Viongozi wa dini waiweka Serikali pabaya kuhusu Katiba Mpya

Viongozi wa dini waiweka Serikali pabaya kuhusu Katiba Mpya

Hivi ni kwa nn viongozi wote wa dini ya kiislamu wana macho mekundu? Just curious


Umejaa uchonganishi kwa kukalia kuangalia macho ya viongozi wa dini inaelekea wewe ni agent wa mauaji ya vikongwe hii concept inakujaje humu fikiri sawasawa acha michepuko!!!!
 
Hii katiba haitakiwi ipigiwe kura kipindi hiki cha uchaguzi yaani yatakiwa tusubiri uchaguzi uishe maana kwa sasa tutapata madudu sio katiba turekebishe tume ya uchaguzi mambo yaendeleee vinginevyo kazi ipoo udini utatumaliza


Hiyo siyo kazi yako waachie wananchi na serikali yao hujui kitu!
 
Wakienda shinyanga wanakouwa vikongwe, hakyanani hawarudi hao.

Shehe Mkuu anatoka Shinyanga, ambapo tatizo la kukosa kuni za kupitia ziliwafanya wenyeji wake kutumia kinyesi cha ng'ombe kama nishati ya kupikia.

Sasa kwa umri aliofika na tatizo la hilo LA kupikia kinyesi cha ngo'ombe badala ya kumi au mkaa ndipo linakuja suala LA macho mekundu. Rejea mauaji ya wazee huko Shinyanga na macho yao mekundu.
 
tatizo la viongozi wa kislamu ni shule,wao wanajua sana kuruani, hivyo ukijua tu kuruani na hadith za mtume unapewa usheik! na uongozi hili ni tatizo kubwa,sasa angalia baada ya kuambiwa hakuna kadhi ndio wanasema hawapigi kura,yaani hawajaona mapungufu yoyote kwenye katiba zaidi ya kadhi,jamani haya ni matatizo,angalia sasa tofauti na wakristo, kwanza wameji organise wote, tamko limetoka kuhusu katiba kwa ujumla wake kwamba katiba haifai,hii sasa ndio shule,ndugu waislam badilikeni jiwekeeni misingi ya uongozi,kwamba hata kama mtu anajua kuruani anapotakiwa kua kiongozi hata wa msikiti awe basi japo na diploma,binafsi mmenikera sana yaani mgepewa kadhi ilikua mnaipigia katiba ndio?whater fuk!!
 
tatizo la viongozi wa kislamu ni shule,wao wanajua sana kuruani, hivyo ukijua tu kuruani na hadith za mtume unapewa usheik! na uongozi hili ni tatizo kubwa,sasa angalia baada ya kuambiwa hakuna kadhi ndio wanasema hawapigi kura,yaani hawajaona mapungufu yoyote kwenye katiba zaidi ya kadhi,jamani haya ni matatizo,angalia sasa tofauti na wakristo, kwanza wameji organise wote, tamko limetoka kuhusu katiba kwa ujumla wake kwamba katiba haifai,hii sasa ndio shule,ndugu waislam badilikeni jiwekeeni misingi ya uongozi,kwamba hata kama mtu anajua kuruani anapotakiwa kua kiongozi hata wa msikiti awe basi japo na diploma,binafsi mmenikera sana yaani mgepewa kadhi ilikua mnaipigia katiba ndio?whater fuk!!

Nilikua napitia mchango wako nikadhani ukeandika hoja ya maana kumbe na wewe mi yale yale mchonganishi masuala ya elimu za viongozi wetu wa dini yanatafuta nini humu JF,ch
ondechonde jambo hili halina maana humu tujielekeze kwenye mambo ya msingi.
 
Nilikua napitia mchango wako nikadhani ukeandika hoja ya maana kumbe na wewe mi yale yale mchonganishi masuala ya elimu za viongozi wetu wa dini yanatafuta nini humu JF,ch
ondechonde jambo hili halina maana humu tujielekeze kwenye mambo ya msingi.

hawana sasa elimu kwa hiyo tunyamaze,wewe huoni tatizo hapo linalotokana na elimu, ambalo ndio lilikua linatupeleka kwenye tatizo kubwa la katiba,yaani waislam wangepewa kadhi walikua wanapitisha katiba,na tena wanasema waziwazi kwakua kadhi hakuna sasa ndio hatupigi kura,tatizo waloliona ni kadhi tu alahauraa salaaree!! hamna shule hapo na bila kuambiana ukweli nakwambia tutakwama
 
hawana sasa elimu kwa hiyo tunyamaze,wewe huoni tatizo hapo linalotokana na elimu, ambalo ndio lilikua linatupeleka kwenye tatizo kubwa la katiba,yaani waislam wangepewa kadhi walikua wanapitisha katiba,na tena wanasema waziwazi kwakua kadhi hakuna sasa ndio hatupigi kura,tatizo waloliona ni kadhi tu alahauraa salaaree!! hamna shule hapo na bila kuambiana ukweli nakwambia tutakwama

Usihukumu watu kwa ujumla wao! Na wala usiwadharau watu kwa dini yao. Usiwe muongo, Waislam hawana elimu? Siii kweli kuna Waislam wanaelimu nzuri saaana tena ni wasomi wa hali ya juu nchini kuliko unavyodhani wewe. Kusema hawana elimu "hamna shule hapo".



Huu ni udhalilishaji, upotoshaji na kutoheshimu dini za wengine zaidi ya hayo tabia hii inaleta mwelekeo wa uchochezi baina ya Wakristo na Waislam. Tabia hii siii njema na wala hatupaswi kifumbia macho, ni wajibu wetu sote wenye mapenzi mema na nchi kukemea tabia hii yenye kichochezi.
 
[h=2]Mahakama ya Kadhi Haipo kwenye Quran[/h]
Ndugu wasomaji.

Leo ningependa kusema kuwa, dai la Waislam wa Tanzania la Mahakama ya Kadhi halina msingi wala usaidizi wa Quran.

Kwa wanao ifahamu Quran, watakubaliana na mimi kuwa HAKUNA AYA HATA MOJA ambayo Allah alisema na au Waamrisha Waislam waende kwenye Mahakama ya Kadhi. Narudia tena hakuna aya.

SASA NDUGU WAISLAM:


1. Who appoints Chief Kadhi and Kadhis?

2. What are the qualification for appointment to the office of a Kadhi (including a Chief Kadhi)?

3. Since the Kadhis are not trained lawyers who understand the Evidence Act and the Civil Procedure Act, how and/or what will they use to administer their Courts?

4. Muslims are mainly of two sects in Tanzania - the Sunni and Shia. Majority of the Muslims in Tanzania are Sunni Muslims but there is a significant population of Shia Muslims too and consideration ought to be given to the appointment of Kadhis of the Shia Sect to cater the interest of the Shia Muslims. Will they have two different Courts? For Sunni and Shia?

5. How will Muslim Women be protected since: Muslim law regards women as less than men in matters of both marriage and divorce, as well as devolution of property: Holy Quran Surah 2:228-232, and Surah 65:1-7 (only a man may divorce his wife even if he is required to provide for her); a man may beat his wife, even if lightly, the evidence of two women, is equal to evidence of one man (Surah 2:282). The application of such beliefs of faith are contrary to the Constitution.


Islamic "Kadhi" courtsis illegal and discriminatory.


Kwanini mnamsaidia Allah kwa kuanzisha Mahakama ya Kadhi?
 
Usihukumu watu kwa ujumla wao! Na wala usiwadharau watu kwa dini yao. Usiwe muongo, Waislam hawana elimu? Siii kweli kuna Waislam wanaelimu nzuri saaana tena ni wasomi wa hali ya juu nchini kuliko unavyodhani wewe. Kusema hawana elimu “hamna shule hapo”.



Huu ni udhalilishaji, upotoshaji na kutoheshimu dini za wengine zaidi ya hayo tabia hii inaleta mwelekeo wa uchochezi baina ya Wakristo na Waislam. Tabia hii siii njema na wala hatupaswi kifumbia macho, ni wajibu wetu sote wenye mapenzi mema na nchi kukemea tabia hii yenye kichochezi.

ulitakiwa uanze kusoma post yangu ya mwanzo,ndio hayo ninayosema shule, na wewe umekurupuka tu kwanza acha jazba,basi ngoja nirudie nilisema viongozi wa dini ya kislamu,ni yule mtu anaejua kuruani na hadith za mtume, ukijua tu hayo basi tayari wewe ni sheikh! na uongozi unapata uwe wa msikiti au jumuiya,waislamu wenye proffesional zao hapa hawapo,na wala hawawezi kupata uongozi sababu kuruani na hadith za mtume hawako vizuri,usichanganye mama ni vizuri ukasoma post yangu ya kwanza,hizi shule jamani
 
Yote haya ameyasababisha kikwete,sita, pinda na ccm yao kwa matumizi ya rushwa na udanganyifu ili kujimlikisha utawala wa nch ambayo ni ya Wtanzania.

Aliyewahadaa kuwapa mahakama si serikali bali ni ccm, hivyo wamalizane na ccm.

Lakini pia waislam waache kujidharaulisha kwamba hawana akili za kuelewa kwamba nchi hii inaongozwa kwa katiba. Katiba ya nchf hairuhusu serikali kufungamana na imani ya dini yoyote. Mbona hilo liko dhahiri? Kwa nini hawataki kukubali kwamba walidanganywa wakalichukua kama somo badala yake wanazidi kulazimisha tu kwamba udanganyifu huo uhalalishwe? Kweli wao ina maana hawajui umuhimu na uzuri wa kuheshimu katiba ya nchi?

Ina maana waislam hao, mtu akiwaambia wafanye naye biashara kwa ahadi kwamba atawapa mlima kilimanjaro na kuwamilikisha wizara ya fedha watakubali tu kwa kuwa wameahidiwa bila kujali uwezo na uhalali wa kutekelezeka kwa hiyo ahadi? Hawawezi kujua kwamba mlima Kilimanjaro haumilikiwi na mtu na kwamba hakuna mtu anaweza kuwapa wao wizara ya fedha? Kwa nini hawataki kuona kwamba ccm si mmililki wa katiba na hana uwezo wa kuvunja katiba na kuifanya atakavyo kwa kuwa katiba ni ya serikali na serikli ni ya watu wengine na si mali ya ccm?

Pamoja na kujua kwamba wamehadaiwa, kwa nini sasa wazidi kulazimisha Watanzania wenye katiba waivunje ili kutimiza ahadi laghai za ccm? Waislam ni watu wenye ufaham wao na akli. Sidani wanaweza kuwa watu wasioelewa kiasi hiki ch a kuendelea kulazimisha serikali itekeleze maagano yao haram na ccm.

Hakuna dini iliyoiweka mahala pabaya serikali. Serikali kwa tamaa ya ccm ndiyo imeiweka pabaya serikali kwa kujiingiza katika masuala ya dini zlizokuwa zimetuliwa zikiheshimu katiba ya nchi.

Dawa pekee si kuendeleza unafiki na kujenga nyufa na mitafaruku inayopelekea machafuko makubwa nchini. Serikali irudi kwenye nafasi yake ya kusimamia na kulinda katiba ya nchi!.

Kinyume cha pale, hakuna amani kwa kuendesha nchi kinafiki huku mkivuruga na kutengeneza machafuko kwa mikono yenu. NJE YA KATIBA HAKUNA MAELEWANO.


Maelezo yako nimeyapata japo ni makali naona umekubali mwenyewe nje ya Katiba hakuna Maelewano kwa maana ya Ukawa walipogomea mchakato wa KaTIBA MPYA walichemka na zaidi unawahamasisha watanzania bila kujali tofauti zao za dini kuipigia kura nyingi za ndiyo kwa kuzingatia msingi uliomo kwenye katika wa kutofungamanisha shughuli za serikali na dini.
 
....hadithi baba mmoja alikuwa na watoto wawili mmoja akawa anabomoa ukuta wa nyumba yao pekee inayotegemewa na mwingine akawa anamzuia hakumuelewa akaenda kumweleza baba yao(serikali) cha kushangaza baba akasema mwache aendelee kubomoa kwa sababu ashazoea!!! kilichoendelea mimi sikuhadithiwa tena.
 
Hii katiba haitakiwi ipigiwe kura kipindi hiki cha uchaguzi yaani yatakiwa tusubiri uchaguzi uishe maana kwa sasa tutapata madudu sio katiba turekebishe tume ya uchaguzi mambo yaendeleee vinginevyo kazi ipoo udini utatumaliza

usiingilie mamlaka yasiyokuhusu wewe sio Serikali, mimi nasubiri taarifa rasmi kuhusu yatakayojiri,nachojuanmimi kura ya maoni kwa katiba inayopendekezwa haiepukiki nchini.
 
katiba+mpya+picha.gif

KWA UFUPI
Akizungumza jana ikiwa ni siku moja baada ya Rais Jakaya Kikwete kusema viongozi wa dini walitoa matamko ya hasira na yasiyokuwa na tija walipowataka wananchi kuipigia kura ya hapana Katiba Inayopendekezwa, Makamu wa Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania, (TEC),Askofu Severin Niwemugizi alisema kulazimisha Katiba ipite kama ilivyo ni udhaifu mkubwa kwa sababu ina upungufu mkubwa ambao hautaweza kurekebishwa baadaye.


Dar es Salaam. Viongozi wa dini za Kikristo na Kiislamu wameendelea kuiweka Serikali katika wakati mgumu baada ya kusema hawataiunga mkono Katiba Inayopendekezwa ikiwa matakwa yao hayatazingatiwa.

Akizungumza jana ikiwa ni siku moja baada ya Rais Jakaya Kikwete kusema viongozi wa dini walitoa matamko ya hasira na yasiyokuwa na tija walipowataka wananchi kuipigia kura ya hapana Katiba Inayopendekezwa, Makamu wa Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania, (TEC),Askofu Severin Niwemugizi alisema kulazimisha Katiba ipite kama ilivyo ni udhaifu mkubwa kwa sababu ina upungufu mkubwa ambao hautaweza kurekebishwa baadaye.

“Naikataa kwa asilimia 100. Kwa kifupi, Rais akubali kutokukubaliana na sisi.”

Wakati askofu huyo akisema hayo, Sheikh Mkuu wa Tanzania, Mufti Issa Shaaban Simba amesema iwapo Serikali haitaitambua Mahakama ya Kadhi na makadhi, Waislamu wataususia mchakato wa upigaji wa kura ya maoni kupitisha Katiba Inayopendekezwa.

Askofu Niwemugizi

Akizungumzia kauli hiyo ya Rais Kikwete, Askofu Niwemugizi alisema msimamo wa Jukwaa la Wakristo wa kuipigia kura ya hapana Katiba Inayopendekezwa haukuwa wa hasira, bali uliangalia kwa mapana masilahi ya Taifa katika miaka 200 ijayo.

Alisema ni udhaifu mkubwa kulazimisha kuipitisha Katiba ikiwa na upungufu na kusisitiza kuwa inatakiwa kutengenezwa kwa ustadi kwa sababu inagusa maisha ya Watanzania.

“Anaposema tamko letu lilikuwa la hasira na kuwa tuwaache wananchi waamue wenyewe anakosea kwa sababu Serikali yenyewe tangu ilipoizindua ilikuwa inawahamasisha wananchi waipigie kura ya ndiyo.

“Rais anaposema tusiwaamulie wananchi anakosea kwani hata sisi ni wananchi, lakini pia kutokana na nafasi zetu tunawawakilisha wananchi ambao hawana elimu, tuna wajibu wa kuwafundisha wasioelewa, wasiojua kusoma wala kuandika.”

Aliilaumu Serikali kwa kuipitisha Katiba hiyo mapema kabla haijaeleweka kwa wananchi.

Mufti anena

Mbali ya kutishia kususia mchakato wa kupitisha Katiba Inayopendekezwa, Sheikh Mkuu alisema Serikali haitatenda haki iwapo italiacha suala la Mahakama ya Kadhi mikononi mwa taasisi za kidini na kuitaka iitambue.
“Mbona CCM ililiweka hilo katika ilani ya uchaguzi mwaka 2010, halafu leo waseme kuwa wanatuachia wenyewe suala la Mahakama ya Kadhi? Hii si haki hata kidogo,” alisema Mufti Simba.

“Kama msimamo ndiyo huo basi sisi tutaendelea kuidai Mahakama ya Kadhi kama ambavyo tumekuwa tukisema siku zote na hatutaipigia kura hiyo katiba,” alisema alisema.

Kadhalika, alitaka Serikali kuacha kuliendesha suala la Mahakama ya Kadhi, ki- Bakwata Bakwata (Baraza Kuu la Waislamu wa Tanzania), bali ihusishe pia taasisi na jumuiya zote za Kiislamu ambazo zinawaunganisha Waislamu wote nchini.

Katika mkutano huo wa juzi, ulioandaliwa na Kamati ya Amani ya Mkoa wa Dar es Salaam na kuwashirikisha wajumbe mbalimbali wakiwamo viongozi wa dini za Kiislamu na Kikristo, Rais Kikwete alisema; “mwelekeo wa mambo hauhitaji uwe bingwa kujua hali hairidhishi, iwapo hatua hazitachukuliwa kutakuwa na uvunjifu wa amani wa kidini ambao moto wake ni mkali.” chanzo.Viongozi wa dini waiweka Serikali pabaya kuhusu Katiba Mpya - Kitaifa - mwananchi.co.tz

hawa viongozi wa dini kwa kweli kwa upande wangu nashindwa kuwaelewa kwamba hivi jukumu lao la msingi ni lipi? Kuwajenga wafuasi wao kiroho au kushiriki siasa?basi waanzishe chama na wakisajili,mie naomba kuwakumbusha kuwa jukumu lao la msingi ni kuwasaidia wafuasi wao kiroho na sikuwafundisha mambo haya yakusema kapigeni kura ya hapana wakati wa kura ya maoni kuhusu katiba inayopendekezwa,hatutaki kuamuliwa,tucheni tuamue wenyewe tunao utashi wa kuamua,kwa sasa tupeni muda tuisome katiba inayoendekezwa.tutafanya uamuzi sahihi kwa wakati muafaka,tutaipigia kura vzriiiiii............
 
Back
Top Bottom