Viongozi wa Kiafrika na Akili za Ki-Esau Esau

Viongozi wa Kiafrika na Akili za Ki-Esau Esau

Burkinabe

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2023
Posts
2,354
Reaction score
4,024
Asalaam Aleykum,

Mwanzo 27:1-46, Biblia inaelezea kisa cha mzaliwa wa kwanza wa Mzee Isaka (Isihaka) ambaye aliitwa Esau pamoja na mdogo wake Yakobo (Yakub).

Kulingana na mila na tamaduni za kipindi hicho, Esau alikuwa ni kiongozi automatically kwa maana ndiye alikuwa mzaliwa wa kwanza.

Kwa bahati mbaya sana kufupisha hiki kisa ni kwamba, Esau alijikuta ameuza uzaliwa wake wa kwanza (ambao uliambatana na majukumu ya kiuongozi) kwa mdogo wake (Yakobo) kutokana na njaa kali aliyokuwa nayo siku moja, kwa bakuli la kunde!

Ijapokuwa hiki kitendo kilifanyika kwa muda mfupi sana, lakini kilikuja kubadilisha kabisa hatma ya maisha ya Esau na uzao wake milele.

Biblia katika kitabu cha Waebrania 12:16,17 inaeleza kwamba Esau alikuja kujutia sana baadaye tena kwa machozi, lakini hakuweza tena kupata kile alichokipoteza kwa mlo mmoja tu.

Hivyo ndivyo walivyo viongozi wengi wa nchi za Kiafrika. Wako tayari kuuza au kumilikisha maliasili zenye rhamani kubwa sana kwa maslahi ya muda mfupi sana.

Hili hata halihitaji ufafanuzi kwa maana sote tunajua kile ambacho viongozi wa Kiafrika wamekuwa wanatoa in exchange of kondomu, kujengewa matundu ya vyoo, kujengewa madarasa, n.k.

Mungu awasaidie sana viongozi wa Kiafrika ili waweze kusahihisha makosa ambayo wamekuwa wakiyatenda kwa siku nyingi kama ambavyo Esau aliomba babaye ambariki walau kidogo.

Kwa sababu makosa yalishafanyika huko nyuma, hatuwezi kuendelea kukosea ilhali nafasi ya kujirekebisha ipo. Ukigundua umekosea njia, haina haja ya kuendelea mbele hata kama umeshatembea umbali mrefu, unatakiwa ugeuke nyuma na kurudi hadi pale ulipokosea, kisha uendelee na safari yako kwa njia sahihi.

Nawatakia wakati mwema.
 
Shirika la umeme Tanzania (TANESCO) limeshindwa kwenye kesi yake IPTL -Independent Power Tanzania Limited.

Hukumu hiyo imefikiwa mwisho wa wiki iliyopita ambapo World Bank tribunal (international centre for settlement of investment disputes.
ICSID imeamuru TANESCO kuilipa Standard Chartered Bank Hong Kong (SCB HK) kiasi cha dola za kimarekani milioni 148.40 pamoja na tozo riba.

SCB HK ndio walionunua mkopo wa IPTL kutoka bank ya Malaysia Danaharta kwa gharama ya dola za kimarekani milioni 76.1

Kwa habari zaidi soma the Guardian la leo:

My take.
Muda si mrefu tutasikia Tanzania yashindwa kesi na DP world yatakiwa kulipa trillioni 15.

Njia mpya iliyobuniwa na wajibu ndani ya serikali kuchota kodi za walala hoi, unasaini mkataba wa kijinga ambao ni kichaa tu anayeweza kuuvumilia alafu ukiulizwa unasema tumeshindwa kesi tulipeni tu.
 
Asalaam Aleykum,
Mwanzo 27:1-46, Biblia inaelezea kisa cha mzaliwa wa kwanza wa Mzee Isaka (Isihaka) ambaye aliitwa Esau pamoja na mdogo wake Yakobo (Yakub).

Kulingana na mila na tamaduni za kipindi hicho, Esau alikuwa ni kiongozi automatically kwa maana ndiye alikuwa mzaliwa wa kwanza.

Kwa bahati mbaya sana kufupisha hiki kisa ni kwamba, Esau alijikuta ameuza uzaliwa wake wa kwanza (ambao uliambatana na majukumu ya kiuongozi) kwa mdogo wake (Yakobo) kutokana na njaa kali aliyokuwa nayo siku moja, kwa bakuli la kunde!

Ijapokuwa hiki kitendo kilifanyika kwa muda mfupi sana, lakini kilikuja kubadilisha kabisa hatma ya maisha ya Esau na uzao wake milele.

Biblia katika kitabu cha Waebrania 12:16,17 inaeleza kwamba Esau alikuja kujutia sana baadaye tena kwa machozi, lakini hakuweza tena kupata kile alichokipoteza kwa mlo mmoja tu.

Hivyo ndivyo walivyo viongozi wengi wa nchi za Kiafrika. Wako tayari kuuza au kumilikisha maliasili zenye rhamani kubwa sana kwa maslahi ya muda mfupi sana.

Hili hata halihitaji ufafanuzi kwa maana sote tunajua kile ambacho viongozi wa Kiafrika wamekuwa wanatoa in exchange of kondomu, kujengewa matundu ya vyoo, kujengewa madarasa, kuruhusu mapenzi ya jinsia moja, n.k.

Mungu awasaidie sana viongozi wa Kiafrika ili waweze kusahihisha makosa ambayo wamekuwa wakiyatenda kwa siku nyingi kama ambavyo Esau aliomba babaye ambariki walau kidogo.

Kwa sababu makosa yalishafanyika huko nyuma, hatuwezi kuendelea kukosea ilhali nafasi ya kujirekebisha ipo. Ukigundua umekosea njia, haina haja ya kuendelea mbele hata kama umeshatembea umbali mrefu, unatakiwa ugeuke nyuma na kurudi hadi pale ulipokosea, kisha uendelee na safari yako kwa njia sahihi.

Nawatakia wakati mwema.
Yaani hawasomi kwa umakini ule msemo wa ..."akunyimae kunde hukupunguzia ...."?Hapo kwenye bakuli la kunde ni hatari sana.🤔
 
Shirika la umeme Tanzania (TANESCO) limeshindwa kwenye kesi yake IPTL -Independent Power Tanzania Limited.

Hukumu hiyo imefikiwa mwisho wa wiki iliyopita ambapo World Bank tribunal (international centre for settlement of investment disputes.
ICSID imeamuru TANESCO kuilipa Standard Chartered Bank Hong Kong (SCB HK) kiasi cha dola za kimarekani milioni 148.40 pamoja na tozo riba.

SCB HK ndio walionunua mkopo wa IPTL kutoka bank ya Malaysia Danaharta kwa gharama ya dola za kimarekani milioni 76.1

Kwa habari zaidi soma the Guardian la leo:

My take.
Muda si mrefu tutasikia Tanzania yashindwa kesi na DP world yatakiwa kulipa trillioni 15.

Njia mpya iliyobuniwa na wajibu ndani ya serikali kuchota kodi za walala hoi, unasaini mkataba wa kijinga ambao ni kichaa tu anayeweza kuuvumilia alafu ukiulizwa unasema tumeshindwa kesi tulipeni tu.
Tutashtakiwa MIGA.Achana na hayo.🤔
 
Asalaam Aleykum,
Mwanzo 27:1-46, Biblia inaelezea kisa cha mzaliwa wa kwanza wa Mzee Isaka (Isihaka) ambaye aliitwa Esau pamoja na mdogo wake Yakobo (Yakub).

Kulingana na mila na tamaduni za kipindi hicho, Esau alikuwa ni kiongozi automatically kwa maana ndiye alikuwa mzaliwa wa kwanza.

Kwa bahati mbaya sana kufupisha hiki kisa ni kwamba, Esau alijikuta ameuza uzaliwa wake wa kwanza (ambao uliambatana na majukumu ya kiuongozi) kwa mdogo wake (Yakobo) kutokana na njaa kali aliyokuwa nayo siku moja, kwa bakuli la kunde!

Ijapokuwa hiki kitendo kilifanyika kwa muda mfupi sana, lakini kilikuja kubadilisha kabisa hatma ya maisha ya Esau na uzao wake milele.

Biblia katika kitabu cha Waebrania 12:16,17 inaeleza kwamba Esau alikuja kujutia sana baadaye tena kwa machozi, lakini hakuweza tena kupata kile alichokipoteza kwa mlo mmoja tu.

Hivyo ndivyo walivyo viongozi wengi wa nchi za Kiafrika. Wako tayari kuuza au kumilikisha maliasili zenye rhamani kubwa sana kwa maslahi ya muda mfupi sana.

Hili hata halihitaji ufafanuzi kwa maana sote tunajua kile ambacho viongozi wa Kiafrika wamekuwa wanatoa in exchange of kondomu, kujengewa matundu ya vyoo, kujengewa madarasa, kuruhusu mapenzi ya jinsia moja, n.k.

Mungu awasaidie sana viongozi wa Kiafrika ili waweze kusahihisha makosa ambayo wamekuwa wakiyatenda kwa siku nyingi kama ambavyo Esau aliomba babaye ambariki walau kidogo.

Kwa sababu makosa yalishafanyika huko nyuma, hatuwezi kuendelea kukosea ilhali nafasi ya kujirekebisha ipo. Ukigundua umekosea njia, haina haja ya kuendelea mbele hata kama umeshatembea umbali mrefu, unatakiwa ugeuke nyuma na kurudi hadi pale ulipokosea, kisha uendelee na safari yako kwa njia sahihi.

Nawatakia wakati mwema.

Wataandika vitabu wakitoka madarakani kujutia, inakuwa imeisha hiyo.
 
Back
Top Bottom