Viongozi wa Dini wasipojua nyakati wanaweza kuchelewa kugundua wanaongozwa na siasa na sio Bibilia au Msahafu

Viongozi wa Dini wasipojua nyakati wanaweza kuchelewa kugundua wanaongozwa na siasa na sio Bibilia au Msahafu

mitale na midimu

JF-Expert Member
Joined
Aug 26, 2015
Posts
10,420
Reaction score
17,735
Trend inaonyesha licha ya kuwepo maagizo ya kidini kusambaza imani zao. Bado wanasiasa wa ulaya watafuta Mali wakiarabu waliwatangulia wana dini kusambaa duniani. Yaani walianza wapererezi wamisionary nao wakafuata. Wengi walijikuta wanasambaza dini kisiasa.

Wanasiasa walipoanza kuhimiza Elimu dunia kama kigezo cha kupata cheo kikubwa. Watu walianza kusoma Degree, PHD, Masters. Bila kujua watu wa dini nao wakafuata mkumbo wakaanza na hadi sasa wanapigana vikumbo katk vyuo wakitafuta hadhi za Elimu Dunia. Cheo kikubwa kidini hupimwa kwa kiwango cha Elimu dunia ya muhusika huku viongozi waasisi wa imani hawakumaliza hata STD 7. Hizi ideas walizitoa kwenye siasa.

Wanasiasa walipogeukia Ujasiliamali na kuwekeza ili kuleta maendeleo. Bibilia na misahafu nayo ilihafifishwa na msisitizo ukahamia huko ambao wana siasa wanasisitiza. Nimehudhuria Mkutano mmoja wa Imani. Mtoa neno alipofikia hatua ya kusisitiza kazi, alipaza sauti, akakomaa kuliko alipokuwa anasisitiza lengo kuu la neno lake. Cha ajabu kesho yake hadi magazeti ya kidini yaliandika huo msisitizo wa kazi kwa sababu ndio msisitizo wa wanasiasa awamu hii.

Kila dini inamalengo yake, inakauli mbiu zake na kusudi. Nawapa ushauri viongozi wa kidini rudini katika mizizi Yenu kwa mini mpo. Msisitizo ya wana siasa waachieni wanasiasa. Mmeifanya dini kuwa kitu chepesi ndio maana Wasanii, wanamichezo na wanasiasa wanatamani nao madhabahu na mimbari maana hata wao wanaona ni kazi rahisi.

Nimeanza kuwa makini hata na maombezi ya viongozi wa kidini katika vipindi hivi vya kampeni. Ikiwa makini unaweza kuokota vipisi vya sentensi za kisiasa katikati ya maombi hayo. Unaweza ukaona kampeni katikati ya maombi hayo. Unaweza kugundua kiongozi haongei na Mungu Bali anawapanga wasikizaji wa maombi hayo ili wamuamini mwanasiàsa anayegombea kama wanavyomuamini yeye.

Mwisho: Bibilia inatutaka tufanye dua na Sala kwa wafalme na wakuu ili kuwe na haki na Amani ktk nchi. (1timotheo 2:1-4). Msizidi hapo mkaanza kupamba watu au kuoshabongo za waumini ili wamuamini mtu fulani.
 
Usischokijua mwandishi ni kwamba, mf, hiyo Bible NDIYO iliyoiona hata Dunia unayoiishi leo na hata baada ya hii uliyopo leo,

Biblia NDIYO iliyoandika habari za elimu, biashara na namna Bora ya utawala Bora, mifumo ya serikari na haikusaza chochote!

Unaposema, eti siasa ndio inayohimiza Jambo jipya duniani unajidanganya Sana Mkuu, hakuna jipya Mkuu, yote yaliishaga asisiwa na Neno la Mungu yaani Biblia

Biblia ilikiona hata kizazi kilichopo leo, kizazi cha nyoka, kisichowatii wazazi Wao, chenye kujipenda, kisichotaka suluhu, kizazi kitukanaji kama siasa zilizopo leo, kuongezeka Kwa technology n.k

Zungumzia agenda nyingine usihusishe vitabu vya Mwenyezi Mungu kwenye hoja zako za kijinga Sawa?
 
Usischokijua mwandishi ni kwamba, mf, hiyo Bible NDIYO iliyoiona hata Dunia unayoiishi leo na hata baada ya hii uliyopo leo,

Biblia NDIYO iliyoandika habari za elimu, biashara na namna Bora ya utawala Bora, mifumo ya serikari na haikusaza chochote!

Unaposema, eti siasa ndio inayohimiza Jambo jipya duniani unajidanganya Sana Mkuu, hakuna jipya Mkuu, yote yaliishaga asisiwa na Neno la Mungu yaani Biblia

Biblia ilikiona hata kizazi kilichopo leo, kizazi cha nyoka, kisichowatii wazazi Wao, chenye kujipenda, kisichotaka suluhu, kizazi kitukanaji kama siasa zilizopo leo, kuongezeka Kwa technology n.k

Zungumzia agenda nyingine usihusishe vitabu vya Mwenyezi Mungu kwenye hoja zako za kijinga Sawa?
Asante kwa maoni Mkuu.
Watu wa imani wamekuwa na agenda na msisitizo yao katika kila zama.

Nakubaliana na wewe kuwa yote yamo ndani ya Bibilia. Ila mzizi wa hoja secular people wakianza kusisitiza Mtu wa imani na yeye anafuata. Hii trend IPO na watu hadi wameiandikia Vitabu kwa utafiti.

Mfano: Abraham alikuwa na Mission take.
Safari ya waislael ilikuwa na mission na objectives sake waliotoka nje waliishia jangwani.
Yesu alikuwa na mission yake. tena wakati wa Yesu kulikuwa na movements za kisiasa kuliko hizi lkn alijikita ktk mission yake.
Mitume walikuwa na mission yao.
Wazee wa kikristo nao
Mohammed alikuwa na mission yake.

Trend imebadilika kuanzia karne ya 19. Wengi wamepoteza identity yao na hata hawajui sababu kwa mini Wapo na utume wao ni nini ili wakite nguvu zao zote humo.

Matokeo ya hilo ombwe hata dini sasa zinaanza kuburuzwa na Popular opinions na secular agendas.

Dunia iliposisitiza Mazingira nao wanageuza agenda yao.

Dunia iliposisitiza Haki za wanawake nao wanaingia na hata kugombana.

Wanasiasa wanapostage agenda zao Nazo zinakuwa agenda na msisitizo mimbarini huku mission kuu ikibaki butu.
Udhaifu huu umefanya Wanasiasa kupenda kutumia dini kufikia watu kuliko hata Michezo ambazo zinawashabiki wengi pia. Kwa sababu kule kuna mianya ya kudivert usukani kuupeleka popote au kuzigeuza kama mbeleko za political popularity.


Uzi huu ni kengere kwa viongozi wa dini kurudi ktk mission zao kwa mini Wapo kwa mujibu wa katiba zao na usajiri wao.

Leo hata mwanasiasa akifanya jambo akifuatwa kiongozi wa dini na watu wa media lazima atoe maoni ya kisiasa wakati Yesu hata kama angefuatwa na wana siasa wa galilaya atoe maoni angwaambia wako makaisali wenzao kwenye maoni bora kuliko yeye akaendelea kuchapa injili
 
Dunia iliposisitiza Haki za wanawake nao wanaingia na hata kugombana.
Kwa maelezo haya, naanza kukuelewa mkuu, tofauti Kabisa na topic Ile ya awali,

Tofauti iliyopo, ni kushindwa kuyasimamia mambo ya madhabahuni ambayo hayana ushirika na awaye yote Ispokuwa ni Mungu na ufalme wake

Hata Yesu mwenyewe, hakuwai kutangaza kamwe mambo yasiyo ya ufalme wa mbinguni

Leo madhabahu zimekuwa zinawatangaza na kuwapigia Debe wafalme wa duniani, ni fedheha kubwa Kwa kweli, madhabahuni kupafanya ndio sehemu ya kumtangaza mtu ama kumpigia Debe mtu anayekuvutia?
 
Kwa maelezo haya, naanza kukuelewa mkuu, tofauti Kabisa na topic Ile ya awali,

Tofauti iliyopo, ni kushindwa kuyasimamia mambo ya madhabahuni ambayo hayana ushirika na awaye yote Ispokuwa ni Mungu na ufalme wake

Hata Yesu mwenyewe, hakuwai kutangaza kamwe mambo yasiyo ya ufalme wa mbinguni

Leo madhabahu zimekuwa zinawatangaza na kuwapigia Debe wafalme wa duniani, ni fedheha kubwa Kwa kweli, madhabahuni kupafanya ndio sehemu ya kumtangaza mtu ama kumpigia Debe mtu anayekuvutia?
Kufanya hivyo ni kunajisi madhabahu na mimbari.
Ni kuwadhihirishia waumini umepoteza dira
Na Mungu hana sehemu ktk hilo
 
Back
Top Bottom