Viongozi wa Manispaa ya Tabora wekeni Taa za Barabarani, muonekano wa Usiku Mitaani ni aibu

Torra Siabba

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2016
Posts
243
Reaction score
287
Wanajamvi, Leo naomba nilete kwenu giza hili la Tabora, kiukweli nimesikia mara kadhaa baadhi ya Viongozi wa Tabora kupiga kampeni ya kwamba, Tabora linatakiwa kuwa Jiji, kwa Giza hili hadhi ya jiji watapata wapi?

Viongozi wa Manispaa ya Tabora, Mkoa wa Tabora hili la Taa walichukue kama changamoto wahakikishe Taa zinawekwa na Mji unapendeza.

Taa za Barabarani ziko Ipuli pekee na baadhi ya maeneo ya Mjini lakini barabara ya kwenda kwa Mkuu wa Wilaya ni Giza, Barabara ya kwenda Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Kitete haina Taa.

Tunataka Mkoa ukue kimaendele, tuanze na vitu vidogo kama hivi ambavyo vinaonekana havina umuhimu, uwepo wa taa Barabarani unaweza saidia muonekano mzuri, unasaidia madereva na wapita njia, pia uwepo wa giza unaweza kuwa chanzo la kushawishi wahalifu kujificha kwenye maeneo hayo.

 
Humo gizani ni maficho ya wahuni kuna mtaa mmoja nilipita asubuhi nikakuta condom zimetupwa kwenye kujiwe cha boda
 
Kabla ya uhuru mji wa Tabora ulikuwa wa tatu baada ya Dar es Salaam na Tanga.
 
Hata Dar barabara nyingi hakuna taa.Barabara kama Ally Hassan Mwinyi /BagamoyoRD kuanzia posta mpaka bagamoyo huko ni giza tu
 
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…