UMUGHAKA
JF-Expert Member
- Sep 1, 2021
- 2,753
- 12,932
Usinchoshe na Nsikuchoshe,Tusichoshane!
Kwanza nikiri ya kwamba Mimi ni shabiki wa kutupwa wa Young Africans
Nikiwa kama mdau wa soka na mpenda maendeleo ya mpira,nimekuwa nikivutiwa na namna ambavyo soka letu limekuwa likioiga hatua,licha ya kucharuana,kutaniana na hata kuzodoana lakini linapokuja suala ukweli bila shaka huwa tunaambiana ukweli,Ukweli mara zote ndiyo umekuwa ukizisaidia timu kubwa hapa nchini kupiga hatua.
Napenda kukiri ya kwamba,Jezi ya watani zangu Simba SC a.k.a Makolo/Madunduka za msimu mpya 2024/2025 ni nzuri na zenye kiwango,Tatizo nililoliona ni neno "SANDA" kwenye jezi hizo.
Nimepata mashaka kidogo kama kweli hizi jezi viongozi waliziona kabla hazijatoka au zimetolewa kinyemela na wao wakiwa hawajazikagua!,Hivi kama kweli umeikagua jezi unawezaje kuruhusu ikatoka ikiwa na neno lenye ukakasi?
Yawezekana kabisa bwana Sunderland alikuwa na nia njema lakini Nia yake njema si Kwa namna hii,huu ni uhuni wa waziwazi Kwa timu kubwa kama Simba!
Kila mmoja anaelewa neno "SANDA" ni Vazi rasmi la Marehemu anapokuwa akizikwa,Sasa inakuwaje wakaruhusu neno "SANDA" likae kwenye jezi?,Ina maana wao hawaelewi maana ya SANDA?,Je hawaoni kama linaweza likawaletea uchuro kwenye msimu huu wa ligi?
Kuna msemo wa kiswahili usemao "Majina huumba"
Kwanini Sunderland asingeandika jina bland yake lote?,Kwanini afupishe?,kama nilivyosema,yawezekana alikuwa na maana nzuri lakini akumbuke hii nchi ya kiswahili,Kuna maneno yawezekana yakawa na maana nzuri nchi nyingine lakini hapa yakawa na maana mbaya!
Mfano
Kuna Mchezaji mzuri sana Simba walikuwa wakimtaka,alikuwa akiitwa Somebody Kapumbu,bila shaka Simba waliacha kumchukua kwasababu ya neno "KAPUMBU",yawezekana neno hilo likawa na maana nzuri kwao lakini si kwetu!
Nakumbuka pia Kuna balozi aliteuliwa nchi fulani kuja kuiwakilisha nchi yake hapa kwetu,akiitwa Somebody Kakuma,yawezekana neno "Kakuma" nchini kwake kusiwe na TAABU lakini nchini kwetu inaleta maana mbaya,hivyo nadhani Kwa busara za Viongozi wetu wakaomba aletwe mwingine!
Halafu pia Sunderland kwani kuna ulazima gani kuweka jina lako kwenye jezi,nani hajui jezi Kwa Sasa anatengeneza Sunderland?,mbona huwa hatuoni jina la Sheria Ngowi kwenye jezi za Yanga,nani asiyejua Ngowi ndiye mbunifu wa jezi za Yanga?
Hivyo niwaombe Viongozi wa Simba ikiwezekana hizo jezi zisiendelee kuuzwa,kama hii ni Batch ya kwanza,basi Batch ya pili zikitoka zisiwe na neno hilo!
Mkiendelea kukaza fuvu sisi watani zenu kazi yetu ni kuendelea kuwatania tu hatutakuwa na namna!
Yangu ni hayo tu leo
Kwanza nikiri ya kwamba Mimi ni shabiki wa kutupwa wa Young Africans
Nikiwa kama mdau wa soka na mpenda maendeleo ya mpira,nimekuwa nikivutiwa na namna ambavyo soka letu limekuwa likioiga hatua,licha ya kucharuana,kutaniana na hata kuzodoana lakini linapokuja suala ukweli bila shaka huwa tunaambiana ukweli,Ukweli mara zote ndiyo umekuwa ukizisaidia timu kubwa hapa nchini kupiga hatua.
Napenda kukiri ya kwamba,Jezi ya watani zangu Simba SC a.k.a Makolo/Madunduka za msimu mpya 2024/2025 ni nzuri na zenye kiwango,Tatizo nililoliona ni neno "SANDA" kwenye jezi hizo.
Nimepata mashaka kidogo kama kweli hizi jezi viongozi waliziona kabla hazijatoka au zimetolewa kinyemela na wao wakiwa hawajazikagua!,Hivi kama kweli umeikagua jezi unawezaje kuruhusu ikatoka ikiwa na neno lenye ukakasi?
Yawezekana kabisa bwana Sunderland alikuwa na nia njema lakini Nia yake njema si Kwa namna hii,huu ni uhuni wa waziwazi Kwa timu kubwa kama Simba!
Kila mmoja anaelewa neno "SANDA" ni Vazi rasmi la Marehemu anapokuwa akizikwa,Sasa inakuwaje wakaruhusu neno "SANDA" likae kwenye jezi?,Ina maana wao hawaelewi maana ya SANDA?,Je hawaoni kama linaweza likawaletea uchuro kwenye msimu huu wa ligi?
Kuna msemo wa kiswahili usemao "Majina huumba"
Kwanini Sunderland asingeandika jina bland yake lote?,Kwanini afupishe?,kama nilivyosema,yawezekana alikuwa na maana nzuri lakini akumbuke hii nchi ya kiswahili,Kuna maneno yawezekana yakawa na maana nzuri nchi nyingine lakini hapa yakawa na maana mbaya!
Mfano
Kuna Mchezaji mzuri sana Simba walikuwa wakimtaka,alikuwa akiitwa Somebody Kapumbu,bila shaka Simba waliacha kumchukua kwasababu ya neno "KAPUMBU",yawezekana neno hilo likawa na maana nzuri kwao lakini si kwetu!
Nakumbuka pia Kuna balozi aliteuliwa nchi fulani kuja kuiwakilisha nchi yake hapa kwetu,akiitwa Somebody Kakuma,yawezekana neno "Kakuma" nchini kwake kusiwe na TAABU lakini nchini kwetu inaleta maana mbaya,hivyo nadhani Kwa busara za Viongozi wetu wakaomba aletwe mwingine!
Halafu pia Sunderland kwani kuna ulazima gani kuweka jina lako kwenye jezi,nani hajui jezi Kwa Sasa anatengeneza Sunderland?,mbona huwa hatuoni jina la Sheria Ngowi kwenye jezi za Yanga,nani asiyejua Ngowi ndiye mbunifu wa jezi za Yanga?
Hivyo niwaombe Viongozi wa Simba ikiwezekana hizo jezi zisiendelee kuuzwa,kama hii ni Batch ya kwanza,basi Batch ya pili zikitoka zisiwe na neno hilo!
Mkiendelea kukaza fuvu sisi watani zenu kazi yetu ni kuendelea kuwatania tu hatutakuwa na namna!
Yangu ni hayo tu leo