Viongozi wa Serikali za Mtaa wanajichukulia poa hawafanyi majukumu yao stahiki

Viongozi wa Serikali za Mtaa wanajichukulia poa hawafanyi majukumu yao stahiki

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
525
Reaction score
1,257
Baadhi ya wakazi wa Kijiji cha Uchira, wilayani Moshi, mkoani Kilimanjaro, wamekusanyika kulalamikia uongozi wa serikali ya Kijiji hicho, kudaiwa kuuza maeneo ya barabara pasipo kuwashirikisha, hali inayowafanya kukosa njia za kwenda kutafuta huduma za kijamii.

Chanzo: ITV

*****

Nimesoma hiyo habari ikanikumbusha mazingira ya mtaani kwangu na mitaa mingine mingi tu ambayo nimewahi kuishi.

Kwa ufupi tangu nakua hadi hapa nilipofika nimeona vingozi wengi wa Serikali za Mtaa wanajiona wao ni wadogo n ahata jamii zetu zinazowazunguka zinawachukulia poa hivyohivyo.

Katika maisha kuna wakati jinsi utakavyojiweka ndivyo ambavyo watu wanaokuzunguka watakavyokuchukulia. Asilimia kubwa ya viongozi wa mtaa wao kazi yao kuuza viwanja na kuchukua posho ndogondogo.

Leo hii tuna matatizo kama ya Panya Road lakini kiuhalisia viongozi hao wa Serikali za Mtaa ndio wanatakiwa kuwa watu wa kwanza kubainisha matatizo ya mitaa yao na pengine kujua wahusika au kutoa mwangaza jinsi ya kudili na vikundi kama hivyo.

Hiyo ni kwao kuwa wao ndio wanaojua mitaa vizuri na wanajua wakazi wao wote, kama kuna mtu mwenye mishe za ajabu ajabu ni rahisi wao kumjua.

Kwa ufupi niseme hatuwatumii vizuri, tunawachukulia poa sana na ndio maana kuna uchafu mwingi nao pia wanauacha kwa kuwa wanaona siyo jukumu lao.
 
Wengi hawa kuchaguliwa na wananchi hivyo inakuwa ngumu kutekeleza majukumu yao mfano ni sehemu moja uko mkoa wa Rukwa Wilaya ya Nkasi kwa Wala vichwa vya samaki walikuwa wanawachana bila kupepesa macho "sisi hatukukuchagua kuwa kiongozi wetu"
 
Baadhi ya wakazi wa Kijiji cha Uchira, wilayani Moshi, mkoani Kilimanjaro, wamekusanyika kulalamikia uongozi wa serikali ya Kijiji hicho, kudaiwa kuuza maeneo ya barabara pasipo kuwashirikisha, hali inayowafanya kukosa njia za kwenda kutafuta huduma za kijamii.

Chanzo: ITV

*****

Nimesoma hiyo habari ikanikumbusha mazingira ya mtaani kwangu na mitaa mingine mingi tu ambayo nimewahi kuishi.

Kwa ufupi tangu nakua hadi hapa nilipofika nimeona vingozi wengi wa Serikali za Mtaa wanajiona wao ni wadogo n ahata jamii zetu zinazowazunguka zinawachukulia poa hivyohivyo.

Katika maisha kuna wakati jinsi utakavyojiweka ndivyo ambavyo watu wanaokuzunguka watakavyokuchukulia. Asilimia kubwa ya viongozi wa mtaa wao kazi yao kuuza viwanja na kuchukua posho ndogondogo.

Leo hii tuna matatizo kama ya Panya Road lakini kiuhalisia viongozi hao wa Serikali za Mtaa ndio wanatakiwa kuwa watu wa kwanza kubainisha matatizo ya mitaa yao na pengine kujua wahusika au kutoa mwangaza jinsi ya kudili na vikundi kama hivyo.

Hiyo ni kwao kuwa Thatwao ndio wanaojua mitaa vizuri na wanajua wakazi wao wote, kama kuna mtu mwenye mishe za ajabu ajabu ni rahisi wao kumjua.

Kwa ufupi niseme hatuwatumii vizuri, tunawachukulia poa sana na ndio maana kuna uchafu mwingi nao pia wanauacha kwa kuwa wanaona siyo jukumu lao.
That is quite true. Miezi sita or so iliyopita aliuawa kiongozi wa Mtaa anaitwa "Kevin" hapa Dar. Nilitazama zile kazi alizokuwa anafanya siku mbili tatu kabla ya kuuawa,na ikawa inanikumbusha sana kuhusu Sunna ya Mtume. Mambo yale yale unayoyasoma katika Hadith,huyu mtu ndiyo kazi yake ya kila siku. Yaani,hii migogoro midogo midogo inayotokea kati ya majirani kila siku. Huyu kajenga kibanda,kanifungia njia; huyu kaniuzia bidhaa,nimeenda pengine,nimeona Ile bidhaa inauzwa bei poa, basi,matatizo madogo kama hayo.
 
Swali ni Moja tu mbona hawana maisha Bora Kama ya hao walioko juu
 
Back
Top Bottom