kumaliza corruption nchini. Jitihada zilionekana hata hivyo hazikuwa sustainable. Baada yake rushwa ilichanua zaidi. Hii ni kwasababu hakukuwepo strong institutions za kusimamia idea na project ikawa unsustainable
Nakubaliana nawe kuhusu kizazi kijacho na kilichopo
Sikubaliani nawe kuhusu Taifa kuwa strong ili kuwa na strong institutions, the opposite is true
Huwezi kusimamia values ukiwa na weak institutions, ni lazima uanze na strong institutions ili ujenge strong nation'
Tunahitaji strong institutions zitakazotuongoza kutengeneza dira ya taifa zikiwemo values ambazo viongozi watawajibika kuzisimamia.
Hili ni kosa, lazima tujifananishe nao kwasababu sisi ni Taifa kama wao. In fact tulipaswa tuwe mbele yao kwasababu wametutengenezea 'template' sisi hatuwezi kuitumia. Tukijaribu kufanya yetu kama tunaishia kwa yale ya Katiba mpya. Tunazunguka na kurudi pale pale hatuna strong institutions zinazotusimamia sisi kama wananchi Sababu kubwa ni kukosekana kwa strong institutions zinazoweza kusimama kwa niaba ya wananchi
Sense of purpose and directions haitoki kwa mtu inatoka kwa wananchi.
Institutions zetu zimekuwa subdued na kushindwa ku 'deliver' hasakatika vetting ya kupata strong leaders. Hatuna uhaba wa strong leaders Shayu, tuna ubaya wa vetting unaosababishwa na weak institutions. Tukifanikiwa kuziimarisha tutapiga hatua

Nikuache na kamfano tu, tumeshindwa kuandika katiba mpya kwasababu moja, tulitegemea viongozi waendeshe machakato na si institutions. Yalipotokea matatizo hakukuwepo institutions za ku rectify the situation.

Wazo la katiba mpya siyo la kiongozi, yalikuwa mawazo ya wananchi ambayo kwa bahati nzuri kiongozi aliyekuwepo aliyasikia. Mchakato wa katiba ulishindikana kwasababu haukusimamiwa na institutions bali matakwa ya watu wachache

Jambo la muhimu katika mapendekezo ya katiba ilikuwa kujenga strong institutions
Ukisoma ile rasimu utaona sehemu kubwa ilikuwa kuwapa wananchi madaraka kupitia institution imara ikiwaacha viongozi kama wasimamizi wa institutions hizo
Naomba nikuulize ni kina nani wanaendesha hizi institutions na waliozianzisha? Embu angalia founders wa hayo mataifa Tuanzie Russia, USA, United Kingdom, France , Japan , German, china.. Wote hawakuwa weak leaders na na hao ndio waliojenga misingi na taasisi unazosema imara and Na lukumbusha tena taasisi hazijiendeshi zenyewe zinaendeshwa na watu. Marekani right now walikuwa wana complain ubora wa elimu yao umeshuka why umeshuka kama kuwa na taasisi imara bila watu bora kila kitu kinakuwa sahihi. Go and study federalist pepars za akina james Madison na Hamilton.
 
Kuhusu hilo neno undifined limekuja tu liko kwenye setting ya JF...wala sikutaka liwepo.
 
"Virtue must underlay all institutional arrangements if they are to be healthy and strong. The principles of democracy are as easily destroyed as human nature is corrupted!' - John Adams
 
Back
Top Bottom