the guardian 17
JF-Expert Member
- Aug 15, 2024
- 395
- 570
Viongozi wa Umoja wa Madereva wa Mabasi Tanzania (UWAMATA) Waomba Mazingira Rafiki ya Kazi
Viongozi wa Umoja wa Madereva wa Mabasi Tanzania (UWAMATA) wameiomba Serikali kuwawekea mazingira rafiki ya kufanya kazi zao ili kudumisha amani na kuchangia ukuaji wa uchumi wa taifa kupitia sekta ya usafirishaji.
Akizungumza na vyombo vya habari tarehe 11 Machi 2025, Mwenyekiti wa UWAMATA, Majura Kafumu, ameiomba Serikali kuhakikisha kuwa wafanyabiashara wadogo waliopo pembezoni mwa barabara wanapangiwa maeneo rasmi ili kupunguza hatari ya ajali na kurahisisha shughuli za usafirishaji.
Naye Katibu Mkuu wa UWAMATA, Abdallah Lubala, ameomba madereva waajiriwe kwa mikataba rasmi ili kuepuka visa vya kuachishwa kazi kiholela, jambo linaloathiri ustawi wao na usalama wa ajira zao.
Viongozi wa Umoja wa Madereva wa Mabasi Tanzania (UWAMATA) wameiomba Serikali kuwawekea mazingira rafiki ya kufanya kazi zao ili kudumisha amani na kuchangia ukuaji wa uchumi wa taifa kupitia sekta ya usafirishaji.
Akizungumza na vyombo vya habari tarehe 11 Machi 2025, Mwenyekiti wa UWAMATA, Majura Kafumu, ameiomba Serikali kuhakikisha kuwa wafanyabiashara wadogo waliopo pembezoni mwa barabara wanapangiwa maeneo rasmi ili kupunguza hatari ya ajali na kurahisisha shughuli za usafirishaji.
Naye Katibu Mkuu wa UWAMATA, Abdallah Lubala, ameomba madereva waajiriwe kwa mikataba rasmi ili kuepuka visa vya kuachishwa kazi kiholela, jambo linaloathiri ustawi wao na usalama wa ajira zao.